CHADEMA, fafanueni tena Kagoda

Plato

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
420
94
Hoja ya msemakweli ina agenda ya siri.wakati ambapo inatolewa,wakati wote alikuwa wapi? Chombo iliporipotiwa,kujiita chadema,ni kwa malengo maalum.ili ionekane sasa kuwa tuhuma zinahusiana na chadema,lakini pia mwana chadema ameitenga kagoda na ccm.ametaja majina ya watu na makusudi kuyatenga na ccm.
Hii ieleweke anawashambulia wabaya wa mengi pekee kwa upande mmoja,na anafanya propaganda za ccm hapohapo.ndiyo maana ya yeye kujiita chadema,na kuwataja kina rostamu na manji kama watu binafsi akiwatenga na ccm kama msekwa na malechela wanavyotaka iwe.
Gazeti la uhuru leo limechekelea sana hoja hiyo
kuna conection na uchaguzi wa igunga ili ccm iseme chama siyo fisadi ila watu binafsi na ushahidi mpya ni huu wa mwanachadema.watu watakuwa bado wanakumbuka hii issue.
Sanze aliyekuwa anasifiwa kutoa andiko kuunganisha mkapa na kikwete ,rostamu na ccm amebezwa.
Msiseme hakuna jipya.lipo.anataka ushahidi wa siku zote unaounganisha ccm na kagoda uonekane feki.
Leo anajifanya anaenda kwa dpp.kwa kuwa ni mpango wa ccm dpp atafungua kesi jumatatu na mahakama itazuia suala la kagoda kujadiliwa igunga.
Nani bado anashangilia mbwembwe za huyu mnafiki? CHADEMA msishangilie ujinga huu wa CCM na msemakweli.toeni msisitizo wa uhusika wa ccm kwa vyombo vya habari mapema kabla hamjapigwa bao tena na ccm.
Msemakweli naye fisadi hatari
 
Mkuu naona una hoja. Hili ni suala la kutafakari kwa umakini. Hata mimi nilisema ya kuwa watanzania wengi tunaamini/tuliaminishwa kwamba Rostam alikwapua pesa za EPA kwenda kuisaidia CCM kwenye uchaguzi wa 2005. Lakini sasa huu ufunuo wa Msemakweli unasema hapana si hivyo hawa ni Rostam na Yusuph Manji CCM haimo!! Na kugundua tu kwamba huyo Rostam yumo inabidi uangalie kwa darubini kali kwa kuwa wanaotajwa ni Kato na Tabu!! Vyombo vya habari vya Mengi pia vimeshangilia habari hizi!!
 
Hapa kuna usanii mkubwa ambao wananchi hawaujui nadhani wanatumiwa na wanasiasa!
Mnaambiwa saizi CCM haimo kwa hiyo CCM ni wasafi walikuwa wanasingiziwa tu?
 
Huu ni mpango wa siri kweli wa kuitenganisha ccm na kagoda kama alivyosema Plato. Bwana Msemakweli inaonekana anajua mengi kuhusu CCM na ndo maana anaitetea na ninamnukuu kwenye barua yake kwa DDP" Watu hawa wamekuwa wakieneza uvumi kwamba fedha zillibiwa na kutumika kwa madhumuni ya kampeni ya CCM mwaka 2005 jambo ambalo si kweli. Lengo wa uongo huu ni kukishawishi chama tawala kutumia vyombo vya dola kunyamazizsha swala hili kwa kuhofia kwamba bila kufanya hivyo chama kitaumbuka.Ukweli ni kwamba mnamo tarehe 30 December 2005 na 2 January 2006 fedha hizo zilikuwa hazijatumika na zikahamishwa kutoka akaunti ya Kagoda Agriculture Limited kwenda kwenye kampuni ya Quality Finance Corporation Ltd na kutoka hapo zikaenda nje ya nchi kupitia Bureau dechange"Anachotaka kutulazimisha tuamini1. CCM haikuhusika na Kagoda na wala hela za kagoda hazina baraka za mkuu yeyote wa SerikaliAnachoshindwa kuikwamua CCM kwenye kashifa hii1. CCM imekubali kushawishiwa na kutochukua hatua kwa muda wote huo tangu 2005 mpaka leo miaka 6 kwa wahusika wa kagoda - Kwa hiyo mkono wa kagoda ni mrefu serikalini kuliko hata CCM yenyewe.2. Kwa nini chama kiogope kuumbuka kwa mambo ambayo hakikijua mwanzo wake na mwisho wake?3. Uzembe wa serikali ya CCM kushindwa kuthibiti taasisi za fedha kama bureau dechane.4. Bila kujali kama hela zilitumiwa na CCM kwa ajili ya uchaguzi au la lazima wizi wowote uchukuliwe hatua. Kushindwa kufanya ni kukumbatia.5. Pinda Waziri mkuu aliwahi kusema ni heri kufa kuliko kufuatilia swala la Kagoda; Je ni hatari kuifuatilia kagoda (John Kato na Baruti Goda)Hata CCM ifanyeje si safi hata kidogo katika kulinda pesa na rasirimali za taifa hili- Kagoda hatuwezi kuwafualitia- Wanyama waliotoroshwa serikali haijiu walipo- Wamiliki wa Dowans serikali haikuwajua- N.k kwa nini watake kujisafisha kwa bei rahisi kwa watanzania?
 
Siasa ni mchezo mchafu. Wananchi tusipofikiri kwa makini, tunaweza tukamakaribisha mwiz ndani ya nyumba kwa kuhisi ni mtetezi wetu. Tuwe makini.
 
Huu ni mpango wa siri kweli wa kuitenganisha ccm na kagoda kama alivyosema Plato. Bwana Msemakweli inaonekana anajua mengi kuhusu CCM na ndo maana anaitetea na ninamnukuu kwenye barua yake kwa DDP" Watu hawa wamekuwa wakieneza uvumi kwamba fedha zillibiwa na kutumika kwa madhumuni ya kampeni ya CCM mwaka 2005 jambo ambalo si kweli. Lengo wa uongo huu ni kukishawishi chama tawala kutumia vyombo vya dola kunyamazizsha swala hili kwa kuhofia kwamba bila kufanya hivyo chama kitaumbuka.Ukweli ni kwamba mnamo tarehe 30 December 2005 na 2 January 2006 fedha hizo zilikuwa hazijatumika na zikahamishwa kutoka akaunti ya Kagoda Agriculture Limited kwenda kwenye kampuni ya Quality Finance Corporation Ltd na kutoka hapo zikaenda nje ya nchi kupitia Bureau dechange"Anachotaka kutulazimisha tuamini1. CCM haikuhusika na Kagoda na wala hela za kagoda hazina baraka za mkuu yeyote wa SerikaliAnachoshindwa kuikwamua CCM kwenye kashifa hii1. CCM imekubali kushawishiwa na kutochukua hatua kwa muda wote huo tangu 2005 mpaka leo miaka 6 kwa wahusika wa kagoda - Kwa hiyo mkono wa kagoda ni mrefu serikalini kuliko hata CCM yenyewe.2. Kwa nini chama kiogope kuumbuka kwa mambo ambayo hakikijua mwanzo wake na mwisho wake?3. Uzembe wa serikali ya CCM kushindwa kuthibiti taasisi za fedha kama bureau dechane.4. Bila kujali kama hela zilitumiwa na CCM kwa ajili ya uchaguzi au la lazima wizi wowote uchukuliwe hatua. Kushindwa kufanya ni kukumbatia.5. Pinda Waziri mkuu aliwahi kusema ni heri kufa kuliko kufuatilia swala la Kagoda; Je ni hatari kuifuatilia kagoda (John Kato na Baruti Goda)Hata CCM ifanyeje si safi hata kidogo katika kulinda pesa na rasirimali za taifa hili- Kagoda hatuwezi kuwafualitia- Wanyama waliotoroshwa serikali haijiu walipo- Wamiliki wa Dowans serikali haikuwajua- N.k kwa nini watake kujisafisha kwa bei rahisi kwa watanzania?

Nakubaliana nawe kabisa mkuu. Ila hapo kwenye wekundu haikuwa Deep Green au meremeta kweli?
 
Plato asante sana kwa uchambuzi wako mdogo na wa kina kizito, Huyu msemakweli anajaribu kumtenganisha kikwete na ccm nzima kutoka kwenye lile sakata za rasilimali za umma, si chadema tu wawe makini na huyu jamaa hata sisi wananchi tumuogope kama ukoma
 
Hii nchi inaitaji mapinduzi ya mtutu na kifikra sababu ccm ni janga la kitaifa au ni laana inayotuandama kwasasa kwahiyo hii ni vita ya kila mzalendo. Na ndio maana vitani anapelekwa kila mtu so tusiwaachie CDM peke yao. Tuache maneno tuamue moja tu waondoke, bora tuanze upya. CCM wanauza madini, wanakwapua pesa (EPA), wanaiba na kuuza nyara za serikali (msekwa), wanauza ardhi na kuwafukuza wazawa kwa kisingizio cha uwekezaji, sasa tunasubiri nini?
 
Hapa JF watu wamekua wanalukia hoja haraka sana hasa wafuasi wa Chadema! Mnakumbuka Askofu Mhogolo wa Kanisa la Anglikan Dodoma alishauri Dr Slaa asitembee na Ushahidi apeleke Kwa DPP lakini mlimtukana sana yule Askofu! Leo Msemakweli anapeleka Ushahidi Kwa DPP mnaanza kuona ni mchezo wa CCM na kwa akili zenu Chadema mnaona kama Msemakweli amewapola hoja yenu! Yeye ana ushahidi basi kumbe Dr Slaa hakuwa na Ushahidi zilikua mbwembwe tu! Chadema niwashauri kwa hili msikasilike bali tushukuru lengo la kupata ukweli wa Kagoda sasa utakua wazi! Viva Msemakweli endelea we need actions na sio ngojera za akina Dr Slaa(Phd)
 
Umefika wakati sasa tupunguze longolongo na porojo kama za akina Dr Slaa kuhubiri mambo bila kuwasilisha ushahidi! Nampongeza sana Msemakweli kwa kuonesha kitendo cha kishujaa!
 
Mkapa alikuwa na role gani katika mipango yote ya Kagoda? Mbona amewaambia marafiki zake kuwa fedha za EPA zilitumika kwa ajili ya uchaguzi wa CCM?
 
Hoja ya msemakweli ina agenda ya siri.wakati ambapo inatolewa,wakati wote alikuwa wapi? Chombo iliporipotiwa,kujiita chadema,ni kwa malengo maalum.ili ionekane sasa kuwa tuhuma zinahusiana na chadema,lakini pia mwana chadema ameitenga kagoda na ccm.ametaja majina ya watu na makusudi kuyatenga na ccm.
Hii ieleweke anawashambulia wabaya wa mengi pekee kwa upande mmoja,na anafanya propaganda za ccm hapohapo.ndiyo maana ya yeye kujiita chadema,na kuwataja kina rostamu na manji kama watu binafsi akiwatenga na ccm kama msekwa na malechela wanavyotaka iwe.
Gazeti la uhuru leo limechekelea sana hoja hiyo
kuna conection na uchaguzi wa igunga ili ccm iseme chama siyo fisadi ila watu binafsi na ushahidi mpya ni huu wa mwanachadema.watu watakuwa bado wanakumbuka hii issue.
Sanze aliyekuwa anasifiwa kutoa andiko kuunganisha mkapa na kikwete ,rostamu na ccm amebezwa.
Msiseme hakuna jipya.lipo.anataka ushahidi wa siku zote unaounganisha ccm na kagoda uonekane feki.
Leo anajifanya anaenda kwa dpp.kwa kuwa ni mpango wa ccm dpp atafungua kesi jumatatu na mahakama itazuia suala la kagoda kujadiliwa igunga.
Nani bado anashangilia mbwembwe za huyu mnafiki? CHADEMA msishangilie ujinga huu wa CCM na msemakweli.toeni msisitizo wa uhusika wa ccm kwa vyombo vya habari mapema kabla hamjapigwa bao tena na ccm.
Msemakweli naye fisadi hatari



wanaasiasa vigeugeuu x2
 
Binafsi nimeanza kuhisi watawala wanajaribu kutuletea Mtikila mwingine baada ya yule wa kwanza kupoteza mvuto. Ngoja tuone kifuatacho.
 
Sina shaka na Msemakweli, Kwani kaeleza wakili Sanze wa Malegesi Law Chambers alivyo ambiwa na Rost tamu kuwa hizi ni fedha za magamba kwa ajili ya uchaguzi. MAGAMBA hawachomoki kwenye hili na Mkapa
 
.Mnawatenganishaje rostam, manji goda na kato na ccm yao wasomi wa bongo kweli bure kabisa, mlitaka cheki iwe imeandikwa ccm ndo muamini kuwa kagoda iliunwa na ccm kwa malengo mahsusi.Au hajui kuwa hata redio uhuru ni ya ccm lakini ukienda kisheria redio uhuru si mali ya ccm ila inamilikiwa na makada wa ccm tu?
 
pesa zilikuwa hazijatumika hadi 2006 January. Ni sawa. Kwani hawa watu wasingeweza kutoa hela kwingine then wakafidia na hizo za kukwapua baadae? Kwangu mimi binafsi naona kama hiyo siyo hoja ya kuwatoa hatiani magamba. Itafutwe nyingine yenye nguvu zaidi. Au jamaa ameamua kuwatoa ili magamba isimuadabishe. Yote haya yanawezekana. Maoni yangu.
 
Back
Top Bottom