Uchaguzi 2020 CHADEMA mkimsimamisha Lissu najiunga na chama chenu

awamu hii imewatesa sana watz ni wakati sahihi wa kulipiza kisasi kupitia sanduku la kura.
wanasema wamefanya makubwa yepi hayo yasiyobadilisha boresha maisha ya watu.Wanayojidaia yamefanyika DAR,DODOMA na CHATO pekee mara,shinyanga,tabora,lindi,moshi,katavi,handeni,tangank hamna kitu cha wao kujivunia awamu hii.
kama ulizulumiwa korosho zako lipa kisasi october,
ulibomolewa nyumba yako,
ujapandishwa mshahara,
ujalipwa mafao yako,
ulichomewa nyavu zako
uliporwa pesa zako kupitia burea de change
umekosa ajira
ujapandishwa cheo
ulifukuzwa kwa uonevu wa vyeti
ulibambikwa kesi
ulinyimwa maendeleo sababutu eti mlichagua upinzani japo wanachukua kodi zenu,ni wizi kuchukua kodi bila kuwaletea maendeleo
ndoa yako imevunjika sababu ya maisha magumu aliyosababisha awamu hii
ulitaifishiwa mifugo yako
ulibambikwa kodi
na madhila yote uliyotendewa na awamu hii iliyoleta ufukara nchini hadi watz wenzetu wamekufa kwa stress OCTOBER 28 ni wakati wako sahii wa kulipa kisasi ili kuponya machungu na maumivu yoote.
 
Nafurahi kuwataarifu Watanzania wenzangu na wanachama wa CCM kuwa Leo nimetimiza azima niliyo ahidi kwa kujiunga rasmi na Chadema kupitia application ya Chadema Digital.
Nimejiunga baada ya wanachama wa Chadema kutuwekea mgombea (ambaye ndiye Rais ajaye) chaguo sahihi kabisa.
Naomba niwasalimie wanachama na wapenzi wote wa Chadema; PEOPLES!
#NIYEYE2020View attachment 1527931
Safi sana ubarikiwe popote ulipo

Hawa wakoloni weusi lazima tuwaondoe madarakani wameshainyonya sana hii nchi vya kutosha ni wakati wa wao kutuachia hili taifa letu sasa ili lirejee katika mikono salama

Nadhani hata taifa lenyewe litakuwa limechoka sana kuongozaa katika mifumo kandamizi maana tangia wakati wa wakoloni taifa linapelekwa Mchaka mchaka tu wakoloni walipokubali kuondoka na kutuachia taifa letu tukadhani kwamba taifa litakuwa katika mikono salama Na kusahau maumivu yote ambayo limepitia ...
Kumbe ndio likawa limedondokea katika sehemu mbaya zaidi " limedondokea kwenye mikono ya walowezi wakoloni weusi .. Wamelitafuna sana hili taifa letu mpaka mpaka inatia huzuni
 
Anga limeikataa ccm ukisoma unabii sababu ccm imekiukwa zindiko la kukimbiza mwenge sababu ya corona.
 
Ndugu Mshangai, Lissu kesha chaguliwa na ni Mpeperusha Bendera ya CHADEMA, Lini unajiunga na Chama
mkuu umeuliza swali zuri sana but kwa watu makini wajualo walifanyalo hua ni watulivu maana hakuna chama chochote kinacho mletea mkate wa kila siku wa familia yake so ni mda wowote anapojisika kutamka au kutotamka ali hali anajua nfsi yake yamtuma nini na wakati gani na kwa mda mhafaka ,watu makini na walio amua jambo fulan toka mioni mwao hua hawakurupuki
 
Hili ni muhimu Sana Lissu ajue, au afahamishwe. Visasi ni sumu. Atangaze mapema kuwa hatafanya visasi vyovyote
inategemea mkuu kama kiongonzi wa nchi kweli visasi sio bora kwa manufaa ya taifa but unapofika kufanya reform si ajabu ukakutana na vizingiti kesheria kwamaba hata kama huna visasi je huyu mtu wamponaje, hapo ndo inabidi tumia ubongo wa ziadada by the way lissu akipita majaribu kama hayo lazima ayashinde ,yaliyopita yamepita anza upya usilipe kisasi kwa yoyote cha msingi jenga taifa la tz basi
 
Yametoka moyoni mwako au unaandika kumfurahisha mtu?
Huyu jamaa sijui umri wake. Lakini ule usemi "hujafa hujaumbika" nadhani hajui maana yake. Mungu amsamehe afe akiwa mzima wa viungo vyote. Ni kauli iliyonisikitisha sana.
 
Mimi pia mkuu kura yangu itakuwa kwa Lissu lakini nitakuwa wa mwisho kuhama CCM
Mkuu ni kweli lakini si lazima kuhama chama, kikubwa hamasisha watu wampigie kura umpendae T Lisu wabunge na madiwani wa CHADEMA.
Baadae kazi ikiisha kamilika utatafakari la kufanya.
Hongera kamanda umefunguka na kuujua ukweli.
Ubarikiwe!!
 
Ndio akili za vijana wetu, nakuambia nimejiunga mwaka mmoja tokea CCM izaliwe yaani 1978 tena nikiwa JKT na kulikuwa na hekaheka za vita kule Kagera.
Pengine wewe ulikuwa hujazaliwa bado.
Unashangaa nini kukubali kwangu kumuunga mkono mgombea bora tokea chama kingine kama huyu tulie naye katuharibia chama?
CCM haikupaswa kuwa na propaganda za kitoto kama zilivyo sasa, ukatili kwa RAIA tunao uona ukifanyika, uongo wa kupitiliza hadi kutufanya wanachama tuonekane wajinga mbele ya jamii na kutoheshimu katiba na sheria.
Tanzania ni ya wote, na ninahakika Nyerere angekuwa hai asingekubali ccm iwe ilivyo na angeshindwa angeiacha.
Hata Kikwete kama mlimsikiliza Kyle Lupaso ni kuwa amechoka karibu atamwaga manyanga au kesha mwaga moyoni bali anaogopa akiwa wazi nini hatma yake? Na jee utawala nje ya ccm nao utakuwaje katika kuheshimu ulinzi wa katiba na kumuacha apumzike?
Nadhani Lissu na serikali yake haitaweka visasi, naye ajitokeze tuu kama Mimi na wengine
Nakuunga mkono 100%!!
Hawa vijana hawajui hata post zingine usingezipata usingekuwa mwanachama wa CCM!!
Sasa kama mzalendo halisi bila mihemko, anayelitakia taifa letu Demokrasia, haki na amani ya kweli tufanye uamuzi sahihi, ili kukomboa taifa toka kwenye kundi la wakoloni weusi!!
Viva Tundu Lissu viva ukombozi wa TZ!!
 
Mkuu, umeshajiunga tayari na CHADEMA? Maana ulitoa sharti wamchague Lissu
Mimi ni mwanachama wa CCM. Sio mwanachama maslahi au mwanachama fuata upepo, la hasha bali mwanachama mwanzilishi hata kama nilijiunga 1978 mwaka mmoja tokea ianzishwe.

Ninafuatilia sana siasa za chama chetu, lakini niseme wazi kuwa tokea mwaka 2016 muda tuu baada ya awamu ya tano kushika hatamu CCM yetu imepotea na kuja kikundi cha aina fulani kuigeuza CCM yetu kutoka chama chenye heshima na utu na kuwa cha kihuni, uongo na tabia za kihalifu.

Shuhudia chaguzi za serikali yetu na sasa chaguzi zetu za ndani ya chama. Ni uhuni na rushwa ya hali ya juu haijapata kutokea tangu chama kianze.

Uongo ndio usiseme, ona tunabuni mpaka kupanga watu kutoa zawadi eti za jogoo njiani kwa Rais? Kweli Rais anaweza kupewa tuu barabarani jogoo na akampokea mikononi bila kujulikana usalama wa zawadi hiyo?

Sasa kwa ujinga unaoendelea kwa chama changu natangaza rasmi binafsi kujiunga na Chadema kama watamsimamisha Tundu Lissu kugombea Urais ili nimpe kura yangu.

Nategemea wengi ndani ya CCM wataniunga mkono kwa sababu za Lissu zifuatazo;

*Anaheshimu Katiba na Sheria.
*Sio muongo anapenda ukweli
*Ana uelewa mkubwa wa ndani na nje ya nchi.
*Anaheshimu Utu wa Mwanadamu
*Hana roho ya visasi.

OMBI;
Tanzania ni yetu, kuiacha tena miaka mitano mingine ipotee kama hii iliyopita ni kuitafuta laana ya vizazi vijavyo. Tuungane tufanye mabadiliko chanya, vyama ni vya kupita tuu lakini taifa lipo palepale. Chadema watuletee Lissu nasi tumpe kura.
Wasalaam aleikum!

View attachment 1522282
 
Nafurahi kuwataarifu Watanzania wenzangu na wanachama wa CCM kuwa Leo nimetimiza azima niliyo ahidi kwa kujiunga rasmi na Chadema kupitia application ya Chadema Digital.
Nimejiunga baada ya wanachama wa Chadema kutuwekea mgombea (ambaye ndiye Rais ajaye) chaguo sahihi kabisa.
Naomba niwasalimie wanachama na wapenzi wote wa Chadema; PEOPLES!
#NIYEYE2020View attachment 1527931
Mkuu, umeshajiunga tayari na CHADEMA? Maana ulitoa sharti wamchague Lissu
.
 
Nakuunga mkono 100%!!
Hawa vijana hawajui hata post zingine usingezipata usingekuwa mwanachama wa CCM!!
Sasa kama mzalendo halisi bila mihemko, anayelitakia taifa letu Demokrasia, haki na amani ya kweli tufanye uamuzi sahihi, ili kukomboa taifa toka kwenye kundi la wakoloni weusi!!
Viva Tundu Lissu viva ukombozi wa TZ!!
Nikiangalia mwenendo wa kampeni unavyo endelea kwa kweli sijutii maamuzi yangu.
Kwanza nafurahishwa na jinsi Lissu anavyo mwaga Sera kwa ukweli na hadhi ya Presidential person tofauti na mgombea wa chama changu cha zamani asiyejua hata anataka kusema nini zaidi ya kuji contradict tuu.
Nimeshuhudia wanaccm wengi sana ninaofahamiana nao wakiwa wane KATA SHAURI KUACHANA NA DHAMBI YA CCM
 
kuendelea na ccm hii ya ubabe, ukatili ni kujitafutia laana yako na vizazi vyako..

tumuunge mkono muujiza lissu, kama alivyotoka salama baada ya risasi zile, atutoe na watz salama tukaishi tanzania ambayo mwananchi ndio boss na kiongozi ni mtumishi, na sio hii ambayo mtu mmoja anaamua nini cha kufanya na wapi asipeleke maendeleo kisa tu ni wapinzani, huku akijisahaulisha kuwa ashachukua kodi zao kitambo na anawagomea maendeleo.

Nikiangalia mwenendo wa kampeni unavyo endelea kwa kweli sijutii maamuzi yangu.
Kwanza nafurahishwa na jinsi Lissu anavyo mwaga Sera kwa ukweli na hadhi ya Presidential person tofauti na mgombea wa chama changu cha zamani asiyejua hata anataka kusema nini zaidi ya kuji contradict tuu.
Nimeshuhudia wanaccm wengi sana ninaofahamiana nao wakiwa wane KATA SHAURI KUACHANA NA DHAMBI YA CCM
 
Mimi ni mwanachama wa CCM. Sio mwanachama maslahi au mwanachama fuata upepo, la hasha bali mwanachama mwanzilishi hata kama nilijiunga 1978 mwaka mmoja tokea ianzishwe.

Ninafuatilia sana siasa za chama chetu, lakini niseme wazi kuwa tokea mwaka 2016 muda tuu baada ya awamu ya tano kushika hatamu CCM yetu imepotea na kuja kikundi cha aina fulani kuigeuza CCM yetu kutoka chama chenye heshima na utu na kuwa cha kihuni, uongo na tabia za kihalifu.

Shuhudia chaguzi za serikali yetu na sasa chaguzi zetu za ndani ya chama. Ni uhuni na rushwa ya hali ya juu haijapata kutokea tangu chama kianze.

Uongo ndio usiseme, ona tunabuni mpaka kupanga watu kutoa zawadi eti za jogoo njiani kwa Rais? Kweli Rais anaweza kupewa tuu barabarani jogoo na akampokea mikononi bila kujulikana usalama wa zawadi hiyo?

Sasa kwa ujinga unaoendelea kwa chama changu natangaza rasmi binafsi kujiunga na Chadema kama watamsimamisha Tundu Lissu kugombea Urais ili nimpe kura yangu.

Nategemea wengi ndani ya CCM wataniunga mkono kwa sababu za Lissu zifuatazo;

*Anaheshimu Katiba na Sheria.
*Sio muongo anapenda ukweli
*Ana uelewa mkubwa wa ndani na nje ya nchi.
*Anaheshimu Utu wa Mwanadamu
*Hana roho ya visasi.

OMBI;
Tanzania ni yetu, kuiacha tena miaka mitano mingine ipotee kama hii iliyopita ni kuitafuta laana ya vizazi vijavyo. Tuungane tufanye mabadiliko chanya, vyama ni vya kupita tuu lakini taifa lipo palepale. Chadema watuletee Lissu nasi tumpe kura.
Wasalaam aleikum!

View attachment 1522282
Bilashaka una jambo lako popote ulipo kumpigia kampeni sana TL
 
Back
Top Bottom