CHADEMA Mkoa wa Singida chaungana na wenzao Arusha!

CHADEMA Mkoa wa Singida chaungana na wenzao Arusha!

ADRIAN

Senior Member
Joined
Dec 31, 2012
Posts
113
Reaction score
27
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO - CHADEMA Mkoa wa Singida kinaungana na wana-Arusha katika kukumbuka mauaji ya kinyama kwa vijana wetu yalitekelezwa na jeshi la polisi tarehe 05/01/2013 waliokuwa wakipinga ukiukwaji wa sheria na kanuni zilizomuingiza meya wa jiji hilo Gaundence Lymo.
Tuendelee kuwakumbuka na naamini walipolala wanazidi kuiombea Chadema ili izidi kupigania haki za watanzania wenzao bila kuchoka. Kwa nguvu ya pamoja tutaishinda dhuluma, udikteta, unyonyaji, ukiukwaji wa haki nk.

Pamoja na salamu za Chadema,

Imetolewa na:

MUTTA, Anselimi

katibu mwenezi Chadema - Singida.
 
tunashukuru kwa kumbukizi hz kwani daima kivuli cha wenye haki huishi daima,hvyo ndivyo damu yao itasambaa na kuleta ukombozi mwa wananch wa tanzania wenye rasilimali lukuki lakini zisizo wasaidia .pia wasingida msivunjwe moyo na propaganda za mafisadi kwa lengo la kuvuruga mwelekeo wa ukomboz,ccm lengo lao ni kuzipa masikio watanzania wasipate mwanga wa ukombozi,viva chadema kutetea wanyonge,
 
Tunawashukuru sana kwa ushirikiano wenu kwetu sisi wana wa Arusha muendelee kuwa na moyo huo wa kujali na uzalendo
 
Back
Top Bottom