CHADEMA mkitaka jifunzeni katika mambo haya

CHADEMA mkitaka jifunzeni katika mambo haya

lonesome

Senior Member
Joined
Oct 10, 2010
Posts
195
Reaction score
66
MIMI NI MTU HURU AMBAYE AKILI YANGU HAIJAGHOSHIWA NA ITIKADI YA CHAMA CHOCHOTE. NI MTANZANIA MWENYE MAPENZI NA TANZANIA.

CHADEMA wakati mnahangaika namna gani ya kulizima jambo la video ya Lwakatare wao CCM wanapanga mikakati ya kuwaingiza watu wao katika mabaraza ya wawakilishi wa mchakato wa katiba mpya kwenda kupeleka hoja za CCM, nyie CHADEMA mnahangaika na Mwigulu Nchemba na Lwakatare.

Kama hamtaki kukubali ulizeni wagombea waliogombea nafasi hizo ambao hawakuwa CCM namna walivyoshindwa si kwa hoja bali vioja, nyie mmepewa TOY mchezee wao wameshasonga mbele wakiendelea na mikakati yao mkija kushtuka mmmeachwa nyuma sana. Hii ndiyo siasa.

CHADEMA mna kazi kubwa ya kukifanya chama kisimame na kiwe na miiko na demokrasia pasipo kuifinya demokrasia. Kwa hili mnapaswa kuamini kuwa katika kukijenga chama si watu waote wanatakiwa wadumishe fikra za mwenyekiti au watu flani.

Chukuen changamoto na hoja za wanachadema wanaopinga mambo flani kukijenga chama si kuwaona kama wapinzani ili mradi wanapinga katika vikao vya chama. Nyie kila atakayepinga jambo flani mnamwona ni CCM mnakibomoa chama chenu maana hawa watu wanatoka na siri nzito za kukiangamiza chama.

CCM hawana muda sana wa kuzungumzia sauala la Lwakatare,CHADEMA ndo mmekuwa mkihangaika sana hasa kwenye gazeti lenu la TANZANIA DAIMA kila siku.Hii inawapotezea muda subiri mahakaman iamue na msitoe toe matamko yasiyo ya kisayansi sana sana thibitishen kuwa video ile ni feki.

Hebu tuoneshen utaalamu huo kwa kuajaribu kutengeneza video moja ya mtu mmoja wa CCM mkaipandikizia maneno ili watanzania sasa wajue mbivu na mbichi.

HII NDIYO SIASA, ADUI YENU SI CCM ILA NI MFUMO MBOVU AMBAO NANYI TARATIBU MNAUKUMBATIA.
 
Bora umesema wewe. Hawa watu hawapendi kabisa kuambiwa. Sasa hivi watasema umetumwa. Ngoja uone!
 
Tanzania kuna vyama vingapi ya siasa? Mleta mada acha upuuzi wa kutokufikiri. Unadhani kwa mawazo yako finyu na usivyoelewa mchakato wa kuwapata wajumbe wa mabaraza ya katiba. Nianze tu kukueleza, mkuu wa wilaya ni CCM, asilimia kubwa ya madiwani ni CCM, asilimia kubwa ya wenyeviti wa mitaa na vijiji ni CCM, mwisho watendaji wote wa mitaa/vijiji na kata mwajiri wao ni CCM (Mkugenzi). Kwa maelezo hayo jibu lake hata ukimuuliza mtoto wangu wa Nursery school jibu anakupa bila wasi wasi.
 
Bora umesema wewe. Hawa watu hawapendi kabisa kuambiwa. Sasa hivi watasema umetumwa. Ngoja uone!

Maoni ya mtu binafsi kwenye mtandao isichukuliwe kuwa ndio tamko la chama ingekuwa viongozi wa chadema ndio wanakuja hapa na kukashifu kila wanachoambiwa basi tungejua kuwa chadema huwa hawapendi kuambiwa.

Lakini hatujui ni kwakiasi gani chama kinayachukua maoni ya watu na kuyafanyia kazi.

Hata hivyo huwezi kutegemea kuongoza chama kwa kutegema maoni ya kwenye mitandao ya jamii.

Swala la kusema kuwa hawa watu hawapendwi kuambiwa ni swala la kiujumla mno na haijajulikana unamlenga nani.

Ila kaa ukijua huku kwenye mtandao kuna kila aina ya akili yaani kuanzia mulungo mpaja msigwa (yaania akili ndogo na akili kubwa zinaongozwa na akili ndogo)
 
Kama ulivyosema kuwa chadema wako bize na ishu ya Lwakatare ni kweli na sababu kubwa ni kwamba kama ile video itakua imetengenezwa kama inavyosemekana basi lengo la m/watengenezaji ni kukichafua chama mbele ya umma, sasa cdm wakikaa kimya umma utaamini kuwa ni kweli ndy maana chama kimewaachia wansheria kushughulika nalo mpaka kieleweke.

CHADEMA hawana sababu ya kutengeneza video ili ndy umma ujue kama video ya Lwakatare imetengenezwa umeshasema mahakama ndiyo itaamua na kama umefuatilia vizuri msemaji wa chama kwenye jambo hilo amesema wanaimani na jaji aliyeteuliwa kwa maana hiyo wanaimani na mahakama pia na haki itandeka.

Mabaraza ya katiba sio ya chama kwasababu katiba inayotengenezwa ni ya Tanzania siyo katiba ya CHADEMA wala ya CCM sasa kama hayo madai yako yana ukweli basi tatizo liko kwa wananchi wenyewe kuzembea na kukubali mustakabali wao kuamuliwa na ccm kwa kupandikiza mamluki kwenye hayo mabaraza na mwisho wa siku katiba ikiwa mbovu itatugharimu wote kama taifa.

Umesema unasubiri matusi kutoka kwa wana chadema hii ni kwa sababu unajua kabisa ulichokisema hapa huna uhakika nalo na umekisema ili uskie watachangia nn ila kwa wanaokujua na lengo lako kusema uliyoyasema lazima wakutukane. Na watao kutuna sio cdm huenda wakawa hata CCM maana uzi wako umewagusa CCM kuliko CHADEMA.
 
MIMI NI MTU HURU AMBAYE AKILI YANGU HAIJAGHOSHIWA NA ITIKADI YA CHAMA CHOCHOTE. NI MTANZANIA MWENYE MAPENZI NA TANZANIA.

CHADEMA wakati mnahangaika namna gani ya kulizima jambo la video ya lwakatare wao CCM wanapanga mikakati ya kuwaingiza watu wao katika mabaraza ya wawakilishi wa mchakato wa katiba mpya kwenda kupeleka hoja za CCM. nyie CDM mnahangaika na Mwigulu nchemba na Lwakatare. hii ndo siasa.

kama hamtaki kukubali ulizeni wagombea waliogombea nafasi hzio ambao hawakuwa CCM namna walivyoshindwa si kwa hoja bali vioja. nyie mmepewa TOY mchezee wao wameshasonga mbele wakiendelea na mikakati yao. mkija kushtuka mmmeachwa nyuma sana. hii ndiyo siasa.

Mkuu ushauri wako ni mzuri!!.. Jambo hili halikuletwa na CCM kubadilisha mwelekeo wa katiba mpya bali kufunika njama za kumdhuru KIBANDA na kui-demonize CDM!..

Hii propaganda ya Lwakatare haiwezi kamwe kunyamaziwa kimya kwakuwa madhara yanaweza kumtokea mhusika na njama hizo kuendelea kufanyika kwa wengine.
 
Ushauti mwafaka lakini yu pale unaposema CHADEMA watengeneze video ya kionbozi wa CCM akipanga mabaya. Ushauri huu si sahihi kwani unawaeleza wavunje sheria ambayo unajua madhara yake. Dhambi haitatuliwi kwa kufanya dhambi inbhine mkuu. Halavu huitaji kuanza kwa kujitambulisha kuwa wewe si mfuasi wa chama chochote vha siasa. siyo kosa kuwa mguasi wa chama na hii haikuondolei kushahuri ikiwa tu ushauri huo ni wa dhati na si wa kinafiki.
 
Wafuasi wa CHADEMA itakua ni chanzo cha kutotawalika baada ya uchaguzi mkuu hujao.
Maana wana matumaini makubwa sana kwamba watashika dola uchaguzi mkuu ujao,hizi ni sawa na ndoto za saa7 mchana,sasa kwa akili hizi za kushikiwa nadhani nchi haitatawalika kabisaaaaaa!
Ewe muumba wa mbingu na ardhi niepushe mimi na watanzania wenzangu kwa hili sekeseke ili yasijetukuta yale ya 'kimbali'
 
150419_355026611263437_1951252696_n.jpg

Itatawalika tu, USIHOFU
 
kama na wewe hujashikiwa akili zako basi nadhani ni mmoja wa zao la Mulugo. Matatizo yapo kote tu hasa ukiwa makini ktk kuangalia bunge linaloendelea dodoma, bunge lote kuanzia meza kuu kwa spika ni dhaifu,wabunge wa upinzani ndio usiseme, chama tawala wao wamekuwa kama wehu vile. Wale wooote wanaogeuza bunge kijiwe cha stori hasa matusi nadhani waishi kwa matumaini 2015 haingii m2 bungen. Bora tuwe na utawala wa dictatorship kuliko uhuru tulionao sasa.

Wafuasi wa CHADEMA itakua ni chanzo cha kutotawalika baada ya uchaguzi mkuu hujao.
Maana wana matumaini makubwa sana kwamba watashika dola uchaguzi mkuu ujao,hizi ni sawa na ndoto za saa7 mchana,sasa kwa akili hizi za kushikiwa nadhani nchi haitatawalika kabisaaaaaa!
Ewe muumba wa mbingu na ardhi niepushe mimi na watanzania wenzangu kwa hili sekeseke ili yasijetukuta yale ya 'kimbali'
 
na haitatawalika kweli kweli maana wana nchi wameshachoshwa na mambo ya ccm sasa kama wakileta ufisadi wao kwenye uchaguzi wakashinda kimagumashi hakuna mtu atawaelewa...
 
CCM siyo mama.
Kinachokufanya usali sala ya Kuku mwenye vifaranga ya kumlaani mwewe ni brain washinging ulopewa na CCM tangu uzaliwe.

Wafuasi wa CHADEMA itakua ni chanzo cha kutotawalika baada ya uchaguzi mkuu hujao.
Maana wana matumaini makubwa sana kwamba watashika dola uchaguzi mkuu ujao,hizi ni sawa na ndoto za saa7 mchana,sasa kwa akili hizi za kushikiwa nadhani nchi haitatawalika kabisaaaaaa!
Ewe muumba wa mbingu na ardhi niepushe mimi na watanzania wenzangu kwa hili sekeseke ili yasijetukuta yale ya 'kimbali'
 
Wafuasi wa CHADEMA itakua ni chanzo cha kutotawalika baada ya uchaguzi mkuu hujao.
Maana wana matumaini makubwa sana kwamba watashika dola uchaguzi mkuu ujao,hizi ni sawa na ndoto za saa7 mchana,sasa kwa akili hizi za kushikiwa nadhani nchi haitatawalika kabisaaaaaa!
Ewe muumba wa mbingu na ardhi niepushe mimi na watanzania wenzangu kwa hili sekeseke ili yasijetukuta yale ya 'kimbali'

Magamba pia wanalijua hilo, wanatumia nguvu kubwa kuzuia speed ya chadema. 2015 machafuko yataletwa na sisiemu!
 
2015 ndio kilele kikubwa na yote haya. CCM na serikali yake wemeshindwa kuongoza na kutimiza ahadi zao lukuki kwa wananchi, wameamua kutumia polisi, usalama wa Taifa na kila aina ya watu kushambulia na kuugaribu upinzani.

Mwanachadema jipe moyo tunashinda. @
 
Wafuasi wa CHADEMA itakua ni chanzo cha kutotawalika baada ya uchaguzi mkuu hujao.
Maana wana matumaini makubwa sana kwamba watashika dola uchaguzi mkuu ujao,hizi ni sawa na ndoto za saa7 mchana,sasa kwa akili hizi za kushikiwa nadhani nchi haitatawalika kabisaaaaaa!
Ewe muumba wa mbingu na ardhi niepushe mimi na watanzania wenzangu kwa hili sekeseke ili yasijetukuta yale ya 'kimbali'
siku hizi hata karatu inaitwa nchi? maana huko ndo wanakoweza kushinda ubunge. au siku hizi hata jimbo la ubunge ni nchi?
hujiulizi kwa nini hata hawakujaribu kwenda kusini kwenye ule mgogoro wa gesi lakini kule nyamong'o walifika siku hiyohiyo? au umesahau kwenye ishu ya akina lisu kuwekwa ndani?
 
Back
Top Bottom