CHADEMA: Heche bado yupo nchini. Taarifa ya idara ya Uhamiaji inapotosha umma

CHADEMA: Heche bado yupo nchini. Taarifa ya idara ya Uhamiaji inapotosha umma

Its Tesha

Senior Member
Joined
Oct 6, 2025
Posts
168
Reaction score
604
Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA kitazungumza na waandishi wa habari saa nane kamili mchana.

Pia Soma >> CHADEMA: Gari la Makamu Mwenyekiti limeshambuliwa kwa risasi za moto Oktoba 18
1760868563609.png

View: https://www.youtube.com/watch?v=ZtFOeA1qkhk

Updates

Akizungumza na waandishi wa habari mkurugenzi wa mawasiliano CHADEMA, Brenda Rupia amesema kuwa Taarifa iliyotolewa na idara ya uhamiaji kuwa John Heche amevunja sheria kwa kwenda nje ya nchi bila kufuata utaratibu si ya kweli na inapotosha kwani Heche bado yupo nchini.

Amesema kuwa taarifa hiyo iliyotolewa na Uhamiaji ni sababu ya kutaka kumuweka Heche kizuizini hadi tarehe 29 Oktoba itakapopita, hivyo taarifa hiyo ni ya kupika.

Amefafanua kuwa chama chao hakitaweza kuhudhuria mazisihi ya Raila Odinga kwa sababu serikali ya CCM imewazuia kuvuka mpaka wa Tanzania na Kenya.

Brenda amegusia pia kuwa toka Passport yake pamoja na ya Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho, Amani Golugwa hazijarudishwa toka zilipochukuliwa kwa nyakati tofauti walipotaka kusafiri miezi michache iliyopita. Wameitaka serikali iwarudishie passport zao.

Ameeleza kuwa siku ya oktoba 18, 2025 gari la mwenyekiti wa chama hicho John Heche lilishambuliwa kwa risasi za moto na kupasuliwa matairi kisha kuvutwa hadi polisi ambapo wanamshikilia na dereva na wamekataa kumpa dhamana.
 
Wakamatwe haraka wanataka kufanya uhaini🐼
 
Maelekezo Maalum kuhusu tarehe 29 Oktoba.

Siku hiyo kazi ni rahisi sana

Viongozi wa CCM tunaishi nao mitaani; Nyumba zao zipo mitaani kwetu, mali zao zipo mitaani kwetu.

Ofisi za CCM zipo mitaani kwetu. Ofisi za Umma nazo zipo mitaani kwetu

VItuo vya kupigia kura vipo mitaani kwetu

Mawaziri, Wabunge na Madiwani tunaishi nao mitaani kwetu, familia zao na ndugu zao tunaishi nao mitaani kwetu. Machawa na mali zao tunaishi nao mitaani kwetu.

Ndugu watanzania, mafuta ya taa, petroli na viberiti havijawahi kuwa adimu.

Tukafanye kazi iliyotukuka hiyo Oktoba 29 hadi hawa Mafisadi watuheshimu na wakome kutuchezea na kutuua.

Share na mwenzako
 
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa CHADEMA Brenda Rupia amethibitisha kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho John Heche yupo nchini na hajuvuka kwenda nje ya Tanzania kama ilivyoripotiwa na Idara ya uhamiaji, ikumbukwe kuwa Uhamiaji waliripoti kuwa Mwenyekiti wa chama hicho amevuka kwenda nchini Kenya bila kufuata taratibu.
 
Hakuna jambo linalo wasumbua sana kuliko kutojuwa Makamu Mwenyekiti alipo sasa hivi; wakati tukielekea Oktoba 29.
Hii ni habari mbaya sana kwao.
 
Msemaji wa uhamiaji hana akili. Sijui ameajiriwa kutumia vigezo gani
 
Back
Top Bottom