Elections 2010 Chadema imefikia kiwango cha nccr 1995?

reandle

JF-Expert Member
May 6, 2009
11,168
8,142
Naizungumzia NCCR ile iliyokuja kuibuka baada ya sakata la Mrema na Chavda! Naizungumzia NCCR iliyokuwa imemtunuku Mrema uenyekiti wa chama hicho mara baada ya kuihama CCM kwa mbwembwe(haijapata kutokea)! Naizungumzia NCCR ile ambayo Katibu Mkuu wake alikuwa Mabere Marando yule na sio huyu! Naizungumzia NCCR iliyokuwa na ma-striker hatari kama Dr. Masumbuko Lamwai ambae aliwasumbua CCM kuanzia Ubungo na kuja kuwachinjia Temeke! Naizungumzia NCCR iliyomsimamisha Mrema kama mgombea urais 1995 na kumtoa makamasi Mkapa licha kupita kupigiwa kampeni na Baba wa Taifa nchi nzima! NCCR ambayo (kama sikosei) ilipata takribani 27% ya kura za urais(Haijawahi kutokea tena)! Naizungumzia NCCR iliyokuwa kabla Mrema hajavumbua staili ya kukimbilia uvunguni mwa meza kukimbia kichapo!
Je, CHADEMA hii iliyonawiri maradufu baada ya kumtangaza Dr. Slaa kuwa mgombea urais imefikia hadhi ya NCCR ile niliyoizungumzia hapo juu?! Je, atavunja rekodi ya 27% (Binafsi sitaki politics, nazungumzia facts kwamba Urais hatapata) aliyokuwa ameipata Mheshimiwa Mrema?! Je, CHADEMA ina chochote cha kujifunza toka kwenye NCCR ile ambayo gari ya mgombea wake wa urais ilikuwa inasukumwa na mashabiki kila anapopita? Je, Marando ataishia kuwa mpiga debe tu kwenye chama chake kipya au atatumia uzoefu wake wa makosa ambayo waliyafanya ndani ya NCCR DUME?!
 
Naizungumzia NCCR ile iliyokuja kuibuka baada ya sakata la Mrema na Chavda! Naizungumzia NCCR iliyokuwa imemtunuku Mrema uenyekiti wa chama hicho mara baada ya kuihama CCM kwa mbwembwe(haijapata kutokea)! Naizungumzia NCCR ile ambayo Katibu Mkuu wake alikuwa Mabere Marando yule na sio huyu! Naizungumzia NCCR iliyokuwa na ma-striker hatari kama Dr. Masumbuko Lamwai ambae aliwasumbua CCM kuanzia Ubungo na kuja kuwachinjia Temeke! Naizungumzia NCCR iliyomsimamisha Mrema kama mgombea urais 1995 na kumtoa makamasi Mkapa licha kupita kupigiwa kampeni na Baba wa Taifa nchi nzima! NCCR ambayo (kama sikosei) ilipata takribani 27% ya kura za urais(Haijawahi kutokea tena)! Naizungumzia NCCR iliyokuwa kabla Mrema hajavumbua staili ya kukimbilia uvunguni mwa meza kukimbia kichapo!
Je, CHADEMA hii iliyonawiri maradufu baada ya kumtangaza Dr. Slaa kuwa mgombea urais imefikia hadhi ya NCCR ile niliyoizungumzia hapo juu?! Je, atavunja rekodi ya 27% (Binafsi sitaki politics, nazungumzia facts kwamba Urais hatapata) aliyokuwa ameipata Mheshimiwa Mrema?! Je, CHADEMA ina chochote cha kujifunza toka kwenye NCCR ile ambayo gari ya mgombea wake wa urais ilikuwa inasukumwa na mashabiki kila anapopita? Je, Marando ataishia kuwa mpiga debe tu kwenye chama chake kipya au atatumia uzoefu wake wa makosa ambayo waliyafanya ndani ya NCCR DUME?!

Huo ujasiri umeupata wapi, na unaposema unazungumzia facts ni za kisayansi au ni za kijiweni? Mapambano ya CHADEMA hayajanza leo wala jana, DR Slaa alikuwa anafahamika hata kabla hajachaguliwa kugombea hiyo nafasi. Na ni vema ukatambua kwamba Kushindwa kama unavyohisi halitakuwa PIGO kwa chadema tu bali ni kwa watanzania wote. Chamsingi ni wewe kuchukua hatua kwa kuwahamasisha Ndugu jamaa na marafiki wapige kura na sio kutabiri kushindwa vita kabla ya mapambano.
 
Nccr ya 1995 mbona ni cha mtoto!! Huwezi kuilinganisha na Chadema. Vinginevo wewe huko makini katika uchambuzi. Nccr ya '95 ilivuma sana lakini haikuwa na watu makini zaidi ya ushabiki. Isitoshe nccr ilipunguzwa nguvu na uwepo na kampeni za baba wa Taifa - Mwalimu Nyerere. Nina uhakika bila Mwalimu NCCR ingechukua nchi. Lakini yule mzee aliisadia sana Ccm kwenye kampeni na ndo mana nccr ya Mrema na Mrema mwenyewe wakaanguka. Leo hii Chadema ina watu makini, wenye uwezo na uadilifu. Naamini watavunja rekodi kama si kukamata urais kabisa. Mi sina wasiwasi na uwezo wao; na imani ya wananchi kwao. Kama huamini subiri uone!
 
Huo ujasiri umeupata wapi, na unaposema unazungumzia facts ni za kisayansi au ni za kijiweni? Mapambano ya CHADEMA hayajanza leo wala jana, DR Slaa alikuwa anafahamika hata kabla hajachaguliwa kugombea hiyo nafasi. Na ni vema ukatambua kwamba Kushindwa kama unavyohisi halitakuwa PIGO kwa chadema tu bali ni kwa watanzania wote. Chamsingi ni wewe kuchukua hatua kwa kuwahamasisha Ndugu jamaa na marafiki wapige kura na sio kutabiri kushindwa vita kabla ya mapambano.

UNAJUA NINI MKUU, kuna wakati fulani na mimi nilikuwa nacheza bahati nasibu iliyokuwa inaendeshwa na TBC1 ya kutabiri timu gani (English Premier League) ingeshinda kwenye mpambano husika! Nikagundua kila inapocheza Arsenal, nilikuwa natabiri itashinda! Arsenal ni chama langu kwahiyo ilikuwa ngumu sana kwangu kuitabiria mabaya! Hilo ni ktk soka, na hili la uchaguzi namshukuru mungu sina chama chochote hivyo sisukumwi na ushabiki. Sina shaka kwamba Dk. Slaa ni good candidate, may be kuliko hata JK but CCM ni better kuliko CHADEMA kutokana na network iliyonayo pamoja na raslimali watu ya kutosha waliyonayo. Wa-TZ mara nyingi wanachagua chama kuliko mtu na ndio hapo ninapopata jeuri ya kuamini kwamba lazima JK atashinda tena si kwa chini ya 70% ya kura zote. Naweza kushawishi walio karibu nami wachague wabunge wa CHADEMA lakini siwezi kuthubutu kuwashawishi wachague rais wa CHADEMA kv najuwa bado hawana human resources ya kutosha kuweza kuongoza nchi yenye matatizo kama hii!
 
UNAJUA NINI MKUU, kuna wakati fulani na mimi nilikuwa nacheza bahati nasibu iliyokuwa inaendeshwa na TBC1 ya kutabiri timu gani (English Premier League) ingeshinda kwenye mpambano husika! Nikagundua kila inapocheza Arsenal, nilikuwa natabiri itashinda! Arsenal ni chama langu kwahiyo ilikuwa ngumu sana kwangu kuitabiria mabaya! Hilo ni ktk soka, na hili la uchaguzi namshukuru mungu sina chama chochote hivyo sisukumwi na ushabiki. Sina shaka kwamba Dk. Slaa ni good candidate, may be kuliko hata JK but CCM ni better kuliko CHADEMA kutokana na network iliyonayo pamoja na raslimali watu ya kutosha waliyonayo. Wa-TZ mara nyingi wanachagua chama kuliko mtu na ndio hapo ninapopata jeuri ya kuamini kwamba lazima JK atashinda tena si kwa chini ya 70% ya kura zote. Naweza kushawishi walio karibu nami wachague wabunge wa CHADEMA lakini siwezi kuthubutu kuwashawishi wachague rais wa CHADEMA kv najuwa bado hawana human resources ya kutosha kuweza kuongoza nchi yenye matatizo kama hii!

Mazee,

I won't go so far as saying kwamba nina "facts" kuhusu kushindwa au kushinda kwa CHADEMA kwa mfano ( you cannot know for sure the outcome of future events, then you cannot claim to know for a fact the outcome of the election). Lakini kama unaongelea kwamba facts zilizopo established, historia na mambo mengine zinaonyesha kwamba CHADEMA atashindwa, na tunachoangalia ni kama atafikisha asilimia fulani ya kura, nitakuelewa.

Then again if you want to be ultra realistic, all the projections in the world cannot give you a true picture.

Katika uchaguzi wa urais wa Marekani wa mwaka 1948, gazeti la "Chicago Daily Tribune" kwa kutumia projections za polls liliandika "Dewey Defeats Truman" katika uchaguzi ambao Truman alimshinda Dewey. The moral of the story is, let us wait until the election is over, there is no substitute.

1948_DeweyDefeatsTruman56976.jpg
 
Back
Top Bottom