Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 21,179
- 37,475
Heshima sana wanajamvi wote.
Kwanza napenda kuwajulisha wanajamvi wote Ngongo si mwanachama wa chama chochote cha siasa Tanzania ila ni mpenzi wa siasa.Ninaposema ni mpenzi wa siasa nina maana ninapenda kushiriki,kusikiliza na kushauriana masuala yote yahusuyo siasa bila kuwa mwanachama wa chama cha siasa.Kwahiyo unapochangia mjadala huu ni vyema ukijikita zaidi katika hoja.
Ni jambo lililo wazi Tanzania inapita katika kipindi kigumu sana tangu kuhasisiwa kwa taifa hili.Vikao vya bunge maalamu la kutunga katiba mpya vinaendelea mjini Dodoma huku baadhi ya wajumbe (UKAWA) wa bunge hilo wakisusia vikao hivyo kwasababu ambazo kwa kiasi fulani hata mimi nakubaliana nazo.Sina haja ya kueleza kwanini tumefikia hapa kwakuwa najua wengi wenu tunazijua sababu hizo ingawa kumekuwa na juhudi kubwa za kimkakati/propaganda za kupotosha kwa maksudi sababu zilizopelekea UKAWA kususia bunge la katiba.
Vyombo vya habari hasa vile vinavyomilikiwa na serekali na chama tawala vimekuwa vikipotosha ukweli kwa makusudi ya kupandikiza taswira mbaya ya UKAWA mbele ya macho ya jamii ya kitanzania hasa wale wasiopenda kuchambua mambo kwa undani.
CHADEMA sijui kama UKAWA wamo katika hii hoja ya maandamano wamekuwa wakipaza sauti za malalamiko na sasa wanataka kuanzisha maandamano nchi nzima kama sehemu ya kuonyesha kutorizishwa na jinsi mchakato wa kuandika katiba mpya unavyopaswa kwenda.Ni kweli bunge la Bwana Sitta limekosa viwango,limekosa ushirikishwa wa mawazo ya wananchi,limejivika kazi za tume ya kukusanya maoni,limekosa mjumuiko wa makundi yote (wanaCCM wametamalaki),limekataa mawazo ya wananchi,limekumbatia mawazo ya watawala.halina maana kabisaaaaa.
Ukweli ni kwamba sababu za kuandamana zipo nyingi sana lakini Ngongo wa JF anakataa maandamano kwasababu ambazo nitazieleza.
Maandamano hayajawahi kuleta mabadiliko chanya Tanzania badala yake yameacha makovu makubwa ambayo hatujawahi kuona matunda yake hata kidogo. Mji wa Arusha ni mfano mzuri wananchi waliandamana kudai uchaguzi wa haki wa meya wa Jiji la Arusha mpaka leo bado meya ni yuleyule na ikumbukwe kuna wananchi walipoteza maisha yao kwaajili ya kuhakikisha haki inapatikana.
Kwanini nakataa maandamano sasa.Nakataa maandamano kwasababu wananchi waliopoteza maisha yao kwaajili ya kuitikia wito wa maandamano mpaka leo hawajatendewa haki.Kuna wanawake leo hii ni wajane wana watoto wanashindwa kupata elimu,afya,lishe stahiki kwakuwa hawana Baba wa kuwatunza.CDM kama chama mpaka leo hawajachukua hatua za kisheria kuhakikisha walioshiriki kutoa uhai wa raia wasiokuwa na silaha wanafikishwa mahakamani,sijasikia wanasheria wa CDM wakisubutu kuanzisha mchakato wa kuishitaki serekali ICC kwa mauaji ya raia.
CDM ilidai ina mkanda wa watu walioshiriki kurusha bomu uwanja wa Soweto Arusha,tena walidai polisi walishiriki kuhakikisha mrusha bomu hakamatwi na raia kwa kurusha risasi ili kumkinga asikamatwe.Siju huo mkanda umewekwa kwaajili gani wakati inajulikana kuna wananchi walipoteza maisha yao pasipo sababu za maana.Ikiwa CDM kweli ina mkanda ni kwanini mpaka leo bado imeukali inasubiri nini kwaajili ya manufaa ya nani au ndio mtaji wake mwaka 2015 ?.Vipi waliopoteza maisha au baada ya kuzikwa na kupiga mapicha za mazishi ndio basi.
CDM iache kucheza na maisha ya watanzania kama kweli inataka maandamano lazima watueleze wananchi walipoteza maisha wamefanyiwa nini ?.Tunajua upande wa serekali imefanya nini kwa makamanda wa mikoa yote yalipofanyika mauaji wengi wamepandishwa vyeo kwa kazi nzuri na njema ya kusimamia mauaji ya wananchi upande wa CDM watuambie familia za waanga wa maandamano na mikutano yake wamewafanyia nini ?.
Naomba kuwasilisha.
Kwanza napenda kuwajulisha wanajamvi wote Ngongo si mwanachama wa chama chochote cha siasa Tanzania ila ni mpenzi wa siasa.Ninaposema ni mpenzi wa siasa nina maana ninapenda kushiriki,kusikiliza na kushauriana masuala yote yahusuyo siasa bila kuwa mwanachama wa chama cha siasa.Kwahiyo unapochangia mjadala huu ni vyema ukijikita zaidi katika hoja.
Ni jambo lililo wazi Tanzania inapita katika kipindi kigumu sana tangu kuhasisiwa kwa taifa hili.Vikao vya bunge maalamu la kutunga katiba mpya vinaendelea mjini Dodoma huku baadhi ya wajumbe (UKAWA) wa bunge hilo wakisusia vikao hivyo kwasababu ambazo kwa kiasi fulani hata mimi nakubaliana nazo.Sina haja ya kueleza kwanini tumefikia hapa kwakuwa najua wengi wenu tunazijua sababu hizo ingawa kumekuwa na juhudi kubwa za kimkakati/propaganda za kupotosha kwa maksudi sababu zilizopelekea UKAWA kususia bunge la katiba.
Vyombo vya habari hasa vile vinavyomilikiwa na serekali na chama tawala vimekuwa vikipotosha ukweli kwa makusudi ya kupandikiza taswira mbaya ya UKAWA mbele ya macho ya jamii ya kitanzania hasa wale wasiopenda kuchambua mambo kwa undani.
CHADEMA sijui kama UKAWA wamo katika hii hoja ya maandamano wamekuwa wakipaza sauti za malalamiko na sasa wanataka kuanzisha maandamano nchi nzima kama sehemu ya kuonyesha kutorizishwa na jinsi mchakato wa kuandika katiba mpya unavyopaswa kwenda.Ni kweli bunge la Bwana Sitta limekosa viwango,limekosa ushirikishwa wa mawazo ya wananchi,limejivika kazi za tume ya kukusanya maoni,limekosa mjumuiko wa makundi yote (wanaCCM wametamalaki),limekataa mawazo ya wananchi,limekumbatia mawazo ya watawala.halina maana kabisaaaaa.
Ukweli ni kwamba sababu za kuandamana zipo nyingi sana lakini Ngongo wa JF anakataa maandamano kwasababu ambazo nitazieleza.
Maandamano hayajawahi kuleta mabadiliko chanya Tanzania badala yake yameacha makovu makubwa ambayo hatujawahi kuona matunda yake hata kidogo. Mji wa Arusha ni mfano mzuri wananchi waliandamana kudai uchaguzi wa haki wa meya wa Jiji la Arusha mpaka leo bado meya ni yuleyule na ikumbukwe kuna wananchi walipoteza maisha yao kwaajili ya kuhakikisha haki inapatikana.
Kwanini nakataa maandamano sasa.Nakataa maandamano kwasababu wananchi waliopoteza maisha yao kwaajili ya kuitikia wito wa maandamano mpaka leo hawajatendewa haki.Kuna wanawake leo hii ni wajane wana watoto wanashindwa kupata elimu,afya,lishe stahiki kwakuwa hawana Baba wa kuwatunza.CDM kama chama mpaka leo hawajachukua hatua za kisheria kuhakikisha walioshiriki kutoa uhai wa raia wasiokuwa na silaha wanafikishwa mahakamani,sijasikia wanasheria wa CDM wakisubutu kuanzisha mchakato wa kuishitaki serekali ICC kwa mauaji ya raia.
CDM ilidai ina mkanda wa watu walioshiriki kurusha bomu uwanja wa Soweto Arusha,tena walidai polisi walishiriki kuhakikisha mrusha bomu hakamatwi na raia kwa kurusha risasi ili kumkinga asikamatwe.Siju huo mkanda umewekwa kwaajili gani wakati inajulikana kuna wananchi walipoteza maisha yao pasipo sababu za maana.Ikiwa CDM kweli ina mkanda ni kwanini mpaka leo bado imeukali inasubiri nini kwaajili ya manufaa ya nani au ndio mtaji wake mwaka 2015 ?.Vipi waliopoteza maisha au baada ya kuzikwa na kupiga mapicha za mazishi ndio basi.
CDM iache kucheza na maisha ya watanzania kama kweli inataka maandamano lazima watueleze wananchi walipoteza maisha wamefanyiwa nini ?.Tunajua upande wa serekali imefanya nini kwa makamanda wa mikoa yote yalipofanyika mauaji wengi wamepandishwa vyeo kwa kazi nzuri na njema ya kusimamia mauaji ya wananchi upande wa CDM watuambie familia za waanga wa maandamano na mikutano yake wamewafanyia nini ?.
Naomba kuwasilisha.