CHADEMA inavyoliangamiza Taifa!

CHADEMA inavyoliangamiza Taifa!

Katibu mkuu wa CHADEMA taifa kwa sasa yuko hoi bin taabani kuongoza chama chake, ambacho hivi karibuni kiliweza kujizolea sifa hapa nchini, kwa kile kinacho daiwa kuwa kiliweza kutoa changamoto kubwa kwa chama tawala (CCM).

Jambo la kushangaza na kushtua kuhusu hiki chama, ni kuporomoka kwa umaarufu wake nchini, baada ya watanzania kugundua kuwa sio chama cha 'demokrasia' na 'maendeleo' kama wanavyo jipambanua, ila ni chama cha vurugu, fujo na maandamano yenye kuhatarisha amani na utulivu wa nchi.

Sifa hizi mpya kwa chama hiki, ambazo ni fujo na vurugu, zimetolewa na wananchi baada tu ya CHADEMA kumpa mamlaka Dr Slaa ya kuwa mtendaji mkuu wa chama hicho, Dr Slaa kwa siasa na mbinu zake, alidhani kwa kutumia maandamano basi ndio itakuwa njia pekee ya kuzidi kuinua jina na hadhi ya chama, kumbe imekuwa kinyume chake.

Mikakati ya Dr Slaa ya kuleta mageuzi ya siasa hapa nchini kupitia chama chake (CHADEMA) na washirika wake IMEDODA, na badala yake mikakati hiyo imefanikiwa kuondoa na kutokomeza kabisa sentensi isemayo "Tanzania ni kisiwa cha amani", na kwa sasa kuwa kisiwa cha wahanga wa mabomu.

Hoja ya msingi hapa ni kwamba, kama Dr Slaa amechemka na yuko hoi kuiongoza CHADEMA kwenye kufanya siasa za kistaarabu na safi. Je, atawezaje kuongoza nchi yetu yenye changamoto za kila aina?, haya ni mambo ya msingi sana kuhoji, kwani kushabikia uozo ambao utaenda kuliangamiza taifa sio UZALENDO hata kidogo.

Hata mkitumia nguvu na pesa na Policcm hamtaweza kuidhoofisha Chadema.
Mnajitoa ufahamu na kujivalisha miwani ya mbao msilione anguko kubwa la ccm, mnahaha kuanzisha thread ya kuichafua chadema nina hakika hamtafanikiwa.

Mtashindana sana..... lakini HAMTASHINDA!!???!
 
Inaonekana bdo wewe upo analogue na haupo kwenye sayari hii yenye mfumo mwngne na fikra tofauti. Kwa kukusaidia huwezi kuwabadili watu ila watu ndio wanaobadlka kutoka na uhalisia. Kwa karne hii huwezi kukaa kmnya kama kipind cha zidumu fikra za fulani.... Kwan uelewa umeongezeka wananchi wanajua wapi kimbilio. Ndg yangu unadalili za ccmonia njoo upewe chademaquin kwa afya yako
 
Katibu mkuu wa CHADEMA taifa kwa sasa yuko hoi bin taabani kuongoza chama chake, ambacho hivi karibuni kiliweza kujizolea sifa hapa nchini, kwa kile kinacho daiwa kuwa kiliweza kutoa changamoto kubwa kwa chama tawala (CCM).

Jambo la kushangaza na kushtua kuhusu hiki chama, ni kuporomoka kwa umaarufu wake nchini, baada ya watanzania kugundua kuwa sio chama cha 'demokrasia' na 'maendeleo' kama wanavyo jipambanua, ila ni chama cha vurugu, fujo na maandamano yenye kuhatarisha amani na utulivu wa nchi.

Sifa hizi mpya kwa chama hiki, ambazo ni fujo na vurugu, zimetolewa na wananchi baada tu ya CHADEMA kumpa mamlaka Dr Slaa ya kuwa mtendaji mkuu wa chama hicho, Dr Slaa kwa siasa na mbinu zake, alidhani kwa kutumia maandamano basi ndio itakuwa njia pekee ya kuzidi kuinua jina na hadhi ya chama, kumbe imekuwa kinyume chake.

Mikakati ya Dr Slaa ya kuleta mageuzi ya siasa hapa nchini kupitia chama chake (CHADEMA) na washirika wake IMEDODA, na badala yake mikakati hiyo imefanikiwa kuondoa na kutokomeza kabisa sentensi isemayo "Tanzania ni kisiwa cha amani", na kwa sasa kuwa kisiwa cha wahanga wa mabomu.

Hoja ya msingi hapa ni kwamba, kama Dr Slaa amechemka na yuko hoi kuiongoza CHADEMA kwenye kufanya siasa za kistaarabu na safi. Je, atawezaje kuongoza nchi yetu yenye changamoto za kila aina?, haya ni mambo ya msingi sana kuhoji, kwani kushabikia uozo ambao utaenda kuliangamiza taifa sio UZALENDO hata kidogo.


View attachment 98558 Mwana-CHADEMA akiwa na majeraha baada ya kupata kichapo stahiki kufuatia kukaidi kwake maagizo ya jeshi la polisi.


View attachment 98559Vijana wakiwa wameshawishika kuandamana na CHADEMA baada ya kunyweshwa viroba katika utekelezaji wa mpango mkakati wa Dr Slaa wa kuleta mageuzi ya siasa nchini.
kaka unapoteza muda wako kuandika upuuzi, watanzania wanakushangaa wewe na chama chako kinachoelekea jehamam; ndiyo maana mmeanza kupanga mbinu chafu za kuharibu amani ya nchi, shame on you.
 
Inaonekana bdo wewe upo analogue na haupo kwenye sayari hii yenye mfumo mwngne na fikra tofauti. Kwa kukusaidia huwezi kuwabadili watu ila watu ndio wanaobadlka kutoka na uhalisia. Kwa karne hii huwezi kukaa kmnya kama kipind cha zidumu fikra za fulani.... Kwan uelewa umeongezeka wananchi wanajua wapi kimbilio. Ndg yangu unadalili za ccmonia njoo upewe chademaquin kwa afya yako

Kama kweli hayo unayoyasema, kuwa wananchi wamebadlika na wanajua wapi kimbilio, sasa kuna haja gani ya CHADEMA kuwashwa na kufanya maandamano yao?

Si wasubiri uchaguzi ufike ili wananchi hao hao mnaosema wamebadilika waitoe CCM na wawape CHADEMA!

Kwanini kama mna amini wananchi wana lijua kimbilio lao, iweje muandae maandamano ya mara kwa mara? hii ni kero kubwa kwa wastaarabu na wapenda amani. Iweje CHADEMA ivurugie watu shughuli zao za kuzalisha kipato kwa maandamano?
 
Mimi nafikiri hawa wtu wanaoleta hizi mada huku wachukue likizo kidogo wiki hii walau waache watu waomboleze. Huu moshi wa kifisadi polepole utageuka kuwa moto. Mtaungulia ndani na ccm yenu utajaniambia.
 
Hayo uliyosema yote hayawezekani kwa Tanzania iliyojaa ufisadi wa kila aina

"To know the enemy is half the victory"
 
hii thread ilibidi waandikie ccm na mapoliccm wanaokandamiza demokrasia nchini
 
Kama kweli hayo unayoyasema, kuwa wananchi wamebadlika na wanajua wapi kimbilio, sasa kuna haja gani ya CHADEMA kuwashwa na kufanya maandamano yao?

Si wasubiri uchaguzi ufike ili wananchi hao hao mnaosema wamebadilika waitoe CCM na wawape CHADEMA!

Kwanini kama mna amini wananchi wana lijua kimbilio lao, iweje muandae maandamano ya mara kwa mara? hii ni kero kubwa kwa wastaarabu na wapenda amani. Iweje CHADEMA ivurugie watu shughuli zao za kuzalisha kipato kwa maandamano?

Kama ni kuandamana si ni haki yao? Mbona huulizi wanaowapiga mabomu wanataka nini. Kwa nini mikutano yao ikiachwa huwa inamalizika vizuri tu, lakini wakiwepo polisi ndipo tatizo linapokuwepo pia? Hujiulizi? Nani chanzo cha tatizo? Mwaka jana polisi waliwazuia waumini wa Kiislamu kukutana Kidongo Chekundu kama sikosei, lakini waumini hao walisema polisi hawana ubavu wa kuwazuia na kwa vile polisi walishindwa kuwadhibiti kulingana na umati mkubwa ilibidi wawaachie tu na hakuna maafa yoyote yaliyotokea na wala hakuna mtu aliyeumia. Lakini kama wangerusha mabomu au kuwapiga raia si maafa au kuumizwa watu kungetokea? Sasa kwa akili yako tatizo liko kwa nani? Hapa naona polisi wanadhindana na dhana "demokrasia" - kuwanyima watu uhuru wa kusema wanachofikiri au kukutana kwa ajili ya shughuli zao za kisiasa.
 
Katika viti vya udiwani 32 vilivyokua vinamilikiwa na CCM 8 kati ya ivo vimechukuliwa na chadema..
 
Mleta uzi amejipambanua kuwa anatatizo katika kufikiri,kutazama au kusikiliza pia.kuwalaumu cdm ambao ndiyo wanaotendewa hayo si haki katika nchi hii kwa wakati huu.NAKUOMBEA MUNGU AKUBADILI KWA KUDRA ZAKE.Sijui kama unajitambua( Selfawareness).Nisamehe nawaza kwa sauti.;Huyu ni mtumwa vile;Fikra,Kijamii na kiuchumi.Jambo ovu au udhalimu haufai bila kujali anafanyiwa nani !
 
Ndugu yangu Bakari,
Kuna DIFFUSION ya busara-yaani leo mtu aweza kuwa na busara kilo moja,kesho robo kile na keshokutwa theluthi?!
Ni wakati gani Kigwangallah huwa na constructive ideas-nje au ndani ya bunge?
Kama ni kote, kwa nini alishindwa kukubaliana na hoja ya Mh.James Mbatia kuhusu kufumua mfumo wa elimu nchini?!
Kama ni sehemu moja, kwa nini si ile nyingine?
Maneno ya busara ya Kigwangallah ni mwendelezo wa unafiki wa wabunge wa CcM kwa watanzania!
Anaunga mkono hoja,halafu anatema nyongo kuonesha matatizo yaliyoko jimboni mwake!
 
Kama kweli hayo unayoyasema, kuwa wananchi wamebadlika na wanajua wapi kimbilio, sasa kuna haja gani ya CHADEMA kuwashwa na kufanya maandamano yao?

Si wasubiri uchaguzi ufike ili wananchi hao hao mnaosema wamebadilika waitoe CCM na wawape CHADEMA!

Kwanini kama mna amini wananchi wana lijua kimbilio lao, iweje muandae maandamano ya mara kwa mara? hii ni kero kubwa kwa wastaarabu na wapenda amani. Iweje CHADEMA ivurugie watu shughuli zao za kuzalisha kipato kwa maandamano?

Mie sijakuelewa ndugu HAMY-D;
1. Hivi, CHADEMA huwa wanaandamana kila siku??!
2. Ni kweli kwamba siku CHADEMA wanayopanga kuandamana ndiyo wananchi wa maeneo hayo huwa na uhakika wa kujiingizia kipato kikubwa kuliko siku ambayo maandamano huwa hayapo?
3. Siku ya matembezi ya mshikamano, au mbio za mwenge, shughuli za watu huwa haziharibiki??!
4. Umaskini wa watanzania unatokana na nini-ni maandamano ya CHADEMA au mipango hovyo ya seriakali ya CcM?!
5. Kama ni kutokana na maandamano ya CHADEMA, Umaskini huo umeanza mwaka 1992?!
 
Sijawahi kuwasikia CHADEMA wakijitambulisha kwa udini, ukabila, ukanda, na ubinafsi kama mwandishi anavyodai. Hizi ni tuhuma ambazo CCM huwa wanazitoa dhidi ya CHADEMA bila kuwa na ushahidi wowote kuthibitisha tuhuma zao. Sana sana tunaona wabunge wa CCM wakiweka uchama Mbele kuliko utaifa na wabunge wa CHADEMA wakiweka utaifa Mbele wakati wakichangia hoja mbalimbali bungeni.

Lakini pia lazima mwandishi uelewe kuwa siyo kila anayepinga sera na mienendo ya CCM ni mwanachama au mshabiki wa CHADEMA vivyo hivyo siyo kila anayepinga mienendo na sera za CHADEMA ni mwanachama wa CCM. Kuna wachangiaji wengi ambao hawafungamani na chama chochote cha siasa na wanasukumwa na utaifa wao tu wakati wa kuchangia hoja.
 
Nadhani alichoongea mtoa mada kina logic ndano yake....so badala ya kumtukana ni vema mkamrekebisha mnapopaona amekosea na mazuri chukueni muyafanyie kazi......yale maoni waliyotoa ni ya kinazi....mimi si mfuasi wa siasa wala chama chochote ila jamaa ana logic ndani yake
 
Arusha ni mji wa kitalii na mlango wa kuingia TZ kwa watalii na wageni! walalahoi wengi hujipatia mkate wao tokana na sifa hizi za Arusha!
Kwanini chama cha upinzani CDM wanaitumia Arusha kuwa kitovu cha machafuko na misukosuko? kwanini hawaendi Kilimanjaro kulikoasisiwa Chadema? walalahoi wa Arusha wanataabika kwasababu Chadema wameamua kuwaadhibu wananchi wa Arusha kwa kuifanya Arusha kuwa mji wa maasi na machafuko ili Arusha iathirike kiuchumi na lengo lao la kuhujumu uchumi wa Arusha lifanikiwe!

Ombi langu kwa Wana Arusha wasikubali kutumiwa na CDM kuhujumu uchumi wa Arusha kwani watakaoathirika niwao na familia zao huku wenzao wa Kilimanjaro wakineemeka kwa kulinda amani na mshikamano wao!
 
Arusha ni mji wa kitalii na mlango wa kuingia TZ kwa watalii na wageni! walalahoi wengi hujipatia mkate wao tokana na sifa hizi za Arusha!
Kwanini chama cha upinzani CDM wanaitumia Arusha kuwa kitovu cha machafuko na misukosuko? kwanini hawaendi Kilimanjaro kulikoasisiwa Chadema? walalahoi wa Arusha wanataabika kwasababu Chadema wameamua kuwaadhibu wananchi wa Arusha kwa kuifanya Arusha kuwa mji wa maasi na machafuko ili Arusha iathirike kiuchumi na lengo lao la kuhujumu uchumi wa Arusha lifanikiwe!

Ombi langu kwa Wana Arusha wasikubali kutumiwa na CDM kuhujumu uchumi wa Arusha kwani watakaoathirika niwao na familia zao huku wenzao wa Kilimanjaro wakineemeka kwa kulinda amani na mshikamano wao!


Umeamka sasa ngapi ndugu yangu?
 
Ebu ondoa ugoro wako hapa.Unaonesha dhahiri jinsi viroba vya magamba vinakupelekesha.Acha uzuzu.
 
Back
Top Bottom