CHADEMA Mkituangusha hatutawasamehe

CHADEMA Mkituangusha hatutawasamehe

Kigarama

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2007
Posts
2,492
Reaction score
1,238
Ikifika mwaka 2015 itakuwa ni miaka 20 kamili imepita tangu kufanyika kwa uchaguzi wa kwanza ulioshirikisha vyama vingi mwaka 1995 tangu kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi uliokuwa umepigwa marufuku miaka 30 kabla, yaani mwaka 1965. Kwenye uchaguzi wa mwaka 2015 inaonekana mchuano utakuwa kati ya CHADEMA na CCM.

Kwenye mazoezi na mechi za utangulizi (Chaguzi ndogo) CCM inaonekana kuzidiwa kwa kupunguziwa viti ilivyokuwa inavishikilia kuanzia ngazi ya vitongoji hadi kwenye ubunge na CHADEMA ikiongeza idadi ya viti vyake sehemu mbalimbali za nchi.

Lakini kwenye uchaguzi wa mwakani ni uchaguzi ambao hautatoa nafasi kwa chama chochote kile kutumia viongozi wa kitaifa au maarufu kufanya kampeni nchi nzima. Uchaguzi wa serikali za mitaa kampeni zake hufanyika kwa siku saba tu. Na chaguzi hizo kwa uzowefu hukabiliwa na dosari nyingi (irregularities) sana na rafu (Rigging) za kutisha. Na ili kukabiliana na dosari na Rafu hizo CHADEMA inatakiwa kuwa na mtandao mpana wa chama ulio Imara.

Toka leo hadi uchaguzi wa mwakani inahitaji juhudi za ziada kujenga mtandao Imara wa chama. Na ujenzi wa mtandao huo huitaji sana fedha ambazo naamini CHADEMA hawanazo. Ule mpango wa kuichangia CHADEMA kwa njia ya simu sijui umeishia wapi? Ilitakiwa kila mwezi angalau wananchi wengejulishwa ni kiasi gani kimekusanywa ili kujenga hamasa na kufanya wanachama wenyewe wajitathimini ni kwa kiasi gani wanachangia chama chao. Bila fedha (Halali lakini) hakuna siasa endelevu kwa vyovyote vile.

CHADEMA inahitaji zaidi ya watu lakini moja kuwa wagombea kwa upande wake kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na maelfu mengine kwa ajili ya mawakala. Nguvu kazi hiyo na wagombea hao ni lazima wawe wametayarishwa tangu mwaka huu na wala si mwakani wakati wa uchaguzi.

Kuna kazi ya msingi ya kufanya kabla ya uchaguzi wa mwakani kama ndiyo msingi wa ushindi kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2015. CHADEMA Msituangushe.
 
Kuna kazi kubwa inayo takiwa kufanyika makao makuu kwanza, chuki za viongozi zimezidi, mpaka kufikia kutoana roho.
 
Kuna kazi kubwa inayo takiwa kufanyika makao makuu kwanza, chuki za viongozi zimezidi, mpaka kufikia kutoana roho.

Kama kawaida yenu,mshaanza kularua...nje kabisa ya mada.
 
hapo kweli pana kazi ila imani yangu kwa cdm ni kubwa tujitahidi kutoa ushauri ambao ni positive kwa chama
 
:rockon: Ndugu zangu wanaotoka mkoa wa singida,wilaya ya Manyoni naombeni tutafutane tukafungue ofisi ya cdm maeneo ya KINTINKU mpakani mwa Dodoma na singinda,mwezi wa sita tarehe tutangaza,samahani kwa kuingilia mada kati wa jf
 
Ni kweli kabisa, kuna ambao hawawezi kufika vijijini lakini wanauwezo na nia ya kuwawezesha wengine ili waweze kufika huko....team work!!
 
lakin yeye alishakanusha zzk kuwa hayo ni maneno ya vjana waliofukuzwa.
 
2015 it's not who vote that count ... It's who count the votes... Bila tume Huru na ya Haki ... CDM itahesabu Maumivu ... Kazi Sasa iwe kuakikisha tume Huru inapatikana .. Mengine ni mbwembwe tu
 
2015 it's not who vote that count ... It's who count the votes... Bila tume Huru na ya Haki ... CDM itahesabu Maumivu ... Kazi Sasa iwe kuakikisha tume Huru inapatikana .. Mengine ni mbwembwe tu

Wewe umesema Mkuu, hapa kinachotakiwa ni free and fair elections.
 
Kumnyang'anya CCM TONGE mdomoni si kazi rahisi yuko tayari kupigana ili asipokonywe TONGE au ulaji. CHADEMA inahitaji maarifa zaidi ili iweze fanikiwa katika hili. Nahisi harufu ya damu 2015.
 
Kuna kazi kubwa inayo takiwa kufanyika makao makuu kwanza, chuki za viongozi zimezidi, mpaka kufikia kutoana roho.

Nani katolewa riho tena na nani?? Hii habari mpya wapelekee Policcm wafungue jalada la ugaidi.
 
PRESS RELEASE: 'SIRI YA KUUAWA ZITTO'-SIO KWELI
wp.me'SIRI YA KUUAWA ZITTO' Katika gazeti la Mtanzania toleo na. 7269 la Jumatano Machi 27, 2013 kuna habari yenye kichwa chenye maneno ' SIRI YA KUUAWA ZITTO YAFICHUKA' na vichwa vidogo ‘yadaiwa ilipan...

Kumbe unazungumzia habari ile ya TP mtanzania. tafuta vyanzo vya habari vya kusoma habari zake sio hizo TP za ccm.
 
Chadema hawana sifa za kuongoza dola huo ndiyo ukweli.
 
Kuna kazi kubwa inayo takiwa kufanyika makao makuu kwanza, chuki za viongozi zimezidi, mpaka kufikia kutoana roho.
Ni kweli zinazidi zile za CCM; lakini M4C tayari imeiva kwa hiyo itawahusu wapiga kura kwenye maeneo yao na siyo makao makuu na ndiyo demokrasia.
 
2015 it's not who vote that count ... It's who count the votes... Bila tume Huru na ya Haki ... CDM itahesabu Maumivu ... Kazi Sasa iwe kuakikisha tume Huru inapatikana .. Mengine ni mbwembwe tu

Kuhusu tume huru na ya haki chini ya utawala wa CCM sahau unachotakiwa ni kuilinda Kura yako.
 
Chadema hawana sifa za kuongoza dola huo ndiyo ukweli.
Kama kuongoza dola ni maamuzi ya Lumumba ni kweli maneno yako, lakini ni kama kura halali wapiga kura watalinda kura zao na atakaeshika dola ni yule atakaepewa ridhaa na wananchi.
 
Ili ushindi upatikane ni lazima Chadema ifike kila kona ya nchi , wananchi wapewe elimu ya uraia kwa kasi, muda unazidi kwisha
 
Back
Top Bottom