KUTOKANA vurugu zilizotokea juzi mjini hapa kati ya wafuasi wa CHADEMA na wale wa CCM, uongozi wa CHADEMA Wilaya ya Dodoma umepanga kumburuta mahakamani Mbunge wa Tabora mjini, Ismail Aden Rage.
Habari zilizopatikana jana na kuthibitishwa na Katibu wa CHADEMA wilaya hiyo, Jella Mambo, wafuasi wawili wa CHADEMA wamefungua jalada la kesi hiyo na huenda leo akafikishwa mahakamani.
Mambo alisema kuwa wafuasi hao waliamua kumfungulia kesi mbunge huyo kutokana kuhusika moja kwa moja kuwapiga pale walipokuwa wamekamatwa na wakereketwa wa CCM.
Mbali na Rage, mwingine atakayehusishwa ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma Mjini, Shaaban Bwanga.
Waliofungua jalada hilo ni Idd Kizota ambaye anawalalamikia Bwanga na Rage kwa kumpiga ilihali Anord Swai akimlalamikia Rage kuwa ndiye aliyempiga.
SOURCE: GAZETI LA MWANAINCHI LEO
MY take
Rage anagonga vichwa vya habari kwa mambo yasiyo na maadili kabisa kama kiongozi, sasa vijana toka jimbo la Tabora mjini wataiga nini toka kwa RAGE? au wanasimba wanajifunza nini toka kwa RAGE. Hivi huyu ni Rage ni nani?
Wapiga kura wa Tabora mjini ninawaamini, na wana simba sport club ninawamini.
Habari zilizopatikana jana na kuthibitishwa na Katibu wa CHADEMA wilaya hiyo, Jella Mambo, wafuasi wawili wa CHADEMA wamefungua jalada la kesi hiyo na huenda leo akafikishwa mahakamani.
Mambo alisema kuwa wafuasi hao waliamua kumfungulia kesi mbunge huyo kutokana kuhusika moja kwa moja kuwapiga pale walipokuwa wamekamatwa na wakereketwa wa CCM.
Mbali na Rage, mwingine atakayehusishwa ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma Mjini, Shaaban Bwanga.
Waliofungua jalada hilo ni Idd Kizota ambaye anawalalamikia Bwanga na Rage kwa kumpiga ilihali Anord Swai akimlalamikia Rage kuwa ndiye aliyempiga.
SOURCE: GAZETI LA MWANAINCHI LEO
MY take
Rage anagonga vichwa vya habari kwa mambo yasiyo na maadili kabisa kama kiongozi, sasa vijana toka jimbo la Tabora mjini wataiga nini toka kwa RAGE? au wanasimba wanajifunza nini toka kwa RAGE. Hivi huyu ni Rage ni nani?
Wapiga kura wa Tabora mjini ninawaamini, na wana simba sport club ninawamini.