Ningependa kuuliza kwa wanaJF wakubwa kwa wadogo waume na wake vijana na watoto ,hivi inakuwaje kumezuka watu humu JF ambao inaonekana kuwa ni wapenzi wa Chama Cha Chadema.Watu hawa wanakuwa na majibu ya matusi au ni lazima waandike matusi ,je hivi ndivyo Chadema ilivyo na ndio wanachama wake wanakuwa na midomo iliyojaa matusi.
Ingawa ukitazama watu hawa utaona hawazidi hata mwaka tangu wajiunge hapa JF ,wamezuka kama uyoga ,wao akili zao zinawatuma kuitetea Chama chao cha chedema kwa matusi au sijui tuseme ndio urithi wamerithi kwa wazazi wao au ukoo wao mzima.Kwani mambo mengine huwa ni ya kurithi na ndugu zetu hawa inaoeneka wanafuata wazazi wao,ingawa mimi siwaoni tenaa watu wa ajabu zaidi ya kuona ni tabia walizolelewa nazo lakini kama binadamu inabidi tukumbushane kuwa hapa sio pahala pa kutoa matusi ,mtu na matuzi yake abaki nayo hukohuko kwa wazazi wake.