CD4 za Maisha zinaposhuka!

CD4 za Maisha zinaposhuka!

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,207
Reaction score
829,193
Wengi naamini bado mnakumbuka mada ya kinga za kiroho, haina tofauti sana na hii na haina tofauti na kinga za kimwili.... Kinga za kimwili zilizozalisha kitu kinachoitwa UKIMWI...

UKIMWI sio ugonjwa, UKIMWI sio maradhi.... Ugonjwa/magonjwa ni kiambishi cha maradhi... Tafsiri ya UKIMWI ni Upungufu wa Kinga Mwilini... Mambo ya selihai nyekundu na selihai nyeupe...
Kinga ya mwili inapopungua basi unakuwa kwenye hatari ya kuvamiwa na ugonjwa wowote ule ambao hatimaye huzaa maradhi yenye kutesa sana
Katika maisha pia tuna kinga za kiroho CD4 za kiroho.. Hizi zikiwa vizuri basi hata afya yako ya maisha itakuwa nzuri.. Utakuwa na nuru... Kila utendalo litafanikiwa.... Mabalaa kwako ni kitu cha nadra.... Mambo yako mengi yatakuwa kwenye mstari na changamoto zako zitakuwa nyepesi na zinazotatulika...!!!

Baba wee CD4 za kiroho zikishuka.... Nyota yako hugubikwa na wingu zito jeusi... Changamoto hazitakuishia, magonjwa na wewe... Wewe na magonjwa... Hakuna kitakachosimama... Hakuna utakachogusa ufanikiwe
Mambo mengi utaanza kwa mafanikio lakini hayafiki popote, usipodhulumiwa, utaibiwa.... Usipoibiwa utapoteza... Usipopoteza utaharibu.....!!!!

Kwa akili yetu ya kibinadamu kuna wajanja wachache wenye kutumia mwanya huo kuumiza wengine kwa kuwatapeli fedha na mali kwa ahadi ya kuwasaidia kusafisha nyota ama kuwarekebishia mambo yako yanyooke....

CD4 zozote ziwe za kimwili ama za kiroho zina chanzo chake, zina asili yake
. Mafarakano katika familia
. Dhuluma
. Kijicho
. Ushirikina
. Ubinafsi
. Chuki
. Roho mbaya
. Laana za ukoo
. laana za familia
. Maagano
. Viapo na mambo mengine yote yanayofanana na hayo?

Je unahisi CD4 zako za maisha zimeshuka? Jichunguze tatizo limeanzia wapi
 
umeeleza vizuri sana lakini kwa sisi wa mjini huwa junajibu hivi:-
  • hakuna kitu kama hicho mambo ya ukoo wala nini tunadanganyana kinachtusumbua ni stress zilizoletwa na utawala huu kafanya kila jambo kuwa gumu.
  • hayo unayotueleza is just imagination na upotoshaji ili watu waangaike makanisani na huenda umetumwa kwa kuwa sadaka zimepungua.
yapo mengi lakini ukweli ndio huo na ukitaka kuona angalia kwa mambo manzuri mfano kijijini kunaweza kuwa na familia iliyoanzishwa na baba mwalimu na mama mwalimu kuna uwezekano mkubwa watu hawa kuwa waalimu au tuangalie hata kwa nafasi za juu karume baba yake rais na yeye akawa rais pia hata kwa kenyata pia.
hivyo yanapotokea lazima kurudi nyuma na kuangalia kuna nini na kwa nini hili limetokea maisha tuanyoishi leo tunayatengeneza kwanza kwa binadamu wa ndani na ndipo binadamu wa nje anafanya hivyo kama ndani hakuna utulivu na kunavurugu kunalia kisasi,laana maagano ya kafara zinazodaiwa na mizimu hakuwezi kuwapatikana utulivu.
changamoto tulionayo maisha yetu yamekuwa vugu vugu unaenda kanisani ukitoka unawahi kwa mganga kisha ndo unarudi nyumbani.
zipo changamoto za usiri hata kuzaliwa kwetu mfano kunauwezekano mama kakuzaaa lakini baba uliyenaye sio baba yako mzazi na wewe umefichwa baba yako kafichwa lakini mtu wa ndani unajua kila kitu kwakweli mtu wa namna hii kufanikiwa inaweza kuwa shida kwa kuwa wakati mwingine hana kibali kwa familia husika katika ulimwengu wa roho.
mwisho wa siku ni kukataliwa na kujikataa na matokeo inaweza kuwa kufanya umalaya uliopitiliza, au chochote kinachoweza kufikia hata kuwa kichaa au kujiua.
 
CD4 zikishuka twafa
Za kiroho nini chaja
Kufa kiroho ndo nini
Kuna athari kubwa?
Matibabu yake yapi?

Bazazi
 
umeeleza vizuri sana lakini kwa sisi wa mjini huwa junajibu hivi:-
  • hakuna kitu kama hicho mambo ya ukoo wala nini tunadanganyana kinachtusumbua ni stress zilizoletwa na utawala huu kafanya kila jambo kuwa gumu.
  • hayo unayotueleza is just imagination na upotoshaji ili watu waangaike makanisani na huenda umetumwa kwa kuwa sadaka zimepungua.

yapo mengi lakini ukweli ndio huo na ukitaka kuona angalia kwa mambo manzuri mfano kijijini kunaweza kuwa na familia iliyoanzishwa na baba mwalimu na mama mwalimu kuna uwezekano mkubwa watu hawa kuwa waalimu au tuangalie hata kwa nafasi za juu karume baba yake rais na yeye akawa rais pia hata kwa kenyata pia.
hivyo yanapotokea lazima kurudi nyuma na kuangalia kuna nini na kwa nini hili limetokea maisha tuanyoishi leo tunayatengeneza kwanza kwa binadamu wa ndani na ndipo binadamu wa nje anafanya hivyo kama ndani hakuna utulivu na kunavurugu kunalia kisasi,laana maagano ya kafara zinazodaiwa na mizimu hakuwezi kuwapatikana utulivu.
changamoto tulionayo maisha yetu yamekuwa vugu vugu unaenda kanisani ukitoka unawahi kwa mganga kisha ndo unarudi nyumbani.
zipo changamoto za usiri hata kuzaliwa kwetu mfano kunauwezekano mama kakuzaaa lakini baba uliyenaye sio baba yako mzazi na wewe umefichwa baba yako kafichwa lakini mtu wa ndani unajua kila kitu kwakweli mtu wa namna hii kufanikiwa inaweza kuwa shida kwa kuwa wakati mwingine hana kibali kwa familia husika katika ulimwengu wa roho.
mwisho wa siku ni kukataliwa na kujikataa na matokeo inaweza kuwa kufanya umalaya uliopitiliza, au chochote kinachoweza kufikia hata kuwa kichaa au kujiua.
 
Back
Top Bottom