Makete Kwetu
JF-Expert Member
- Jan 8, 2012
- 531
- 166
Baraza la Vijana Chadema (Bavicha) Mkoa wa Kigoma, limesema litamshughulikia Zitto Kabwe iwapo ataamua kugombea ubunge katika Jimbo la Kigoma Mjini badala ya Kigoma Kaskazini.
Akihutubia wakazi wa Kata ya Gungu mjini hapa juzi, mwenyekiti wa baraza hilo, Omary Gindi alisema wamejiandaa kushinda ubunge na kutetea nafasi ya kuongoza Halmashauri ya Kigoma Ujiji kama walivyofanya mwaka 2010.
Gindi alisema watambana baada ya Zitto kudai hatagombea kwenye jimbo alilokuwa anaongoza kupitia Chadema na badala yake amejipanga kugombea katika Jimbo la Kigoma Mjini kubadilisha na Peter Serukamba (CCM).
"Zitto aje tu hapa Kigoma Mjini. Tutamuuliza aliwafanyia nini watu wa jimbo lake kiasi kwamba amemaliza kero zao na kuamua kuhama, vinginevyo tutawaeleza wananchi kwamba hafai na amekimbia kwao kwa sababu wananchi wamemwambia hawatamchagua tena kutokana na kushindwa kushirikiana na wapiga kura wake," alisema Gindi.
Alisema watu wa Kigoma wanaipenda na kuiunga mkono Chadema kwa vile baadhi yao walifungwa jela, kupoteza mali, kujeruhiwa na kupata ulemavu na wengine kukosana na wake au waume zao, jambo lililowafanya kujiona ni sehemu ya chama hicho.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Kigoma, Shaaban Madede aliwaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.
"Lazima mhakikishe CCM inang'oka madarakani ili Chadema iweze kuongoza dola na kupigania masilahi ya watu, kwa vile sehemu nyingi kuna kero ya huduma mbovu za elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara vijijini, suluhisho pekee ni kuiondoa CCM madarakani," alisema Madede.
Source: Mwananchi
Akihutubia wakazi wa Kata ya Gungu mjini hapa juzi, mwenyekiti wa baraza hilo, Omary Gindi alisema wamejiandaa kushinda ubunge na kutetea nafasi ya kuongoza Halmashauri ya Kigoma Ujiji kama walivyofanya mwaka 2010.
Gindi alisema watambana baada ya Zitto kudai hatagombea kwenye jimbo alilokuwa anaongoza kupitia Chadema na badala yake amejipanga kugombea katika Jimbo la Kigoma Mjini kubadilisha na Peter Serukamba (CCM).
"Zitto aje tu hapa Kigoma Mjini. Tutamuuliza aliwafanyia nini watu wa jimbo lake kiasi kwamba amemaliza kero zao na kuamua kuhama, vinginevyo tutawaeleza wananchi kwamba hafai na amekimbia kwao kwa sababu wananchi wamemwambia hawatamchagua tena kutokana na kushindwa kushirikiana na wapiga kura wake," alisema Gindi.
Alisema watu wa Kigoma wanaipenda na kuiunga mkono Chadema kwa vile baadhi yao walifungwa jela, kupoteza mali, kujeruhiwa na kupata ulemavu na wengine kukosana na wake au waume zao, jambo lililowafanya kujiona ni sehemu ya chama hicho.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Kigoma, Shaaban Madede aliwaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.
"Lazima mhakikishe CCM inang'oka madarakani ili Chadema iweze kuongoza dola na kupigania masilahi ya watu, kwa vile sehemu nyingi kuna kero ya huduma mbovu za elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara vijijini, suluhisho pekee ni kuiondoa CCM madarakani," alisema Madede.
Source: Mwananchi