Paul Happe
New Member
- Jun 16, 2011
- 2
- 0
Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kimekuwa mstari wa mbele kutetea haki na maslahi ya mtanzania, hii ni kupitia hoja za wabunge wake bungeni, maandamano halali ambayo nguvu ya serikali huingilia kati na kuyaita haramu, vyombo vya habari na vijalida mbalimbali bila kusahau matumizi ya tekinolojia kama hii 'social network' ya jamii forum. Nawashangaa wafuasi wa chama cha kijani wakijaa juu kwa hoja ya kulinda amani, hapana..ukweli ni kuwa wanaogopa uwazi unaowekwa hadharani na Chadema hivyo wanadhani wanachonganishwa na wananchi. Hainingii akilini pale mbunge anaposema vurugu kwenye taasisi za elimu ya juu zinachangiwa na chadema kwa kuwa wanarubuni wanavyuo kugoma, bado haingii akilini, nadhani mwanafunzi wa chuo kikuu ana upeo mpana wa kuona hali halisi na kujuua ukweli ulipo.
CCM waache uwoga, hili ni jukwaa la siasa inabidi wagombane kwa kutumia hoja zilizo na tija na siyo zile potofu.
CCM waache uwoga, hili ni jukwaa la siasa inabidi wagombane kwa kutumia hoja zilizo na tija na siyo zile potofu.