CHADEMA mbona mmewatupa watanzania? Msitukane aisaidii

CHADEMA mbona mmewatupa watanzania? Msitukane aisaidii

WAZIWAZI

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2014
Posts
1,815
Reaction score
1,576
Wana janvi mimi sio mpenzi wa cdm ila naumia kuona nchi yetu inakosa kiungo muhimu cha demokrasia ambacho ni upinzani wenye nguvu kwa chama kinackokuwa madarakani, sasa CCM wamekunja nne, hakuna asiyejua kuwa hata uchaguzi wa 2015 watashinda na wengine watabaki kushabikia tu kama tulivyoona cdm wanamshabikia Sitta kuwa mwenyekiti wakiongozwa na kijana msomi mwenye vimelea vya kiburi kamanda antpass Tundu Lisu alafu sasa hivi wanahaha.

Wazee wetu kipindi wanaanzisha mfumo wa vyama vingi lengo kuu ilikuwa ni kuwa na vyama 2 ambavyo vingejipambanua kwa hoja na hatimaye wananchi wapime hoja na kukipa kimojawapo dola. sasa kuna sintofahamu ya mstakabali wa nchi yetu maana tuna utitiri wa vyama na ukichungulia kwa jicho la kizalendo viongozi wa vyama hivyo ni waganga njaa tu.

Kwa nini CHADEMA?
Ni chama ambacho kilianza vizuri na graph ikiwa ikipanda siku hadi siku na kujipambanua kwa umaridadi na nadhifu hasa 2007-2010 kabla kundi ovu kupewa nafasi za juu nakuwa wasemaji wa chama hiki, kundi hili lilianza kujipenyeza taratibu kuanzia 2008 na baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 likajimilikisha chama na kuanza kuweka makundi ndani ya chama kwa kuita wanachama wenzao wenye mitazamo tofauti na wao wasaliti. Waovu hao wakateka kikundi cha cdm propaganda mitandaoni na kukilisha maneno na wao wakawa watumwa wa waovu.Leo hii ukitoa ushauri wowote juu ya wapi cdm imeteleza unatukanwa eti bk7 at work. Matokeo yake kila mtu hapa anafahamu kinachowapata ingawa mitandaoni kikundi chao kinaendelea kufanya propaganda hasi ya kujifariji kusiko na tija eti mpaka kieleweke tuna Mungu. Nawaombeni sana maridhiano tunayoyaona mnafanya na CCM dodoma na Ikulu ndio njia sahihi ya kusonga mbele na nyinyi rudini mezani mfanye maridhiano ya pamoja juu ya tofauti zenu nazani mtapata jibu na ndo malezi mazuri hayo ndani ya demokrasia.

Chadema ndo chama ambacho toka vyama vingi vimeanza ndo chama ambacho kilikubalika na rika zote wasomi, wafanyakazi na wakulima ila sasa japo chadema mtandaoni wanajifariji, ukweli chama kinapoteza wapenzi kwa kasi kumbwa mno ila bado mna nafasi nzuri ya kujirekebisha na hatimaye imani ikarudi kwa jamii mkasaidia jamii kuichangamsha serikali katika mambo ya kimaendeleo na hata kushika dola kwa njia ya kidemokrasia siku za usoni.

Wenu rafiki wa kweli
WAZIWAZI:A S 103:
 
Nadhani watasikia kilio chako. Kimya kingi kina mshindo mkuu. Kama ninavyojua, kuna kitu kinakuja cha kuleta matumaini kwa Watanzania, tusife moyo!
 
Kuna wakati wa kushauri na wakati wa kuchukua hatua , sijui wewe wakati huu kwako ni wa jambo gani kati ya hayo mawili hapo....
 
Itawauma sana eti hata CCM nao inawauma,maajabu haya,isiwaume CDM wenyewe ije kuwauma CCM, kweli?

Endeleeni kusitikitika na kuneng'eneka lakini mda si mrefu mtaijua CDM ni nini kila siku mmekalia majungu,kwani umelazimishwa kuipenda CDM?

Wasalimie lumumba na buku 7 zako kachukue!
 
Kuna wakati wa kushauri na wakati wa kuchukua hatua , sijui wewe wakati huu kwako ni wa jambo gani kati ya hayo mawili hapo....
kama umesoma ujumbe wangu na sio heading tu, utajua ni wa jambo gani.
 
ahsnte mkuu kwa mchango wako kila lakheri mimi ngoja nikachukue buku 7.
 
Itawauma sana eti hata CCM nao inawauma,maajabu haya,isiwaume CDM wenyewe ije kuwauma CCM, kweli?

Endeleeni kusitikitika na kuneng'eneka lakini mda si mrefu mtaijua CDM ni nini kila siku mmekalia majungu,kwani umelazimishwa kuipenda CDM?

Wasalimie lumumba na buku 7 zako kachukue!
ahsnte mkuu kwa mchango wako kila lakheri mimi ngoja nikachukue buku 7
 
Itawauma sana eti hata CCM nao inawauma,maajabu haya,isiwaume CDM wenyewe ije kuwauma CCM, kweli?

Endeleeni kusitikitika na kuneng'eneka lakini mda si mrefu mtaijua CDM ni nini kila siku mmekalia majungu,kwani umelazimishwa kuipenda CDM?
 
Ni kweli inauma sana hasa.kwa watanganyika wanaohitaji mabadiliko ya kweli na kuona maendeleo ya kweli yenye uwiano na rasilimali za nchi yetu.
 
Shida ya chadema ukiwapa ushauri wanakutukana ukiwapongeza the same ni bora kuwaombea mabaya tu wapotee kabisa kwenye siasa za bongo.
 
Itawauma sana eti hata CCM nao inawauma,maajabu haya,isiwaume CDM wenyewe ije kuwauma CCM, kweli?

Endeleeni kusitikitika na kuneng'eneka lakini mda si mrefu mtaijua CDM ni nini kila siku mmekalia majungu,kwani umelazimishwa kuipenda CDM?
Mkuu huyo jamaa mzoee anamatatizo makubwa sana ya kimawazo na fikra.
 
Wana janvi mimi sio mpenzi wa cdm ila naumia kuona nchi yetu inakosa kiungo muhimu cha demokrasia ambacho ni upinzani wenye nguvu kwa chama kinackokuwa madarakani, sasa CCM wamekunja nne, hakuna asiyejua kuwa hata uchaguzi wa 2015 watashinda na wengine watabaki kushabikia tu kama tulivyoona cdm wanamshabikia Sitta kuwa mwenyekiti wakiongozwa na kijana msomi mwenye vimelea vya kiburi kamanda antpass Tundu Lisu alafu sasa hivi wanahaha.

Wazee wetu kipindi wanaanzisha mfumo wa vyama vingi lengo kuu ilikuwa ni kuwa na vyama 2 ambavyo vingejipambanua kwa hoja na hatimaye wananchi wapime hoja na kukipa kimojawapo dola. sasa kuna sintofahamu ya mstakabali wa nchi yetu maana tuna utitiri wa vyama na ukichungulia kwa jicho la kizalendo viongozi wa vyama hivyo ni waganga njaa tu.

Kwa nini CHADEMA?
Ni chama ambacho kilianza vizuri na graph ikiwa ikipanda siku hadi siku na kujipambanua kwa umaridadi na nadhifu hasa 2007-2010 kabla kundi ovu kupewa nafasi za juu nakuwa wasemaji wa chama hiki, kundi hili lilianza kujipenyeza taratibu kuanzia 2008 na baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 likajimilikisha chama na kuanza kuweka makundi ndani ya chama kwa kuita wanachama wenzao wenye mitazamo tofauti na wao wasaliti. Waovu hao wakateka kikundi cha cdm propaganda mitandaoni na kukilisha maneno na wao wakawa watumwa wa waovu.Leo hii ukitoa ushauri wowote juu ya wapi cdm imeteleza unatukanwa eti bk7 at work. Matokeo yake kila mtu hapa anafahamu kinachowapata ingawa mitandaoni kikundi chao kinaendelea kufanya propaganda hasi ya kujifariji kusiko na tija eti mpaka kieleweke tuna Mungu. Nawaombeni sana maridhiano tunayoyaona mnafanya na CCM dodoma na Ikulu ndio njia sahihi ya kusonga mbele na nyinyi rudini mezani mfanye maridhiano ya pamoja juu ya tofauti zenu nazani mtapata jibu na ndo malezi mazuri hayo ndani ya demokrasia.

Chadema ndo chama ambacho toka vyama vingi vimeanza ndo chama ambacho kilikubalika na rika zote wasomi, wafanyakazi na wakulima ila sasa japo chadema mtandaoni wanajifariji, ukweli chama kinapoteza wapenzi kwa kasi kumbwa mno ila bado mna nafasi nzuri ya kujirekebisha na hatimaye imani ikarudi kwa jamii mkasaidia jamii kuichangamsha serikali katika mambo ya kimaendeleo na hata kushika dola kwa njia ya kidemokrasia siku za usoni.

Wenu rafiki wa kweli
WAZIWAZI:A S 103:

Inafurahisha jinsi unavyokielezea chama ambacho wewe si mwanachama. umekiri wazi kuwa wazee weti walikusudia viwepo vyama viwili tuu vikubwa
mbona muda wote cdm ilipokua inafanya vizuri hukujiunga nao? labda hujui adui wa mageuzi makubwa kama haya cdm inayoyapigania ni unafiki. uoga na watu wanaolalamika muda wote.
 
Heri kuwa na chama kimoja kuliko kuwa na chama cha upinzani kinachoendeshwa kibangibangi kama cdm
 
Kwa mtu anayependa serikali kusimamiwa vizuri huwezi kufurahia hata siku moja Chama tawala kuwa na wabunge wengi bungeni. Watanzania wengi bado uelewa wao ni mdogo sana hata wale ambao wanaonekana wamesoma bado nao ni mbumbumbu tu, elimu yao imebakia tu kwenye makaratasi. Uwezo wa kuchanganua mambo bado hawawezi kabisa. Akili zao ni za kushikiwa tu.

Mimi ningefurahi sana chama chochote tawala kinachoendesha serikali kiwe CCM,CHADEMA, CUF, NCCR, DP etc, kama wamepata nafasi ya kuendesha serikali basi bungeni wawepo wapinzani wengi angalau nusu kwa nusu ili waweze kusimamia serikali vizuri.

Kama angalau wakiwa nusu kwa nusu serikali haiwezi kupitisha mambo ambayo ni ya kuwakandamiza wananchi. Hata kama leo hii CHADEMA kichukua uongozi wa nchi basi nisingefurahia wawe na wabunge wengi, angalau wafike nusu, na nusu nyingine iwe inachukuliwa na wapinzani ili waweze kusimamia serikali vizuri.

Madhara ya kuwa na wabunge wengi wa chama tawala ni mengi sana. Wananchi kupata haki ni ngumu sana. Laiti kama vyama tawala kila wakati vingekuwa vinabadilika hakuna ambaye angebweteka akiingia madarakani maana anajua akikosea anatoswa. Na wangejitahidi kwa vyovyote vile kuwatumikia wananchi badala ya matumbo yao. Ila wale ambao Mungu amewapa ufahamu na bado kwa makusudi kabisa wanapotosha wale ambao hawana ufahamu, siku ya mwisho hukumu yao itakuwa kubwa mno, na watubu na kurejea katika misingi stahili.

Mungu atusaidie watanzania tubadilike tuache ushabiki wa kishamba ila tuangalie hali halisi jinsi inavyostahili kuwa ili TAIFA LETU liweze kusonga mbele katika misingi stahili ya uhuru na haki.
 
vyama vyetu vingi vinaundwa ili kuhujumu vyama vinavyoonekana kulinda utaifa dhidi ya ccm.vyama vingi vikipata nguvu hugeuka adui wa vyama vyote nchini.chili halina ubishi kwa wafuatiliaji was vyama hapa tz.
kikubwa zaidi hata watanzania wengi bado wako too primitive. hebu Fikiri kufanya siasa katika jamii ambayo bado haijui hata umuhimu was vyoo? Nchi hii. bado tunatoana tongotongo za ujinga vichwani mwetu.name mtaji was ccm ndio hao ambao bado wengi, hao wa kuelimishwa hadi kutumia choose majumbani mwao.
 
Itawauma sana eti hata CCM nao inawauma,maajabu haya,isiwaume CDM wenyewe ije kuwauma CCM, kweli?

Endeleeni kusitikitika na kuneng'eneka lakini mda si mrefu mtaijua CDM ni nini kila siku mmekalia majungu,kwani umelazimishwa kuipenda CDM?

Wasalimie lumumba na buku 7 zako kachukue!

Sawa cdm masalia, unahisi unakijenga chama kwa kuandika hivi. Kumbe ndio unakibomoa zaidi
 
Back
Top Bottom