KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,149
Kwa takriban wiki 3 au 4 sasa kumekuwapo na sintofahamu huko kusini mwa Tanzania eneo linaloaminika kwamba liko nyuma kidogo kimaendeleo hapa nchini,sintofahamu hiyo imetokana na kugundulika kwa gesi kwenye eneo hilo..gesi ambayo serikali kuu ingependa kuona inaifadisha nchi nzima ikiwemo mikoa ya kaskazini hususan Kilimanjaro na Arusha lakini kwa namna moja ama nyingine wakazi wa maeneo hayo ya kusini kulikopatikana gesi wamekua na mtazamo tofauti, wao wangependa gesi hiyo iwe yao peke yao!
swali langu kwa vyama vya upinzani hususan chama kikuu cha upinzani bila shaka CHADEMA,je wao wanawaambia ama wanawaahidi nini wana kusini kama kwa mfano leo wanaachiwa nchi waienedeshe wao CCM ikae pembeni kama mtazamaji...je watakubaliana na wana Mtwara gesi iwe yao peke yao na kuwaudhi watu wa kaskazini,ziwa,mashariki na kwingineko ambao rasilimali zinazopatikana kwao wamekua wakishare na watu wa nchi nzima wakiwemo watu wa Mtwara????
Nawasilisha but naomba tuwe fair tu kwenye kuchangia hapa,ushabiki kupita kiasi wa vyama tuuweke pembeni,tujikite zaidi kwenye facts.
asanteni sana.
swali langu kwa vyama vya upinzani hususan chama kikuu cha upinzani bila shaka CHADEMA,je wao wanawaambia ama wanawaahidi nini wana kusini kama kwa mfano leo wanaachiwa nchi waienedeshe wao CCM ikae pembeni kama mtazamaji...je watakubaliana na wana Mtwara gesi iwe yao peke yao na kuwaudhi watu wa kaskazini,ziwa,mashariki na kwingineko ambao rasilimali zinazopatikana kwao wamekua wakishare na watu wa nchi nzima wakiwemo watu wa Mtwara????
Nawasilisha but naomba tuwe fair tu kwenye kuchangia hapa,ushabiki kupita kiasi wa vyama tuuweke pembeni,tujikite zaidi kwenye facts.
asanteni sana.