CHADEMA kwa Usahaulifu Wamekubuhu

CHADEMA kwa Usahaulifu Wamekubuhu

Kojo Dowido

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2015
Posts
354
Reaction score
111
Ni pale wanapo lalama kuhusu kura au alama alizopata mgombea wao wa urais kutokana na utafiti wa twaweza.

Kulikuwa na kura ya maoni iliendeshwa hapa jamvini kati ya Dr Slaa na Lowassa (wakati huo akiwa CCM). matokeo wote tunajua. Moderators wanaweza kutuwekea kama reference. Jambo la kustajabisha pamoja na maoni yale ya wanaJF wao waliopt kuachana na Slaa wakamchukua Lowassa.

Sasa Twaweza wanapokuja na takwimu hizi mnacholalamikia ni nini hasa? mliamua kwa kupitia mwenyekiti wenu kubadili gia angani na uliza, je huu ni ungwana, kulalama wakati Lowasa ni chaguo lenu?

Mtu ambaye kwenye kipengele cha uadilifu kule CCM alikuwa wa 44 kati ya wagombea urais 44. Nyie mkaona muwaletee watanzania kuwa wamchague awe rais wao na kwa maana hii CHADEMA katika kigezo cha uadilifu Lowassa ni nambari moja. Mmeyataka wenyewe hamna wa kumlaumu.
 
sasa twaweza wanapokuja na takwimu hizi mnacholamikia ni nini hasa?
Hivi na wewe kwa akili yako unaona Magufuli na Lowassa wanatofautiana kwa kiwango chote hicho cha asilimia 44? Kwa lugha nyepesi, Magufuli na Lowassa kweli wanatofautiana kwa idadi ya wapiga kura milioni nane?
 
Hivi na wewe kwa akili yako unaona Magufuli na Lowassa wanatofautiana kwa kiwango chote hicho cha asilimia 44? Kwa lugha nyepesi, Magufuli na Lowassa kweli wanatofautiana kwa idadi ya wapiga kura milioni nane?

kwa hili suala la uadilifu hata hiyo 44 ni kidogo ingetakiwa iwe zaidi ya hapo. huko ccm alikuwa wa 44 yaani wa mwisho.
 
Kuna mawasilino kati ya Mwigulu na wapiga debe wenzake yalionaswa na MAWIO,humo,anawaagiza kuingilia hizi tafiti za kimagumashi. Hadanganyiki mtu hapa,kama ni kweli nini kinawatoa ccm mapovu n matusi kila siku
 
wasahaulif n ccm,wamesahau kila k2 kuanzia misingi yake mpaka kwa mahitaj ya watz
 
Tafiti zote zinapikwa lumumba na wiki ijayo redet wanatoa iliyopikwa tena hapo lumumba. Bahati nzuri mwaka huu kuna vijana wazalendo ndani ya chama ambao hawako tayari kuona hadaa hizi.
 
Tatizo la wana ukawa ni kutokubali ukweli. Kwenu ni kitu kinachowatetea ndio sahihi hata kama mnapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa! Tusubiri october 26 tuone sura za watu zitakuwaje!
 
Kuna mawasilino kati ya Mwigulu na wapiga debe wenzake yalionaswa na MAWIO,humo,anawaagiza kuingilia hizi tafiti za kimagumashi. Hadanganyiki mtu hapa,kama ni kweli nini kinawatoa ccm mapovu n matusi kila siku

Hivi kweli mtu uliye makini unaweza kuamini kinachoandikwa na magazeti kama Mawio,mwanahalisi,Uhuru au Tanzania daima?
 
Lowasa hana jipya zaidi ya hela za kifisadi alizomhonga mbowe! na mijitu inafuata tu maneno ya mbowe wakijua baada ya uchaguzi huu anaingia kwenye listi ya matajiri wakubwa bongo kwa hela atakazopiga kwenye kampeni hizi
 
Porojo..huwezi kulinganisha umaarufu wa lowassa na ule wa slaa.
 
Watashindwa kuanza utafiti hadi kwenye uchaguzi watake wasitake hapa Kazi, ujinga wao ndio unawaponda vichwa, na msikimbii baada ya Matokeo sababu hakuna kwenda Mahakamani ni moto mdundo Makufuli mpaka ikulu
 
Back
Top Bottom