asakuta same
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 14,829
- 5,039
hapo jana trh 4/3/2011 chadema wamehitimisha awamu ya kwanza ya ziara yao ya ukombozi kanda ya ziwa.watanzania tumeshuhudia uungwaji mkono mkubwa kwa chadema kutoka kwa wananchi kiasi kwamba ccm ,mafisadi na vibaraka wao wamebaki kutapatapa.hii yote imetokana na watanzania kuchoka na utawala wa ccm na kujenga imani kubwa kwa cdm.
kimsingi imani ya umma wa tanzania kwa chadema haikuanza leo ,ilikuwepo toka ilipoonyesha uwezo wa kuwa na safu ya viongozi wenye uzalendo mkubwa ,uwezo mkubwa wa kujenga hoja zenye maslahi kwa umma ,kutoa fursa ya kiuongozi kwa vijana na zaidi ya yote kuwa na wabunge imara wakiongozwa na slaa kwenye bunge la tisa waliokuwa na uwezo usiotia shaka hata kidogo wa kusimamia maslahi ya watanzania ndani na nje ya bunge.
lakini pia ni ukweli usiopingika kwenye uchaguzi kumsimamisha mgombea urais(slaa)mwenye sifa zilizotukuka kwamfano kwa uchache wake ni mzalendo ,mpiga vita ufisadi ,mwadilifu ,uwezo wa kuthubutu ,jasiri ,mkweli ,muwazi ,ufahamu wa mambo mengi ,makini ,msomi n.k na zaidi kunadi ilani ya uchaguzi iliyojenga matumaini kwa watanzania waliowengi kulizidisha uhalali wa cdm kuwa tumaini jipya la watanzania ,mkombozi wa ukweli na suluhisho pekee la matatizo yao.
kwa niliyoyaeleza hapo juu napenda kutoa angalizo kwa cdm ,kwa kuwa upepo huu wa mabadiliko utawabeba wote wakiwemo wasiohusika ni muda muafaka kwa cdm kuja na
1.ITIKADI YA CHAMA.
2.KATIBA YA CHAMA ITAKAYOENDANA NA HAYA MABADILIKO.
3.DIRA YA CHAMA.
4.KUTEKELEZA KWA VITENDO CHADEMA NI MSINGI.
5.MPANGO MKAKATI WA KUIMARISHA CHAMA MPAKA NGAZI YA CHINI KABISA.
haya ni muhimu kwasababu siku zijazo wanapoelekea kushika hatamu kutahitajika timu kubwa ya watendaji mpaka ngazi ya chini kabisa karibu na wananchi kuwasaidiA kina DR. slaa kutimiza kile watanzania wanachokitarajia kutoka kwa cdm na kimsingi hawa watendaji ni lazima waandaliwe kwa msingi niliyoitaja hapo juu ili kupata watu waadilifu ,wazalendo ,wenye dhamira ya kweli ya kutatu matatizo ya watanzania n.k.
naomba kuwasilisha.
kimsingi imani ya umma wa tanzania kwa chadema haikuanza leo ,ilikuwepo toka ilipoonyesha uwezo wa kuwa na safu ya viongozi wenye uzalendo mkubwa ,uwezo mkubwa wa kujenga hoja zenye maslahi kwa umma ,kutoa fursa ya kiuongozi kwa vijana na zaidi ya yote kuwa na wabunge imara wakiongozwa na slaa kwenye bunge la tisa waliokuwa na uwezo usiotia shaka hata kidogo wa kusimamia maslahi ya watanzania ndani na nje ya bunge.
lakini pia ni ukweli usiopingika kwenye uchaguzi kumsimamisha mgombea urais(slaa)mwenye sifa zilizotukuka kwamfano kwa uchache wake ni mzalendo ,mpiga vita ufisadi ,mwadilifu ,uwezo wa kuthubutu ,jasiri ,mkweli ,muwazi ,ufahamu wa mambo mengi ,makini ,msomi n.k na zaidi kunadi ilani ya uchaguzi iliyojenga matumaini kwa watanzania waliowengi kulizidisha uhalali wa cdm kuwa tumaini jipya la watanzania ,mkombozi wa ukweli na suluhisho pekee la matatizo yao.
kwa niliyoyaeleza hapo juu napenda kutoa angalizo kwa cdm ,kwa kuwa upepo huu wa mabadiliko utawabeba wote wakiwemo wasiohusika ni muda muafaka kwa cdm kuja na
1.ITIKADI YA CHAMA.
2.KATIBA YA CHAMA ITAKAYOENDANA NA HAYA MABADILIKO.
3.DIRA YA CHAMA.
4.KUTEKELEZA KWA VITENDO CHADEMA NI MSINGI.
5.MPANGO MKAKATI WA KUIMARISHA CHAMA MPAKA NGAZI YA CHINI KABISA.
haya ni muhimu kwasababu siku zijazo wanapoelekea kushika hatamu kutahitajika timu kubwa ya watendaji mpaka ngazi ya chini kabisa karibu na wananchi kuwasaidiA kina DR. slaa kutimiza kile watanzania wanachokitarajia kutoka kwa cdm na kimsingi hawa watendaji ni lazima waandaliwe kwa msingi niliyoitaja hapo juu ili kupata watu waadilifu ,wazalendo ,wenye dhamira ya kweli ya kutatu matatizo ya watanzania n.k.
naomba kuwasilisha.