Unaweza kusema hivi kama tu hunifuatilii na hujui ninachosimamia, wala si mara ya kwanza kusema hili, na ninavyobonda CHADEMA ujue nishabonda CCM maradufu. Kuanzia Kikwete, Malecela, Msekwa, Chiligati etc, "Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea" mpaka Nyerere mwenyewe ambaye hata CHADEMA hawawezi kumgusa, nipo on record hapa JF nishawaua sana tu, sasa sielewi unavyosema mimi ni CCM una maana gani.
Kwa hiyo huwezi kusema hata siku moja kwamba mimi ni mtetezi wa CCM.
Tatizo lenu mna operate kwa kutumia one track mind, kwamba mtu yeyote anayebondea CHADEMA ni kibaraka wa CCM. Hamjui kwamba kuna watu haturidhiki na uongozi wote wa kisiasa Tanzania, si CCM wala CHADEMA. Na tukibondea "chama mbadala" haina maana kwamba tunaunga mkono CCM.
Hili linakuwa gumu sana kuonekana kwa simpleton wa kufikiri "if you are not with us, you are with our enemy" mimi naweza kuwa siko na ninyi na wala sipo na enemies wenu CCM.
Uki expose hii simplicity of thought unanionyesha sababu zaidi kwa nini niko sawa kuwa critical of your lot.