mafundisho
JF-Expert Member
- Sep 26, 2015
- 388
- 136
Asilia na Magufuli
mimi Niko na slaa
Ni kweli na dhahiri kwamba ujio wa Lowassa umeleta mpasuko mkubwa ndani ya chama cha mabadiliko. Chama kimebadilika kweli kweli..
Inasikitisha kuona chama kilichofanya kampeni ndefu zaidi ya vyama vyote, yaani miaka 7 na miezi minne leo hii kimegeuka kuwa kituko..
Leo tuangalie tabia za wanachadema ASILIA (watoto wa Mungu) na Chadema PESA (Mkapa aliwaita malofa), chini ni listi ya tabia zinazoashiria makundi haya:-
CHADEMA ASILIA:
* Hawa ni WAZALENDO na hawanunuliki hata kwa milioni 300
* Hawa ni wasomi na watu makini sana na huwezi kuwaona kwenye mikutano ya Lowassa
* Hawa wanajua CCM sio tatizo bali tatizo ni kiongozi, wakati wa Nyerere na Mwinyi hakukuwa na udokozi wa hali hii
* Hawa wanajua HAWAWEZI KUMCHAGUA MTU aliyekuwa kwenye LISTI OF SHEM.
* Hawa wanajua ndani ya CCM, Warioba, Msuya, Mwandosya, na wengine wengi sana sio mafisadi bali ni watu wachache wasiozidi kumi
* Hawa HAWAJAPOTEZA kumbukumbu, wanajua MWIZI NI MWIZI TU na hawababaishwi na MACHOZI ya MAMBA.
* Hawa wanajua maendeleo hayaletwi leo wala kesho na kwao cha muhimu ni Maendeleo bora na sio bora maendeleo
* Hawa watazienzi harakati za Zitto na Dr Slaa na kamwe hawatateteleka
* Hawa wanajua umaskini anaochukia Lowassa ni umaskini wake mwenyewe
CHADEMA PESA:
* Hawa kwa kiasi kidogo cha shilingi 1,000 mpaka 2,000 wako tayari kuvaa shati na kofia ya CCM na kushangilia sana!
* Hawa huwa hawataki kuongelea sera maana hazipandi
* wengi wao huwa wanaonekana wajanja mpaka pale wanaposema serikali imeuza twiga wote!
* Wanamchukia sana Dr Slaa na kila anachosimamia kwa sasa
* Hawa wengi HAWANA KUMBUKUMBU ya kampeni ya kuuwa ufisadi nchini au wamejitoa akili hivi majuzi
* Hawa wanamwita Lowassa MPAKWA MAFUTA!
* Hawa wanadhani CCM ni pepo badala ya chama
* Hawa wanadhani CCM ni mkapa, ridhiwani, Raisi kikwete, tibaijuka na chenge
* Hawa wanadhani watumishi wote serikalini wanatibiwa India.
* Hawa NI WATU WA MATUSI TU, hawawezi kuandika bila kuteleza na tusi
SWALI:
JE WEWE NI CHADEMA GANI??? (Kura yako ni Siri yako)
nendeni act kwa nini mnaing'ang'ania chadema?. hamieni act mkaendeleze koko nyie.
naona wenye akili wameanza kukaa chini na kufikiria hili, ila kusema ukweli na nadhani wengine wamelisema, Dr. Slaa labda alikuwa sawa au hakuwa sawa kuondoka.Muda wa Dr.Slaa kukumbukwa ni sasa.
walijiita, hawakuwa asilia kweli, wale asilia kweli walikuwa wamekaa nyumbani wanasubiri tarehe 25 Oct wafanye kweliWaliojiita chadema asili walikuwa wanatumiwa na Masaburi kuandamana mkaishia viboko na kumtaja aliyewatuma.