Nesi mkunga
JF-Expert Member
- Nov 28, 2022
- 701
- 1,849
VIJANA WA CHADEMA AMUENI TUMALIZANE NA JAMBO MOJA KWANZA NDIO TUHAMIE LA PILI
Na Thadei Ole Mushi
Kwa miezi sita vijana wa Chadema wamebeba agenda tatu ambazo hawazifikishi mwisho. Walianza na katiba mpya wakaacha wakaelekea uelekeo wa Dubai kwenye hoja ya Bandari naona toka juzi jioni wameachana na Bandari wameelekea kwenye vichwa vya Treni.
FACT KUHUSU TRENI MNAYOIPONDA
Watanzania uacheni utani, naona mnataka vichwa vya train kama ya Shinkansen hili linawezekana kwa uchumi upi tulionao? Ni nchi 16 tu duniani zinatumia Shinkansen au Bullet Train ambao kwa baadhi ni Japan, China, Franch, Ujeruman nk.
Kwa sasa Train ya juu kabisa ukianchana na Shinkansen ni Maglev za China ambazo zina speed ya 431Km/h kwa maana ya kwamba ukiipanda kutoka Dar kwenda Moshi saa 12 asubuhi saa Moja utakwenda nyumbani kulala na mkeo hadi saa mbili kamili uingie kazini kwako na jioni utarudi tena nyumbani Saa kumi kamili utapumzika hadi saa 11 jioni utaipanda tena unarudi Dar na saa 12 jioni utakuwa unachoma utumbo wa ng’ombe kule Kimara. Hii ndio tunaitaka? Hizi shinkansen zinaanzia speed 210Km/h hadi speed 320Km/h ambazo zinatumiwa na nchi 16 tu kabla ya hili balaa la Maglev la China kuja ambalo ni speed 431Km/h.
Mzigo tulionunua sisi unatengenezwa na kampuni ya Kikorea inayoitwa Conglomerate Hyundai Rotem kwa Gharama Za USD 292 Milion ambazo ni sawa na 680,944,000,000 hii ni pesa nyingi sana.
Kampuni hii pia ndio ilitengeza mabehewa na vichwa vya treni katika nchi za Egypt, Tunisia, na Nigeria na zinafanya kazi vizuri tu.
Ni kweli hata mimi natamani taifa langu limiliki hizo Shinkansen lakini kwa kuwa najua uwezo wa taifa langu wala sipati shida . Hata nyumbani kwako kwa kuwa watoto wanajua uwezo wako hawakulinganishi na vitu anavyomiliki Mo au kina GSM. Jambo la Msingi la kupigia kelele kwa sasa Mama Samia atupatie ni Umeme wa uhakika, Maji, Uhakika wa Chakula na huduma bora za Afya na Elimu. Huko walipo Japan na Ujerumani Tutafika tu kwa kuwa Taifa huzaliwa hukuwa na hufa ni suala la Muda tu.
Niliwahi kuwaambia kuwa kati ya watanzania Milioni 60 wanaolipa kodi pale TRA ni Milioni tatu tu fuata link hii kuona walipa kodi ambao wapo registered na TRA
Hapa bado tuna misamaha kibao ya kodi kwenye bidhaa hasa kwenye bidhaa za kilimo, kwenye Afya magonjwa kibao tunatibiwa bure, kwenye Elimu bure nk kitu ambacho mataifa niliyotaja hapo juu hawana misamaha hiyo.
Haya tu assume Tumenunua hizo Shikansen ndugu zangu wasukuma na waha wataweza kulipia nauli yake? bei ya Hizo Shinkansen tukizitaka tutaacha mambo Mengine yote Kama kulipa Mishahara ya watumishi, tutaacha kununua Madawa, tutaacha miradi yote halafu tununue tren ya Sina hiyo tuwape waliguru waje Dar na Kurudi Moro kwa Dakika 40 halafu akifika anaenda bar anamsubiria Shemeji au Mjomba kwa masaa matatu aje amchukue. Nafikiri tupate mahitaji ya msingi kwanza halafu hayo mengine yatakuja.
Hata Maslow's katika nadharia hierarchy of needs anatutaka tuwe na mahitaji ya msingi kwanza kabla ya kutaka mambo mengine yaani bado taifa linapambana na kaya Masikini halafu tunataka Anasa?
Hata JPM aliponunua zile Ndege Upinzani waliponda kuwa ametununilia mapangaboi leo hii tunazipanda wote. Upinzani sio kuondoa akili zote kichwani na kupinga kila kitu.
FACT KUHUSU WATUMISHI
Kwa watumishi watanielewa zaidi kuwa kama kuna utawala wa kukumbukwa katika kushughulika na Stahiki zao basi Rais Samia ndiye Champion katika hili. Ni mtumishi gani wa umma mwenye uthubutu wa kumyoshea Rais Samia Kidole? Tunakumbuka alikotutoa ambao kuna watu walikaa hadi miaka 8 bila kupanda Daraja la Mshahara, leo kwa kipindi cha Miaka miwili kafuta Makosa yote ya watangulizi wake kuhusu mishahara. Kama kuna mtumishi hamwelewi katika hili basi atakuwa ameamua kumuonea hili la Nyongeza ni kitu kidogo sana tumwamini.
Turudini kwenye Bandari kwanza hatujamalizana au mmeshaelewa? Tumpe Mama Muda anaitengeneza nchi….
Na Thadei Ole Mushi
Kwa miezi sita vijana wa Chadema wamebeba agenda tatu ambazo hawazifikishi mwisho. Walianza na katiba mpya wakaacha wakaelekea uelekeo wa Dubai kwenye hoja ya Bandari naona toka juzi jioni wameachana na Bandari wameelekea kwenye vichwa vya Treni.
FACT KUHUSU TRENI MNAYOIPONDA
Watanzania uacheni utani, naona mnataka vichwa vya train kama ya Shinkansen hili linawezekana kwa uchumi upi tulionao? Ni nchi 16 tu duniani zinatumia Shinkansen au Bullet Train ambao kwa baadhi ni Japan, China, Franch, Ujeruman nk.
Kwa sasa Train ya juu kabisa ukianchana na Shinkansen ni Maglev za China ambazo zina speed ya 431Km/h kwa maana ya kwamba ukiipanda kutoka Dar kwenda Moshi saa 12 asubuhi saa Moja utakwenda nyumbani kulala na mkeo hadi saa mbili kamili uingie kazini kwako na jioni utarudi tena nyumbani Saa kumi kamili utapumzika hadi saa 11 jioni utaipanda tena unarudi Dar na saa 12 jioni utakuwa unachoma utumbo wa ng’ombe kule Kimara. Hii ndio tunaitaka? Hizi shinkansen zinaanzia speed 210Km/h hadi speed 320Km/h ambazo zinatumiwa na nchi 16 tu kabla ya hili balaa la Maglev la China kuja ambalo ni speed 431Km/h.
Mzigo tulionunua sisi unatengenezwa na kampuni ya Kikorea inayoitwa Conglomerate Hyundai Rotem kwa Gharama Za USD 292 Milion ambazo ni sawa na 680,944,000,000 hii ni pesa nyingi sana.
Kampuni hii pia ndio ilitengeza mabehewa na vichwa vya treni katika nchi za Egypt, Tunisia, na Nigeria na zinafanya kazi vizuri tu.
Ni kweli hata mimi natamani taifa langu limiliki hizo Shinkansen lakini kwa kuwa najua uwezo wa taifa langu wala sipati shida . Hata nyumbani kwako kwa kuwa watoto wanajua uwezo wako hawakulinganishi na vitu anavyomiliki Mo au kina GSM. Jambo la Msingi la kupigia kelele kwa sasa Mama Samia atupatie ni Umeme wa uhakika, Maji, Uhakika wa Chakula na huduma bora za Afya na Elimu. Huko walipo Japan na Ujerumani Tutafika tu kwa kuwa Taifa huzaliwa hukuwa na hufa ni suala la Muda tu.
Niliwahi kuwaambia kuwa kati ya watanzania Milioni 60 wanaolipa kodi pale TRA ni Milioni tatu tu fuata link hii kuona walipa kodi ambao wapo registered na TRA
VIDEO: Imetajwa idadi ya wanaolipa kodi TRA kati ya Watanzania mil 45 - Millard Ayo
Kama unakumbuka Serikali ya awamu ya tano ilianza kwa kampeni ya "dai risiti" unaponunua bidhaa na hata wafanyabiashara ambao walikuwa wanakwepa kulipa kodi nao walibanwa ili kulipa na ambao hawakufanya hivyo walifikishwa mahakamani Leo Kamishna wa mamlaka ya mapato Tanzania 'TRA', Alphayo...
millardayo.com
Hapa bado tuna misamaha kibao ya kodi kwenye bidhaa hasa kwenye bidhaa za kilimo, kwenye Afya magonjwa kibao tunatibiwa bure, kwenye Elimu bure nk kitu ambacho mataifa niliyotaja hapo juu hawana misamaha hiyo.
Haya tu assume Tumenunua hizo Shikansen ndugu zangu wasukuma na waha wataweza kulipia nauli yake? bei ya Hizo Shinkansen tukizitaka tutaacha mambo Mengine yote Kama kulipa Mishahara ya watumishi, tutaacha kununua Madawa, tutaacha miradi yote halafu tununue tren ya Sina hiyo tuwape waliguru waje Dar na Kurudi Moro kwa Dakika 40 halafu akifika anaenda bar anamsubiria Shemeji au Mjomba kwa masaa matatu aje amchukue. Nafikiri tupate mahitaji ya msingi kwanza halafu hayo mengine yatakuja.
Hata Maslow's katika nadharia hierarchy of needs anatutaka tuwe na mahitaji ya msingi kwanza kabla ya kutaka mambo mengine yaani bado taifa linapambana na kaya Masikini halafu tunataka Anasa?
Hata JPM aliponunua zile Ndege Upinzani waliponda kuwa ametununilia mapangaboi leo hii tunazipanda wote. Upinzani sio kuondoa akili zote kichwani na kupinga kila kitu.
FACT KUHUSU WATUMISHI
Kwa watumishi watanielewa zaidi kuwa kama kuna utawala wa kukumbukwa katika kushughulika na Stahiki zao basi Rais Samia ndiye Champion katika hili. Ni mtumishi gani wa umma mwenye uthubutu wa kumyoshea Rais Samia Kidole? Tunakumbuka alikotutoa ambao kuna watu walikaa hadi miaka 8 bila kupanda Daraja la Mshahara, leo kwa kipindi cha Miaka miwili kafuta Makosa yote ya watangulizi wake kuhusu mishahara. Kama kuna mtumishi hamwelewi katika hili basi atakuwa ameamua kumuonea hili la Nyongeza ni kitu kidogo sana tumwamini.
Turudini kwenye Bandari kwanza hatujamalizana au mmeshaelewa? Tumpe Mama Muda anaitengeneza nchi….