GE2025 CHADEMA: Matokeo yaliyotangazwa hayana uhalisia, hakukufanyika uchaguzi Tanzania

GE2025 CHADEMA: Matokeo yaliyotangazwa hayana uhalisia, hakukufanyika uchaguzi Tanzania

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Makumbele

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2009
Posts
241
Reaction score
1,056
TAARIFA YA AWALI YA CHAMA JUU YA KINACHOITWA MATOKEO YA UCHAGUZI TANZANIA​

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinapinga vikali kinachoitwa matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi.

Matokeo haya hayana uhalisia wowote kwani ukweli ni kwamba hakukufanyika uchaguzi Tanzania.

Wananchi hawakushiriki katika uchaguzi wa Oktoba 29 kutokana na mazingira yasiyo huru, haki, na kukosekana kwa uwanja sawa wa kisiasa.

Aidha, Chadema tunasisitiza kwamba Tume ya Uchaguzi imetoa takwimu ambazo hazina uhalisia wowote zaidi ya kudhihirisha nia ovu ya Samia Suluhu Hassan na chama chake ya kuiba uchaguzi jambo ambalo walifanikiwa.

Chadema tumeeleza mara kadhaa msimamo wetu wa "No Reforms, No Election" (Hakuna Mabadiliko, Hakuna Uchaguzi). Tulionya wazi kuwa bila marekebisho ya kweli katika mfumo wa uchaguzi, na sheria za kisiasa, uchaguzi huu usingeweza kuwa huru, wa haki, na wa kuaminika.

Maandamano yaliyoenea nchi nzima ni uthibitisho wa wazi kuwa wananchi hawakushiriki kwenye kile kinachoitwa uchaguzi na kutomkubali yeyeto anayetokana na mchakato huu mbovu wa kiuchaguzi.

Hivyo Chadema;
  1. Kutangazwa kwa matokeo leo ni mapinduzi ya wazi dhidi ya matakwa ya Watanzania ambao wamenyimwa haki yao ya kidemokrasia ya kuchagua kiongozi wanaomtaka.
  2. Haimtambui Samia Suluhu Hassani kama Rais wa Jamhuri ya Tanzania kwa kuwa hajachaguliwa na wananchi wa Tanzania.
  3. Inaishauri jumuiya ya kimataifa kutomtambua Samia Suluhu Hassan kama kiongozi wa Tanzania kwani hana uhalali huo kwa kuwa hajachaguliwa na wananchi wa Tanzania.
Imetolewa leo Jumamosi, tarehe 01 Novemba 2025

38d620c0-8b25-4284-b635-51873546c2bc.jpeg
 
WaTanzania zaidi ya milioni 30 wajitokeze kupiga kura lakini hata misululu ya kuingia kupiga kura isionekane popote, nchi nzima?

Asili mia zaidi ya 86 ya watu wenye sifa ya kupiga kura wajitokeze siku ya uchaguzi; huyo Samia Suluhu Hassan uchawi wa namna hiyo kautoa wapi?
 
Shida yangu ni wale vijana chawa wa ccm najua wapo ambayo tayar wanaomboleza misiba. Ya ndugu zao na familia inatawatazana ,wasanii wa tanzania wamekubali kupokea pesa ili mashabiki zao wauliwe barabarani ,tulionaki tutaishi wote ,wasanii wa Tanzania dunia imewaona
 
Mpishi wa haya yote na sterling tangu square A ni mchengrwa kwa kujipendekeza kwa mama mkwe na ulafi wa madaraka

Huyu ndiye anastahili kujibu yote itakapofika ICC hapo baadaye, ni suala la muda tu! Hamna aliyetegemea protest na muda wake ulipofika zikawa na sasa muda wa ICC utafika tu pia, damu zote zilizomwagika zitakua accounted hatimaye
 
Kubaki madarakani kwa kutumia vyombo dola na tume ya uchaguzi.
 
Tukubali tu kiukweli km ni Uchaguzi wa kidemokrasia basi hatuna tuamue tuwe na chama kimoja basi tusiwe tunahangaika hivi 🙌🙌
 
Tusaidieni pia wananchi waliokua wakiandamana maeneo mbalimbali nchini kama mlivyoandika kwenye hii taarifa ..

CHADEMA SIO CHAMA NI GENGE LA KIHALIFU NA IMETHIBITIKA RASMI.
 
Back
Top Bottom