Hivi ccm wamebaki na uasili wake?
Wanamtandao
Wanamaslahi
Wanaccm asilia
Ipi mwalimu aliiacha?
Ruzuku yote wanagawana Dr.Slaa na Mbowe, wananunua majumba Dubai, Ulaya, South Afrika, wanakopeshana pesa za ruzuku.
Hiyo RUZUKU ni kiasi GANI? Kwasababu hayo MAJUMBA DUBAI ni kiasi gani cha RUZUKU itatosha kuzinunua?
Sasa kwa Upande wa chama cha CCM Mbona Mawaziri Wastaafu na Wengine walikuwa Mawaziri kwa Ungwe Moja tu wana Majumba Nje ya NCHI... Sasa Tatizo lako ni MBOWE na wao RUZUKU yao imekuwa kubwa katika Uchaguzi wa 2010 baada ya kuwashinda CUF hivyo hapo ina Maana hiyo UNGWE MOJA tu ya hiyo RUZUKU wameweza kununua hayo Majumba?
Kwani RUZUKU ya wa CCM inakwenda wapi? Sasa ni kina nani hao Wanaofanya biashara ya UNGA?
Kweli kila mtu ananunua Majumba - Lau Masha ana Majumba South Africa; na Mawaziri wengi kibao wote wa CCM na sio kwamba walipata hizo pesa kihalali...
Hakuna kiongozi yoyote hapa nchini anayeweza kununua Majumba nje ya nchi bila ya kutumia MILANGO ya NYUMA
Mnasema MBOWE ni RUZUKU; Lakini yeye ana DISCO TEC; Ana TOP CLASS HOTEL na Mashamba Makubwa ya KAHAWA (VALUABLE CASH CROP) na ni tangu zamani AMERITHI... Sasa Rais wetu mstaafu Mkapa alikuwa hana chochote akajipa IRON ORE MINE... Hamuoni kama ni MAKOSA hakuwa na pesa hata kidogo sasa hivi Mmmm; Abdallah Kigoda one of the king pin... Waliuza VIWANDA vya SERIKALI bila kuwajali wananchi walala hoi... pesa zote ziliishia kwao...
Sasa sisi hapa tunawakimbia Waliotuangusha VIBAYA -- Tunakimbilia ati RUZUKU ya CHAMA na kuwaita WEZI wakubwa Sasa na hawa wengine ni wakina nani??? ABOVE THE LIMIT?? they cannot be touched; prosecuted and questioned???
Kwasababu wao ni BORA ZAIDI; Chochote watakiua lakini as long as CCM ipo MADARAKANI hayo yatazimwa na kutupiwa WANYONGE hayo MAKOSA...
Serikali ya CCM ina VYOMBO VYA HABARI - TV; RADIO; POLISI; MAHAKAMA; JESHI; JELA; - Hauwezi kubishana na HIYO SERIKALI utashindwa tu...
Angalia HOJA YAKO ni ya kushambulia watu wawili MBOWE na SLAA na unapata wakukuunga MKONO kuliko wa kukuuliza PESA za RADA zimekwenda WAPI????
Sasa ninavyoongea HIVI; Mtasema MIMI NI CHADEMA na ni walewale tu na kudharau UKWELI... na kukimbilia yaleyale UZUSHI na UONGO...
tatizo linalokuponza ni buku saba chadema kama chama chenye uadilifu akiwezi kufuga wezi na wanyang'anyi kwa kuhofia kufa au?kingine chochote unachokiwaza wewe magamba ukweli utabakia kuwa ukweli na uongo utabakia kuwa uongo msaliti wa mabadiliko yoyote yule hata awe baba yangu sitamfumbia macho kwa namna iwayo yote,inatakiwa ccm na nyie mjifunze kuwawajibisha mafisadi walioko ndani ya chama chenu ambao wamekua miungu watu.wanaukumbi.
Chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) ambacho sasa hivi kipo chini ya mwenyekiti freeman mbowe na katibu mkuu dr. Slaa, kinazidi kupoteza dira na mwelekeo wake wa asili, na hivyo kuharibu sifa za chama hicho kama kilivyosifiwa na mwalimu nyerere enzi za uhai wake.
Badala ya kuwa chama cha siasa kinachotumia hoja na ustarabu kutafuta ushawishi kwa umma, chadema ya sasa imegeuka kuwa chama cha kiharakati kisichoheshimu hata mamlaka ya nchi kwa mtindo huu chadema hakiwezi kufika popote kama chama cha siasa, lazima mbowe na dr. Slaa waambiwe ukweli, kimsimamo wapo tofauti na naibu katibu mkuu wa chadema zitto kabwe, ambao ni miongoni mwa makada wachache wazalendo na watiifu.
Zitto, ambaye ana kundi kubwa la vijana pamoja na baadhi ya wazee amekuwa akitengwa kushiriki kwenye kazi
za chama kama vile operesheni za vuguvugu za m4c, operesheni sangara, toka kumalizika kwa uchaguzi mwaka 2010, zitto amekuwa akitofautina na misimamo kadhaa ya chama chake, ambayo inaonekana siyo ya kisiasa ni ya kiharakati zaidi. Kama suala la kumtabua rais kikwete kama rais halali wa tanzania, na mwaka 2010 dr. Slaa, hata wabunge wenzake walipoweka azimio la kususia hotuba ya rais bungeni kutoka nje, zitto aliamua kujitenga nao, viongozi wa chadema nao wanazidi kumtenga zitto, hata majuzi walipopata mwaliko ikulu kutoka kwa rais kikwete, kujadili masuala ya katiba walienda peke yao, suala la ukaguzi wa mahesabu yavyama vya siasa ambalo linafuatliwa na kamati ya bunge ya mahesabu ya serikali pac, chadema wanaona kama ni suala la zitto.
Chadema sasa imeshindwa kuwajenga vijana kuwa na moyo wa uzalendo wa nchi yao, na badala yake imekuwa ikiwahamasisha kuvuruga misingi ya uzalendo na kutotii sharia na mamlaka zilizopo, pia wengi wa wabunge wa chadema ni watiifu kwa mbowe na dr. Slaa, ni wale wanaodaiwa kuingia ndani ya chama kwa lengo la
kusaka ubunge tu, na maslahi huku wakiwa hawana historia yoyote ya mchango wao wa kujenga chama.
Hali hii ndiyo imefanya chadema sasa ionekane machoni mwa jamii ya watanzania kama chama cha vurugu na ubabe, hali inawafanya pia wananchi wasite kukiamini kwa kukikabidhi madaraka makubwa ya kuongoza dola.
Vijana wa Chadema kutoka mikoa mbali mbali isipokuwa maeneo ya kaskazini, wameapa na kuweka wazi kuwa hawatakubali yaliyotokea mwaka 2009 kukwata jina lake kugombea Uenyekiti.
Naomba chadema wayakumbuke maneno haya
chama cha ukoo kitafia kwenye ukoo husika tusubiri mtaniambia wenyewe.
Hivi ukiandika kama ulivyoandika hapa ndiyo unalipwa sh ngapi mkuu ?
Mkuu lini tumekupa ajira ya kuwa msemamji wetu ??
Mhhh, hapa ni utamu wa nini anasikia? Muziki, Green and Yellow au M-bamia wa Jamaa? Kweli CCM raha jamani, utaaamu.
![]()