jaba jumah
Senior Member
- Sep 24, 2015
- 150
- 50
Viongozi wa 4um na viongozi wa boda boda wa mkoa wa mbeya wameamua kuhama chadema na kujiunga na ccm kutokana na mambo maovu yanayo endelea ndani ya chadema na ukawa kwa ujumla hali hyoo imekwa ikiendelea kwa muda mrefu jambo ambalo limepelekea sintofaham ya viongoz hao wa 4um na kushindwa kueshimiana kati ya viongozi wa cdm na viongoz hao wa 4um kwa kauli yao moja wamesema watahakikisha wanampigania dr, magufuli na kumnadi nyumba kwa nyumba hadi kieleweke na mwishowe kuibuka na ushindi wa kimbunga,,,, tumekuja pahala salama kabisa na sehem ya kwenda ikulu......................
TAARIFA KWA UMMA
Kumekuwa na uvumi na uzushi unaosambaa baada ya watu wasiotakia mema 4u Movement kufanya "press conference"na kujitambulisha kuwa wao ni viongozi wa 4u Movement mkoa wa Mbeya na wamehama kutoka 4u Movement friends of lowassa na kuhamia kwa Magufuli.
Uongozi wa 4u Movement imesikitishwa sana na uzushi huo,kwani Mratibu wa 4u Movement mkoa wa mbeya ambaye anatambulika kwa jina la Robert Elia na msaidizi wake Samwel Hume hawajahama 4u movement wapo na wanaendelea na majukumu yao ya kila siku.
Uongozi wa 4u Movement unawataka wanachama wake wote kuupuza uzushi huo kwani hauna mashiko wala ukweli wowote na ni dalili za watu walioishiwa mbinu na maarifa.
Imetolewa na
Vian Nchimbi
Mratibu Msaidizi Taifa
Utumishi
Uwajibikaji
Umoja
Uzalendo
www.4u Movement.com