VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Katikati ya miaka ya 60,Nguli wa utunzi wa Vitabu na Lugha ya Kiswahili,Hayati Shaaban Robert alitunga Riwaya ya Kusadikika. Humo,akamtumia Waziri Mkuu Majivuno wa Kusadikika kama mhusika mkuu. Yumo pia kijana Adili ambaye alishtakiwa Barazani/Mahakamani kwa kuwa Mwalimu wa 'ukweli'. Kesi ya Adili ilikuwa ya kuwaambia watu ukweli. Mwisho mwishoni Adili alishinda. Kesi hii ya Kusadikika naifananisha na kesi wanayosukumiwa CHADEMA. Akina Majivuno wa CCM hawapendi ukweli unaofundishwa na CHADEMA. Watafanikiwa?