amba.nkya
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 446
- 131
[h=2] Heshima mbele wanajamvi...
Tafadhari rejea Thread ya jana Mlipuko wa CHADEMA watokea Mtaa wa Mavurunza, Kimara ambao ulikuwa ni Mkutano wa maandalizi ya ujio wa Katibu Mkuu wa chama Taifa, Mh. Dr. Wilibroad Slaa pamoja na viongozi wengine wa kitaifa kwenye Mkutano wa Kata siku ya Jumamosi ya 25 Februari 2012.[/h] Taarifa kamili ni kwamba kutakuwa na Mkutano wa hadhara CHADEMA Kata ya Kimara, utakaofanyika kwenye eneo la wazi lililopo nyuma ya BS Grocery, Barabara ya Bonyokwa, siku ya Jumamosi ya tarehe 25 Februari 2012 kuanzia saa nane mchana. Barabara ya Bonyokwa inaungana na Barabara ya Morogoro kuanzia Kimara Mwisho kuelekea Segerea na Kinyerezi.
Kwa watakaotumia usafiri wa gari/daladala wanashauriwa washuke kwenye kituo cha kwa Mashaka na waulize BS Grocery ilipo.
Mgeni rasmi kwenye mkutano huo atakuwa Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa, Mh.Heche akimwakilisha Mh.Dr.Wilibroad Slaa ambaye amepata dharura. Vile vile, viongozi wengine wa kitaifa kupitia CHADEMA wanaotarajiwa kuambatana na Mh. Heche ni pamoja na makamanda wafuatao: Mh. Mnyika, Tundu Lissu, Mh. Zitto, Halima Mdee na Mr Sugu. Kabla ya Mkutano huo kutakuwa na shughuli za uzinduzi wa Matawi na kusimika misingi ya CHADEMA kwenye mitaa yote ya Kata ya Kimara.
Aidha, kwenye Mkutano huo wa hadhara Mh. Heche anatarajiwa kuzindua Tawi la Mavurunza pamoja na harambee kwa ajili ya ofisi ya Tawi hilo, kupokea wanachama wapya na kuhutubia wanachama, wadau na wananchi kwa ujumla akipewa support ya nguvu kutoka kwa makamanda atakoambatana nao. Hakika CHADEMA itatikisa tena Kimara, Mtaa wa Mavurunza
Hivyo, ukiwa kama mwanachama au mdau muhimu wa CHADEMA, unaombwa kuhuduria mkutano huo muhimu sana bila kukosa.
Nawasilisha
Tafadhari rejea Thread ya jana Mlipuko wa CHADEMA watokea Mtaa wa Mavurunza, Kimara ambao ulikuwa ni Mkutano wa maandalizi ya ujio wa Katibu Mkuu wa chama Taifa, Mh. Dr. Wilibroad Slaa pamoja na viongozi wengine wa kitaifa kwenye Mkutano wa Kata siku ya Jumamosi ya 25 Februari 2012.[/h] Taarifa kamili ni kwamba kutakuwa na Mkutano wa hadhara CHADEMA Kata ya Kimara, utakaofanyika kwenye eneo la wazi lililopo nyuma ya BS Grocery, Barabara ya Bonyokwa, siku ya Jumamosi ya tarehe 25 Februari 2012 kuanzia saa nane mchana. Barabara ya Bonyokwa inaungana na Barabara ya Morogoro kuanzia Kimara Mwisho kuelekea Segerea na Kinyerezi.
Kwa watakaotumia usafiri wa gari/daladala wanashauriwa washuke kwenye kituo cha kwa Mashaka na waulize BS Grocery ilipo.
Mgeni rasmi kwenye mkutano huo atakuwa Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa, Mh.Heche akimwakilisha Mh.Dr.Wilibroad Slaa ambaye amepata dharura. Vile vile, viongozi wengine wa kitaifa kupitia CHADEMA wanaotarajiwa kuambatana na Mh. Heche ni pamoja na makamanda wafuatao: Mh. Mnyika, Tundu Lissu, Mh. Zitto, Halima Mdee na Mr Sugu. Kabla ya Mkutano huo kutakuwa na shughuli za uzinduzi wa Matawi na kusimika misingi ya CHADEMA kwenye mitaa yote ya Kata ya Kimara.
Aidha, kwenye Mkutano huo wa hadhara Mh. Heche anatarajiwa kuzindua Tawi la Mavurunza pamoja na harambee kwa ajili ya ofisi ya Tawi hilo, kupokea wanachama wapya na kuhutubia wanachama, wadau na wananchi kwa ujumla akipewa support ya nguvu kutoka kwa makamanda atakoambatana nao. Hakika CHADEMA itatikisa tena Kimara, Mtaa wa Mavurunza
Hivyo, ukiwa kama mwanachama au mdau muhimu wa CHADEMA, unaombwa kuhuduria mkutano huo muhimu sana bila kukosa.
Nawasilisha