Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
[h=3]CCM WAZINDUA KAMPENI UZINI(JANA)[/h]
Dk.Karume ndiye aliyezindua kampeni hizi
Umati wa wana CCM kwenye uzinduzi wa kampeni jimbo la Uzini jana
Kampeni sasa zimepamba moto katika jimbo la Uzini Zanzibar baada ya CCM nayo kuzindua kampeni zake jana katika viwanja vya Ghana nyuma ya CHADEMA na CUF.Kwa kulinganisha kwa macho mkutano huu wa CCM umekuwa na watu wengi kuliko ile ya CHADEMA na CUF.Midundiko ya CCM na ngoma nazo zimeanza na jana vijana wa CCM nusura wapigane a wale wa CHADEMA baada ya kupita jioni barabarani wakipiga mziki,vijana na wanawake wa chadema walijikusanya na kuanza kuwazomea CCM jambo ambalo lilizua tafrani lakini likatulia baada ya gari iliyokuwa na vijana wa CCM kuondoka eneo hilo.Baadaye CHADEMA nao wakapita wakiwa na fuso lao kubwa la matangazo wakipiga wimbo wa CCM presha inapanda na kushuka huku vijana wengi wakiwa juu ya gari hilo.Hata hivyo hakuna vurugu kubwa zilizotokea.Uzinduzi wa CCM ulihudhuriwa pia na Mh.Pius Msekwa.
Dk.Karume ndiye aliyezindua kampeni hizi
Umati wa wana CCM kwenye uzinduzi wa kampeni jimbo la Uzini jana
Kampeni sasa zimepamba moto katika jimbo la Uzini Zanzibar baada ya CCM nayo kuzindua kampeni zake jana katika viwanja vya Ghana nyuma ya CHADEMA na CUF.Kwa kulinganisha kwa macho mkutano huu wa CCM umekuwa na watu wengi kuliko ile ya CHADEMA na CUF.Midundiko ya CCM na ngoma nazo zimeanza na jana vijana wa CCM nusura wapigane a wale wa CHADEMA baada ya kupita jioni barabarani wakipiga mziki,vijana na wanawake wa chadema walijikusanya na kuanza kuwazomea CCM jambo ambalo lilizua tafrani lakini likatulia baada ya gari iliyokuwa na vijana wa CCM kuondoka eneo hilo.Baadaye CHADEMA nao wakapita wakiwa na fuso lao kubwa la matangazo wakipiga wimbo wa CCM presha inapanda na kushuka huku vijana wengi wakiwa juu ya gari hilo.Hata hivyo hakuna vurugu kubwa zilizotokea.Uzinduzi wa CCM ulihudhuriwa pia na Mh.Pius Msekwa.