Katibu wa itikadi na Uenezi CCM amewaomba radhi watanzania wote kutokana na tatizo la ununuzi wa umeme kwa njia za kielektroniki lililo jitokeza nchini kote kwa siku tatu mfululizo,
Baada ya kupokea taarifa za tatizo hilo Shaka Hamdu Shaka alifanya ziara usiku kwa kuzunguka katika vituo vyote vilivyoelekezwa kupatikana huduma ya LUKU na kujionea kadhia walioipata watanzania walio wengi.
Leo Katika Mkutano wa Katibu Mkuu na waandishi wa habari Katika ofisi za CCM DODOMA , Shaka H Shaka alipata wasaa wa kumueleza katibu Mkuu wa CCM Ndg Daniel Chongolo kadhia yote waliyoipata watanzania na kisha kumuomba aseme neno Pindi anapoongea na waandishi wa habari, nae alisema,
"Nionye wale wenye nia ovu na Nchi yetu ambao walitaka kutuweka gizani, niipongeze Serikali kwa hatua za awali walizochukua katika kuhakikisha wananchi wanaepukana na changamoto ya manunuzi ya Umeme....."
akaongeza, wale wote watakaodhibitika kuwa walihusika na kadhia hii kwa wananchi, wachukuliwe hatua stahiki za kisheria
Kupitia sakata hilo Shaka Hamdu Shaka alimpongeza Sana Mh Waziri Mkuu wa jamuhuri ya muungano wa TanzaniaMh Kassim Majaliwa kwa kuchukua hatua za haraka sana Katika kukabiliana na tatizo hilo ndani ya muda Mfupi Sana na Kutoa maagizo ya uchunguzi wa kina juu ya tatizo hilo.
Lakini pia Ndg Shaka Hamdu Shaka alitoa pongezi za dhati kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania SAMIA SULUHU HASSAN kwa umakini wake wa kusimamia serikali na watendaji wake wote.
Leo 20/05/2021 kwa mara ya kwanza katibu Mkuu wa CCM alikuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu mustakabili mzima wa chama cha Mapinduzi na serikali yake.
SEKTETARIATE MPYA