CHADEMA & Kushindwa: The Future!

napenda kuuliza Bw. Malecela, kama ulikuwa mfuatiliaji wa kesi hii na ushahidi ulokuwepo Je haki imetendeka? Be honest na Mungu kabla hujajibu, nahitaji Yes or No... Nitajadili baada ya jibu lako thx
 
Kwa hiyo nyinyi CDM mkishinda mmetendewa haki,mkishindwa hamkutendewa haki mtasubili sana! KIDUMU CHAMA TAWALA CHA CCM.

Kwa wizi na dhuluma kitadumu sana ila kwa haki na usawa hakitodumu!
 

- Yaani inaonyesha kwamba wewe ulishaamua hata kabla ya kesi kwamba hukumu iwe vipi, mimi sio the ishu hapa lakini sikuwahi kulalamika popote kwamba nimeonewa, again and again nimesema hivi:-

Nimerudi miezzi minne iliyopita baada ya kukaa nje kwa karibu miaka 30, lakini nikaweza kupita Secretariat, CC, Wabunge wa CCM, mpaka kwenye Finally full Bunge, that was a big achievement infact it speaks a lot about my future in politics za bongo.

- Otherwise, kukubali kushindwa ni kujenga utamaduni wa kukubali kwa amani kwa the future ya taifa, badala ya kujali taifa la leo tu!

William.
 
Wewe Mwenyewe ulishindwa kwenye kinyang'anyiro wa bunge la Afrika mashariki ukasema rushwa imetumika hata wapinzani walikuwa wanapokea rushwa . sasa hivi unamtetea mtu aliyekamatwa na masanduku ya kura? Wiliam jaribu hata kutumia saburi lako moja tu kufikiria vitu virahisi ambavyo havihitaji hat ubongo kufikiria
 

- Nimeishia kwenye wekundu tu, maana huwa ninaamini hoja nzito haipaswi kuwa na matusi, ikishakuwa nayo tu basi ni mufilisi na huwa siiisomi tena!

- Mkuu nakuomba tena kaangalie bingwa wa hoja Mzee Mwanakijiji, uone kama kuna mahali anatumia matusi kujenga hoja!


William.
 
Hata mimi kama ningekuwa naitwa Precise John Malecela ningeweza hilo jina la Malecela ni promo tosha
 

Kwa hiyo kwa mtizamo wako unataka kutuambia kuna uchaguzi wa huru na haki TZ kwa vile tu CDM huwa wanashida sometimes au?? Tatizo lenu CCM ni kufikiria kuwa Watanzania wote ni wajinga isipokuwa ninyi. Hizo propanganda zenu za kutaka watu waamini kuwa wapinzani hawakubali kushindwa zishaanza kukosa mshiko. Nyie wenyewe kwenye chaguzi za ndani hamuishi kuraramika na huwa mnasema wazi wazi kuwa kuna mazingira ya rushwa. Hili swala la kulalamika na rushwa kwenye chaguzi zenu hata wewe umetuambia humu. Sasa sijui unataka tuwaamini vipi tunapoona kuwa kuna mazingira ya kuporwa haki zetu?? Jaribuni kubadili strategies.
 

- Waheshimiwa Zitto, Januari, na Mbowe walisema maneno kama yangu, je na wao walishindwa ubunge wa EAC? I mean where is a common sense japo kidogo tu?

William.
 
Mahanga alikamatwa na masanduku ya kura alifikishwa kituo cha Polisi Buguruni kwa mshangao mkubwa order ikatoka juu Mahanga akaachiwa na jana mahakama imemwachia tena huru kwa mshangao wa hali ya juu. CCM mtabaka HAKI mpaka lini wananchi wamechoka kuonewa hii haki wameisubiri sana sasa itafika mahara watu watasema sasa baaaaasi.
 

Mkuu najua ulifurahi sana kutokana na hukumu ya jana, hivi unajua hata hukumu ilishavuja hata kabla ya jana kusiomwa na watu tayari walishasherekea toka wiki iliyopita jambo la kujiuliza nani aliivujisha? na alifanya huvyo kwa madhumuni gani? na kwanini alipata ujasiri wa kufanyua ivyo? .Unafikiri jaji angekuwa kwenye hali gani kama hukumu ingekuwa imevuja huku ikionyesha CHADEMA wameshinda?. Ukiweza kujibu maswali haya utajua vile mfumo wetu wa muhimili wa mahaka unatakiwa kufanyiwa mabadiliko makubwa. Nakushauri hebu kabla hujarudi NY. tembelea magereza yetu upate ushahidi ya watu wangapi wanateseka kwa kuvifungo vya kuonewa na kukomolewa.
 

- Haki sio wanaposhinda Chadema tu, hapana ni tabia potofu sana kwa jamii ambayo mnategemea kuja kuiongoza one day!

William.
 

- Myth!


William.
 
Sie MSAMIATI wetu; mahakama ni chombo cha HAKI pale maamuzi yanakuwa na faida kwetu na si vinginevyo;

Tumeshuhudia tukitendewa haki; Singida, Biharamuro, Mbozi

Tumeshuhudia tukinyimwa haki; Arusha Mjini, Shinyanga Mjini, Segerea

Tuache uzembe hatuwezi kukubali kila maamuzi bila kuangalia msingi wa kuyafikia hayo maamuzi.Kama jana mahakama ilitenda haki haimaanishi juzi pia ilitenda haki na kesho itatenda haki.embu tusimame kwenye ukweli tusiwe kama makondakta wa daladala,kila siku wanadanganya,siti za kumwaga wakati ukichungulia tu njemba zimebanana hata kugeuka haiwezekani
 
Kweli Magamba ni Magamba tu, hata uyapake rangi vipi yataendelea kuwa Magamba! Hivi wewe unadhani kama kungekuwa hakuna kubebana ungefika kote huko? Sasa unatoa wapi ujasiri wa kujitapa hapa? Unadhani angekuwa mtoto wa Mkulima japo kakaa Tz miaka 30 Chama cha Magamba kingem-shortlist? Wewe shukuru tu kuwa kubebana kwa Magamba ndio kulikufikisha hatua hiyo, ila kwakuwa HUNA SIFA HATA MOJA ndio maana Bungeni ukaangukia Pua. Yaani kwa mtazamo huu heri ungefikiria kimasaburi kuliko kigogo! Mpuuuuzi kweli wewe!
 

Malecela! Kuna tofauti kubwa kati ya mahakama na haki, and as between judgement and justice. Not every judgement gives justice! Ulitaka Chadema wasilalamikie uozo wa mahakama? Nani asiyejua mahakama zetu zina serve executive? Or let me ask you, do you honestly believe that Mahanga won the case fairly?
 
Kwani William ni wapi ume-quote msimamo wa Chadema kama chama kuwa Mahakama haikutenda haki? Unafikiri kwa kutumia nini William?

I know you know we know you are not that smart (you know what I mean Le mutuz big show...ha. ha. ha: Stupid!)
:car:
 

Mkuu ulichosema ni kweli kabisa maana hata ukiangalia kesi ya Arusha police walimiminwa wengi kuliko kawaida inamaana kilichokuwa kinatokea kilijulikana ila hii ya segerea ikawa je ulinzi haukuimarika hivyo? Na nakumbuka kuna thread moja nilisoma last wik hapa ilikuwa ikimsema huyu aliyeshinda aliyeshaanza kujitamba mtaani kuwa ile keshamaliza kila kitu
 

Willium

Ni vema tukawa wakweli kwa nafsi zetu, Mahanga yeye ndio alianza kujitangazia ushindi akiwa Arusha siku Nne kabla ya hukumu kutolewa na ushahidi upo, sasa tujiulize yeye hizo taarifa alizipata wapi???? nachojaribu kusema hapa ni kwamba kwenye mahakama zetu hakuna haki hususani kama umetofautiana na watawala kama Mpendazoe.. Tunatambua jamaa anaonewa kwa kitendo chake cha kuondoka CCM. hilo halina ubishi hata kiodgo

Kuhusu mafanikio yako, sidhani kama unaitendea nafsi yako haki uliingia kwenye kinganganyiro ili ushinde na sio ushindwa hii ilikuwa strategy yako tangu mwanzo.. Unaposema mafanikio wakati ulishindwa na kambi yako ilikuwa inalalama kwamba kuna wabaya wako kisiasa walitumia pesa nyingi ili ushindwe mie sikuelewi kabisa
 

Willie,

Kama utanifuatilia vizuri utajua mimi ni mmoja wa watu ambao walikuwa wanakukubalia sana sana.. Toka enzi za kina Rev. Kishoka kabla ya hawa kina Rejao na Ritz hawajavamia jamvi. Lakini naanza kujiuliza kwamba umekutwa na kitu gani. Ni kuwa CCM tuu au kuja kwenye hali ya hewa ya Tanzania na hili vumbi linaanza kukuharibu upeo wako wa kufikiri na kuelewa mambo.

Mbona kwenye kesi za chaguzi zote hii ya Segerea ilikuwa nyepesi sana haikuhitaji Jaji kuamua ? Hata mtu wa mwaka wa kwanza wa kitivo cha habari au utamaduni anaweza kuamua na kupatia kabisa... Mbona hata wana CCM walio wengi kama sio wote walikuwa wanajua hii kwao ni ngumu.. Kuna wakati nilikutana na mtu mmoja ana nafasi ya juu katika CCM tukaliongelea suala hili akasema hii imekaa vibaya sana kwao lakini wanajaribu kuuibadilisha iwe in CCM's favor ingawa walikuwa wanajua itawaletea sana kashfa na Jaji hali kadhalika. Yeye kwa mtazamo wake alisema namnukuu.... " unajua mimi niliwaeleza kuwa tukubali tuachane nalo tukubali kushindwa... Ila kuna msukumo wa hali ya juu kuwa Makongoro Mahanga ashinde kwani ni kijana wa EL. Na kama wakiweza kumshindisha Mahanga basi nitaamini kuwa sisi CCM hatuna aibu na hatuitakii hii nchi mema...." mwisho wa kunukuu..

Kwa kuwa huyo mtu ninamheshimu sana sana sikutaka kumpiga maswali mojawapo kuwa na yeye ni mmoja wa wasioitakia mema hii nchi... Sasa kaka Willie tafadhali hebu tafakari na chukua hatua...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…