CHADEMA ahidini kutatua kero za Waislam

Status
Not open for further replies.
Huyo itakuwa mujahidna, anawaza kijahidina na wala haelewi kama kuna tofauti ya chama cha siasa na taasisi/jumuiya na/au vyama vya kidini. Anatkiwa aelimishwe tu.

kwa hiyo chdm hakihitaji kura za waislamu? siyo vibaya chama cha siasa kusikiliza matatizo ya makundi mbalimbali ktk jamii yakiwemo makundi ya kidini. ubaya uko wapi kwa mbowe, slaa na viongozi waandamizi kumtembelea mufti na kubadilishana nae mawazo. kuwatembelea viongozi wa kanisa katoliki, anglikana, kkkt, makanisa ya kilokole, wasabato...... mimi sioni tatizo na hili. kote ulimwenguni kura na kuungwa mkono hutafutwa kwa kuonana na makundi maalumu. kuihusisha cuf na waislamu sidhani kama ni suluhisho. jambo hilo linaendelea kuwafanya waislamu wakione cuf kama chama chao. idadi ya waislamu wanayoiunga cuf itazidi kuongezeka. siasa hufanywa kwa kumvuta mtu upande wako siyo kumkimbia na kumbeza. IJULIKANE KUWA BILA KUUNGWA MKONO NA WAISLAMU, CHDM KAMWE HAKIWEZI KUINGIA IKULU. kwa wanao juwa idadi ya waislamu hapa nchini watakubaliana na mimi. huo ni ushauri wangu wa bure.
 
Sishauri...wacha wanaoegemea huko na kuwadnganya waumini waendelee....chadema kaeni mbali na haya mambo ya kidini...kwanza kero za waislamu ndo nini? Mie ndhani unazungumzia kero za wananchi. Acha kuwaza mambo ya kusadikika.


kwa hiyo chdm hakihitaji kura za waislamu? siyo vibaya chama cha siasa kusikiliza matatizo ya makundi mbalimbali ktk jamii yakiwemo makundi ya kidini. ubaya uko wapi kwa mbowe, slaa na viongozi waandamizi kumtembelea mufti na kubadilishana nae mawazo. kuwatembelea viongozi wa kanisa katoliki, anglikana, kkkt, makanisa ya kilokole, wasabato...... mimi sioni tatizo na hili. kote ulimwenguni kura na kuungwa mkono hutafutwa kwa kuonana na makundi maalumu. kuihusisha cuf na waislamu sidhani kama ni suluhisho. jambo hilo linaendelea kuwafanya waislamu wakione cuf kama chama chao. idadi ya waislamu wanayoiunga cuf itazidi kuongezeka. siasa hufanywa kwa kumvuta mtu upande wako siyo kumkimbia na kumbeza. IJULIKANE KUWA BILA KUUNGWA MKONO NA WAISLAMU, CHDM KAMWE HAKIWEZI KUINGIA IKULU. kwa wanao juwa idadi ya waislamu hapa nchini watakubaliana na mimi. huo ni ushauri wangu wa bure.
 
serikali ya CCM imeshindwa kabisa kutatua kero mbalimbali za waislam nchini,
Kuna kelele nyingi zinapigwa kuwa chadema kina mtizamo hasi katika mambo ya waislam,
sasa maoni yangu ni kuwa chadema ahidini kutatua kero za waislam ili kuondoa fikra hizo,
na pia kuongeza wapiga kura wengi zaidi wa chama hicho.

Hakuna kero za waislam wala hakuna kero za wakristo!
Km muumini, yeye anapaswa kupata uhuru wa kuabudu kwa usalama! mengine yanatatuliwa kwa minajili ya uraia/utaifa wala si kwa minajili ya kidini! kidogo kidogo tunaanza kupotoka kudhani kero hizi za waislam na kero hizi za wakristo, mwisho wake ni udini kiti kibaya sana!
 
serikali ya CCM imeshindwa kabisa kutatua kero mbalimbali za waislam nchini,
Kuna kelele nyingi zinapigwa kuwa chadema kina mtizamo hasi katika mambo ya waislam,
sasa maoni yangu ni kuwa chadema ahidini kutatua kero za waislam ili kuondoa fikra hizo,
na pia kuongeza wapiga kura wengi zaidi wa chama hicho.
Mkuu; ningekulaumu lakini pengine huelewi.Sasa kama utakuwa huelewi; kwa kukulaumu bado tutakuwa hatujakusaidia.Pengine nadhani njia ya sawa ni kukupa somo.Naomba u zingatie mambo ya fuatayo na tumai utaelewa.

  • Tanzania ni nchi ya Kisecular.Wazo la nchi za kisecular; ni kuhakikisha kunakuwa na uongozi madhubuti katika nchi yenye watu wa itikadi tofauti tofauti, na kuhakikisha kuwa uongozi (serikali) liyo inaleta ustawi katika nchi hiyo bila ubaguzi wala upendeleo wa aina yeyote kwa tabaka lolote lile.
  • Nadharia ya kuwa na nchi ya kisecular; ndio nadharia pekee inayoweza kuunda serikali/uongozi unaoweza kusimama na kufanya kazi katika nchi yenye watu wenye itikadi tofauti tofauti.
  • Kwa kuwa serikali katika nchi za secular zinazofuata mfumo wa kidemokrasia kama Tanzania, huundwa na vyama vya siasa; basi ni lazma vyama hivyo navyo pia viwe na muundo, mfumo na mtizamo wa kisecular (yaani kuhudumia watu wote kwa usawa).Hii pia ipo kwenye sheria ya vyama vya siasa nchini.


  • Chama chochote kinachojaribu kuingia madarakani kwa kuwahadaa au kutoa ahadi za kweli kwa makundi ya dini (kwa kuwa wewe ni wa dini fulani basi utapata/hutapa kitu fulani); Chama hicho kinafanya siasa chafu, siasa mbaya kabisa na kimekosa uadilifu.Inapotokea chama cha namna hii, kinachotakiwa ni kukikemea na kukichukulia hatua.
  • Kama ilishawahi kutokea katika historia ya Tanzania; chama fulani kikawa ahidi watu wa dini fulani kitu fulani (kwa kuwa tu watu hao ni wa dini fulani), iwe kilitekezeza au hakikutekeleza; Chama hicho kilifanya kosa tena kosa baya kabisa.
  • Kosa linapofanyika; cha kufanya si kuliendeleza badala yake ni kuliepuka.Kwa sasa chama bora ni kile kitakachotoa ahadi kwa watanzania na si kwa watu wa dini fulani eti tu kwa kuwa wao wana dini fulani.
  • Wanachotakiwa kufanya chadema kwa sasa na chama kingine chochote chenye nia nzuri na nchi hii; ni kutoa ahadi kwa watanzania kwa ujumla wao na kujiepusha kabisa ushawishi wa makundi ya kiimani kama unavyotaka kufanya wewe.Hapo ndipo tutakapoweza kuwa na Tanzania tunayoitaka.
  • Elewa kwamba uadilifu ni zaidi ya chama.Uadilifu ni kumfanyia mwenzako ambacho unapenda kufanyiwa.Nchi ni zaidi ya chama kutafuta kura.Ni bora tukalinda uadilifu wetu, utu wetu na nchi yetu kwanza; halafu ndio tukafiki juu ya kura ambazo chama kitapata.
  • Natumai umenielewa Shekhe wangu.
 
REJEA RASIMU YA KATIBA MPYA UKURASA WA 2

HIVYO BASI, KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE MAALUM LA KATIBA imetungwa na SISI
WANANCHI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kupitia KURA
YA MAONI kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na kuhakikisha kuwa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia
na utawala wa sheria, kujitegemea na isiyokuwa na dini.
 
kero za waislam ni za kitoto so sio priority kwa chadema..yaani watu wanaogombea kuchinja bata sijui mara kuku wa nini hao
 
Mchungaji Peter Msingwa anaweza kweli kutatua kero za Waislam.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom