Kijakazi
Platinum Member
- Jun 26, 2007
- 9,300
- 14,967
CHADEMA msitafute Mchawi, Mchawi wenu ni IQ ndogo ya Wanachama wenu, nitawapa Mfano, Sasa kuna mchakato wa kuandika Katiba Mpya, ktk hali ya kawaida nilitegemea nguvu zote za Wanachadema na Wapinzani kwa Ujumla zielekee kwenye kuboresha Mazingira ya wao kuweza kuwa na Usawa na Chama tawala pindi uchaguzi utakapokuja, lkn wapi woote wamegeukia kudai jina la Tanganyika, kana kwamba wakilipata kesho basi Daftari la Wapiga kura nalo litajiboresha na kuacha madai ya Msingi ambayo ndio yanawakosesha ushindi kwa mfano Mwenyekiti wa Tume kuteuliwa na Raisi, Madaraka makubwa ya Raisi pmj na Watu wake kama Wakuu wa Mikoa, Wilaya n.k, hapo hapo wakishindwa Uchaguzi wanaanza kulalamikia kwamba sijui Daftari la Wapiga kura halikuboreshwa, sijui Vijana wengi wamekatwa kwa makusudi, na haya Mambo yoote yamo kwenye Rasimu lkn sijasikia hili wala fyoko, nasikia tuu tunataka Jina la Tanganyika...Hivyo wakulaumu hapo ni IQ ndogo ya Wanachama wenu!