CHADEMA, CCM wakunjana ziara ya Makalla na John Mnyika

PISTO LERO

JF-Expert Member
Mar 8, 2011
2,819
1,454
Dar es Salaam. Ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla jana iliingia dosari baada ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge na Diwani wa Kata ya Kimara, Paschal Manota (Chadema), kurushiana matusi mbele ya wananchi na nusura wakunjane mashati.


Tukio hilo lilitokea jana wakati wa mkutano wa wananchi wa Kata ya Saranga, Kimara uliofanyika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Mavurunza ikiwa ni siku ya pili ya ziara ya Makalla katika ukaguzi wa miradi maji ya Dawasco.

Vurugu hizo zilitokea baada ya Makalla kuagiza polisi kuwakamata wafuasi wa Chadema kwa madai kuwa walitaka kuvuruga mkutano huo. Baada ya Makalla kutoa agizo hilo, Diwani Manota na Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika walisimama na kupinga uamuzi huo na walirushiana maneno na Mwenyekiti Madenge aliyesema wawili hao waache upumbavu.


"Unatetea nini? Acha upumbavu... Hatuwezi kuendesha mkutano na watu wanaofanya vurugu," alitusi Madenge huku Manota akiwa na jazba kabla ya viongozi wengine wa kisiasa kuwatuliza.

Hata hivyo, kabla ya Makala kuzungumza, Mnyika aliyekuwa ameongozana naye katika ziara hiyo alikuwa na wakati mgumu wa kuzungumza kutokana na zomeazomea kutoka kwa wafuasi wa CCM.

Makalla alisema kosa kubwa lililosababisha kutokea kwa vurugu hizo ni maandalizi mabovu ya wafuasi wa vyama vyote.

"Wafuasi walikuwa na itikadi zao zaidi kuliko kuja kusikiliza hoja za serikali kupitia ziara. Pia labda waliwakosa uvumilivu kutokana na ahadi ya maji kuwapo kwa muda mrefu, lakini kuvurugana wanasiasa ni kukosa uvumilivu," alisema.


Kwa upande wake, Mnyika alipendekeza ziara zote za kiserikali zisiwe na uhusiano na vyama vya kisiasa.

"Kama ingekuwa ni mambo ya kuzungumzia ilani ya chama, tangu mwaka 2005/10 ahadi ya maji ya asilimia 90 kwa Jiji la Dar es Salaam haijatekelezwa," alisema Mnyika
.

Chanzo: Mwananchi

attachment.php

Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan wa CCM (KULIA), akiamulia ugomvi wa Diwani wa Kimara, Pascal Manota wa Chadema (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge waliotaka kuzichapa ulipotokea mzozo katika mkutano wa hadhara wa Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla katika Uwanja wa Shule ya Mavurunza, Kata ya Salanga, Jimbo la Ubungo,
attachment.php

Wafuasi wa CCM na Chadema wakitaka kuzipiga kavu kavu baada ya kutokea mzozo ambapo wanaCCM walikuwa wakimzomea Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Mhe John Mnyika akihutubia na WanaChadema wakimzomea Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akihutubia katika mkutano huo.
attachment.php

Naibu Waziri wa Maji, Mhe Amos Makalla (kushoto) na Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Mhe John Mnyika (Chadema), wakitofautiana jukwaani wakati Makalla akiamuru polisi kuwatoa wafuasi wa Chadema waliokuwa wakimzomea wakati akileleza Utakelezaji wa Ilani ya CCM JUU YA MAJI, HUKU mNYIKA AKITAKA WAENDEE KUZOMEA AKIDAI KWAMBA WAZIRI HAKUFANYA HAKI KWANI YEYE ALIPOKUWA AKIZOMEWA NA WANA CCM HAKUWACHUKULIA HATUA KAMA HIYO KATIKA MKUTANO WA HADHARA ULIOFANYIKA KATIKA UWANJA WA SHULE YA MAVURUNZA, KATA YA SALANGA.
attachment.php
 
Ila ni aibu sana hivi hayo maji anayopigia kelele mnyika ni ya wana chadema?ama kweli vichaa nchi hii ni wengi ila majalala ni machache.hapo sasa anaye hujumiwa ni mnyika au wanajihujumu wenyewe?ndugu zangu tukumbuke kuwa siasa isiyo kuletea maendeleo haikufai hata kidogo.
 
Maccm ni wendawazimu wamekusanya wahuni ili kufanya fujo kwenye mikutano hiyo kwasababu hawana la kuwaambia wananchi juu ya ahadi za dhaifu kwenye kampeni. Wananchi nao walivyo majuha wanawakubalia, wakiondoka tu wanaanza kulia oooooooh majiiii........

Nyambafu mnalia nini wakati mlikubali hongo ya siku moja mkisahau tatizo lenu ni la tangu dahali?

BACK TANGANYIKA
 
Kichaa ukimwambia aachane na jalala mtaelewana?!! basi ndivyo kwa CCM na maisha duni kwa kila mtanzania asie fisadi
 
Ila ni aibu sana hivi hayo maji anayopigia kelele mnyika ni ya wana chadema?ama kweli vichaa nchi hii ni wengi ila majalala ni machache.hapo sasa anaye hujumiwa ni mnyika au wanajihujumu wenyewe?ndugu zangu tukumbuke kuwa siasa isiyo kuletea maendeleo haikufai hata kidogo.

Hivi unajielewa kweli wewe kwa hiki ulichoandika? Pamoja na hujuma zenu za kijinga hamtafua dafu,wananchi kwa sasa wanawaeleweni na usanii wenu maccm a-z! Hao waliokuwa wanazomea ina maana hawazioni juhudi za Mnyika bungeni na nje ya bunge katika kushughurikia suala la maji Ubungo? Mbona sisi tupo mwanza na tunatamani kuwa na mbunge kama Mnyika ambaye juhudi zake tunaziona?
 
Kumbe ni Mwenyekiti wa ccm (w) Kinondoni ndiye aliyeanzisha lugha ya matusi. Tena jina lake ni "Madenge"!
USHAURI:
Kwakuwa Ubungo ni Kinondoni kwanini asirudi kesho palepale Mavurunza aitishe mkutano wake mkubwa wa hadhara halafu aporomoshe mitusi mwanzo mwisho? Mwenyekiti Madenge achana na ziara ya Makala na Mnyika, nawe anzisha ziara yako upite mule mule, pengine kuna wananchi wangependa kusikiliza matusi.
 
  • Thanks
Reactions: Pai
Hivi unajielewa kweli wewe kwa hiki ulichoandika? Pamoja na hujuma zenu za kijinga hamtafua dafu,wananchi kwa sasa wanawaeleweni na usanii wenu maccm a-z! Hao waliokuwa wanazomea ina maana hawazioni juhudi za Mnyika bungeni na nje ya bunge katika kushughurikia suala la maji Ubungo? Mbona sisi tupo mwanza na tunatamani kuwa na mbunge kama Mnyika ambaye juhudi zake tunaziona?
I think you have missed a point.
 
Hivi unajielewa kweli wewe kwa hiki ulichoandika? Pamoja na hujuma zenu za kijinga hamtafua dafu,wananchi kwa sasa wanawaeleweni na usanii wenu maccm a-z! Hao waliokuwa wanazomea ina maana hawazioni juhudi za Mnyika bungeni na nje ya bunge katika kushughurikia suala la maji Ubungo? Mbona sisi tupo mwanza na tunatamani kuwa na mbunge kama Mnyika ambaye juhudi zake tunaziona?

Mkuu bujash hebu msome tena huyo jamaa maana mimi ninavyoona ni kama tuko pamoja labda kama sijamwelewa Ila nakusisitiza sana Kamanda wangu msome tena.

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
Nchi iliyojaa wapumbavu!miaka 50 ya uhuru bado serikali na wanasiasa wanaongelea upatikanaji wa maji!...maji,maji...haiwezekani.TZ ni nchi inayoshangaza upande wake wa mashariki inapakana na bahari hivyo ni kutumia technolojia ya uarabuni tu ya kuondoa chumvi kwenye maji ya bahari kisha maji tele! but issue serikali ya Tz haiwezi kuwa wazo hilo.upande wa magharibi kuna ziwa victoria rukwa na tanganyika na mito kibao!sasa acha hilo serikali ya TZ haina wazo la kuvuna maji ya mvua na kuyasafirisha kwenda maeneo kame!....sasa hivi wanatambia ya kukimbia majukumu yao kwa kisingizio ya wananchi kuchangia eti maendeleo yao!.
 
kwa sasa maccm hawataki maendeleo wamebaki kujenga chama arumeru mashariki huku arusha Nasari Alitoa madawati kwaajili ya kuboresha elimu madiwani wa ccm wanakataa eti wataharibiwa kukosa kura 2015,kiikweli kwasasa maendeleo kwasa wanajenga chama chao tu chakifisadi,
 
attachment.php

Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan wa CCM (KULIA), akiamulia ugomvi wa Diwani wa Kimara, Pascal Manota wa Chadema (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge waliotaka kuzichapa ulipotokea mzozo katika mkutano wa hadhara wa Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla katika Uwanja wa Shule ya Mavurunza, Kata ya Salanga, Jimbo la Ubungo,
attachment.php

Wafuasi wa CCM na Chadema wakitaka kuzipiga kavu kavu baada ya kutokea mzozo ambapo wanaCCM walikuwa wakimzomea Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Mhe John Mnyika akihutubia na WanaChadema wakimzomea Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akihutubia katika mkutano huo.
attachment.php

Naibu Waziri wa Maji, Mhe Amos Makalla (kushoto) na Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Mhe John Mnyika (Chadema), wakitofautiana jukwaani wakati Makalla akiamuru polisi kuwatoa wafuasi wa Chadema waliokuwa wakimzomea wakati akileleza Utakelezaji wa Ilani ya CCM JUU YA MAJI, HUKU mNYIKA AKITAKA WAENDEE KUZOMEA AKIDAI KWAMBA WAZIRI HAKUFANYA HAKI KWANI YEYE ALIPOKUWA AKIZOMEWA NA WANA CCM HAKUWACHUKULIA HATUA KAMA HIYO KATIKA MKUTANO WA HADHARA ULIOFANYIKA KATIKA UWANJA WA SHULE YA MAVURUNZA, KATA YA SALANGA.
attachment.php
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1405504220.940962.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1405504220.940962.jpg
    8.3 KB · Views: 2,843
  • ImageUploadedByJamiiForums1405504264.239620.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1405504264.239620.jpg
    15.4 KB · Views: 2,837
  • ImageUploadedByJamiiForums1405504329.393525.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1405504329.393525.jpg
    9.9 KB · Views: 2,805
  • ImageUploadedByJamiiForums1405504433.746482.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1405504433.746482.jpg
    50.2 KB · Views: 2,958
Kwanza nawapa pole sana CCM maana wananchi wameshawaelewa siyo wachapakazi wao na mambo yao yale mengine poleni sana chadema tusonge mbele
 
Naibu Waziri wa Maji Amos Makala amenusurika kipigo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali ambao wamechukia baada ya ziara yake kukosa majibu ya kero ya Maji

Mkutano umeahirishwa hapa Goba baada ya fujo
..

More updates to come...
 
Back
Top Bottom