CHADEMA Kigoma wampania Zitto

CHADEMA Kigoma wampania Zitto

Status
Not open for further replies.
Hivi wale wazee wa Mbowe waliomchukulia fomu wamefia wapi.

Teh teh teh
 
Basi wewe huna kumbukumbu, umeandikathread ndefu nimesoma mstari mmoja tu wa kwanza na nakujibu. Zito alitangaza kutokugombea ubunge 2009, kuwa ataenda Ujerumani kusoma, acha uongo wako.
 
Baraza la Vijana Chadema (Bavicha) Mkoa wa Kigoma, limesema litamshughulikia Zitto Kabwe iwapo ataamua kugombea ubunge katika Jimbo la Kigoma Mjini badala ya Kigoma Kaskazini.

Akihutubia wakazi wa Kata ya Gungu mjini hapa juzi, mwenyekiti wa baraza hilo, Omary Gindi alisema wamejiandaa kushinda ubunge na kutetea nafasi ya kuongoza Halmashauri ya Kigoma Ujiji kama walivyofanya mwaka 2010.

Gindi alisema watambana baada ya Zitto kudai hatagombea kwenye jimbo alilokuwa anaongoza kupitia Chadema na badala yake amejipanga kugombea katika Jimbo la Kigoma Mjini kubadilisha na Peter Serukamba (CCM).

“Zitto aje tu hapa Kigoma Mjini. Tutamuuliza aliwafanyia nini watu wa jimbo lake kiasi kwamba amemaliza kero zao na kuamua kuhama, vinginevyo tutawaeleza wananchi kwamba hafai na amekimbia kwao kwa sababu wananchi wamemwambia hawatamchagua tena kutokana na kushindwa kushirikiana na wapiga kura wake,” alisema Gindi.

Alisema watu wa Kigoma wanaipenda na kuiunga mkono Chadema kwa vile baadhi yao walifungwa jela, kupoteza mali, kujeruhiwa na kupata ulemavu na wengine kukosana na wake au waume zao, jambo lililowafanya kujiona ni sehemu ya chama hicho.

Katibu wa Chadema Mkoa wa Kigoma, Shaaban Madede aliwaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.

“Lazima mhakikishe CCM inang’oka madarakani ili Chadema iweze kuongoza dola na kupigania masilahi ya watu, kwa vile sehemu nyingi kuna kero ya huduma mbovu za elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara vijijini, suluhisho pekee ni kuiondoa CCM madarakani,” alisema Madede.

Source: Mwananchi
Mkuu labda ungesema CCM ndiyo wametoa hiyo kauli lakini siyo Chadema.

Kigoma Mjini Chadema hakuna, soma hii kiduchu.

Katika uchaguzi mkuu wa waka 2005, CHADEMA ilipata pigo kubwa Kigoma Mjini. Peter Serukamba wa CCM ndiye alishinda katika jimbo hili kwa kura 29,281 (55.7%) dhidi ya kura 21,720 (41.3%) za Dr. Warid Kabourou. Ushindi huu wa CCM ulitokana pia na nguvu ya mgombea urais wake, Jakaya Mrisho Kikwete ambaye naye alipata asilimia 71.2 ya kura za Urais.Siasa zile za mapambano yanayovutia zilizoendeshwa na Kabourou zikamalizwa na kijana wa miaka 38 tu wakati huo. Baada ya kuangushwa mara hii, Walid Kabourou aliamua kuupa upinzani kisogo na akatimkia CCM ambako yuko hadi hivi sasa.Mwaka 2010 CCM haikuacha kumrejesha Peter Serukamba safari hii akiwa na uzoefu wa ubunge kwa miaka mitano, naye hakufanya makosa, alishinda ubunge wa Kigoma Mjini kwa kura 20,594 (47.87%) dhidi ya Ally Khalfan Mleh wa CHADEMA ambaye alipata kura 19,414 (45.12%). Serukamba wa CCM alimpita Mleh wa CHADEMA kwa asilimia 2.75 tu ya kura.-

Haya tuambie hao wanaojiita Chadema wapo wapi.
 
Hivi wale wazee wa Mbowe waliomchukulia fomu wamefia wapi.

Teh teh teh

Tei teh teh hawa wahuni kwa maigizo wamefuzu. Najutia sana miaka yangu yote niliyomaliza huko msituni napigania ukombozi wa pili. Nilidhani niko na watu wenye nia safi kumbe manyang'au wanaoongozwa na tamaa tu. We unashangaa igizo la wazee wa kigoma kumchukulia fomu mbowe?

Kuna lile la Mchange kutaka kutungua helkopta ya dk.slaa..hahahahahahahaha tanzania hakuishi vituko na maajabu ya dunia.
 
Acha kupoteza muda,Kigoma hakuna tena chama kinachoitwa chadema.

Kwa sasa Kigoma ukiskia mtu yupo chadema basi anataka fedha za mbowe kama ilivyo kwa wapambe wa Lowassa ambao wanampiga pesa tu halafu kimoyomoyo wana mdis
Kama ambavyo Zitto alipewa pesa Tshs 15 mil + Gari na Mbowe huyo huyo kwaajili ya kampeni zake 2005
 
Zitto anaweza asishinde majimbo ya Kaskazini tu na hii sio kwamba watakao shinda ndio wanakubalika, hapana ni kutokana na Siasa zao za Ukanda na Udini vinginevyo Zitto jimbo lolote lile ndani ya Tanzania hii anashinda.
 
Zitto anaweza asishinde majimbo ya Kaskazini tu na hii sio kwamba watakao shinda ndio wanakubalika, hapana ni kutokana na Siasa zao za Ukanda na Udini vinginevyo Zitto jimbo lolote lile ndani ya Tanzania hii anashinda.

Mwambie aje arusha
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom