CHADEMA mtumieni Jenerali Ulimwengu


Nani kakwambia CCM haifai kisera au kiitikadi? CCM ina itikadi nzuri na sera nzuri tu ila utekelezaji ni taabu kwa sababu ya maslahi binafsi kushika usukani kwenye kuendesha CCM. ndiyo maana watu kama Ulimwengu wapo wanakosoa ndani kwa ndani huku wakiwa na moyo kwamba CCM haina mbadala na mapambano yao ya kuielimisha CCM na kuuelimisha umma yataifanya CCM ifuate tena misingi yake.. Kazi ya ulimwengu haitaji kuwa kiongozi au mshauri wa chama chochote yeye kama mwanandishi na mwanaharakati anasema anachokiona na jamii inajifunza na kuamua mustakabali wa nchi..kadi yake ya kijani haikuhusu.
 
Hivi ule waraka wa Kikwete aliokua anauandika kwenye Raia Mwema bado unaendelea? Kwakua nilikua nausoma lakini sijui niliishia wapi kwakua ulikua ni waraka mrefu mno!
 
Mdondoaji na wengine,
Kuwa mshauri wa chama sio mpaka uwe na kadi, tujadili hoja iliyopo, habari za aliniambia kuwa anataka kujiunga CDM hazina mashiko hapa jamvini. Strike the point!
 

Kwanza kama na yeye ana ona umuhimu wa kuchangia ktk mabadiliko ya hii nchi basi aingie CDM, awe mwanachama then atapata hiyo hadhi ya kuwa mshauri wa CDM formally...otherwise uanachama wa kubembelezwa na ahadi za kupeana kazi hauna mashiko wala mantiki yoyote. Sidhani kama Prof Baregu na Prof Safari walishawishiwa kujiunga CDM, naamini walijiunga kwa matashi yao wenyewe...
Pamoja sana!!!!
 

Kumbuka sio wote wenye Kadi ya CCM wana mapenzi ya dhati na CCM ila mfumo na mazingira yanalazimu wawe nazo ili maisha ya kila siku yasiwe na bugudha, umeshawahi jiuliza CDM wanapata wapi taarifa za ndani za CCM? umeshawahi jiuliza CDM wanatoa wapi nyaraka za serikali na za CCM ili hali zilikuwa za siri sama?

Haya yoote yanathibitisha kuwa watu wamechoka na mfumo wa CCM ila hawawezi kuondoka au kujitoa kirahisi kama udhaniavyo ndio maana wanagawa nyaraka na habari muhimu kwa CDM ili wafanikishe mchakato wa kuiweka CCM Pembeni
 
Tuacheni Ushabiki wana JF swala la kuomba busara haijalishi kama ni wa chama gani kwan alichosema 'Akelu' ni kuchota Hekima na Busara zake tu Jenerali huo Ugamba wake umetoka wapi mbona mahela ya SABODO tunapokea nae ni Mwana Gamba Pure nadhan umefika wakati cdm kupokea ushauri kutoka kwa watu wenye hekima bila kujali wanatoka upande upi wa chama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…