Winston Mtanzania
JF-Expert Member
- Mar 27, 2014
- 340
- 117
watu kama mtoa mada huyu ni wagumu mno kuelewa. siyo kwamba Waryoba hakuzingatia maoni yenu ila alisema maoni hayo yatumike kwenye uandaaji wa katiba za nchi washirika. Rasimu ya katiba ya Waryoba ilibeba mambo ya muungano tu.
Mzimu soma rasimu hapa, utayaona hayo. Attached: RASIMU YA PILI YA KATIBA YA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA
MWAKA 2013.pdf (1.05 MB)
Hayo unayoyasema kuhusu hiyo mahakama yanayo faida gani kwa Mkristo ambaye HAIAMINI, HAIMHUSU WALA HATAHUKUMIWA na mahakama hiyo.??
Mbona yote ya kwenu, kwanini msianzishe? Mnasubiri tuwape ruhusa?
Umesema ni mfumo wa maisha, ila hayo si maisha yetu Wakristo ni yenu. Anzisheni basi mhukumiane mnakoamini. Serikali haina dini, mnataka mhimiri wake mmoja uwe na dini, mkimaliza mtulazimishe kuwachangia fedha zetu..!!! BIG NO!
Hoja ya kodi ni hoja dhaifu sana kutolewa na mtu yoyote ambae ameenda shule na kuelewa masomo yake vyema. Kwani ni wakristo peke yao ndio wanaolipa kodi. Basi sisi waislamu tunataka kodi zetu zigharamie Mahakama ya kadhi!. Sasa wewe shauri utaratibu gani utumike kuzitenganisha kodi hizo!.
Kama ni uhuni katika Mchakato Mzima wa Katiba, ulianzia katika tume ya Warioba kwa kuchakachua Maoni ya Watanzania waliowengi na hasa Waislamu kupitia Maoni ya Mtu mmoja mmoja na taasisi zao. Mimi ni mmoja wa Watanzania niliotoa maoni, miongoni mwao ni Kuanzishwa Mahakama ya Kadhi kwa Mujibu wa Katiba kama ilivyo kwa nchi za Kenya, Uganda, Afrika ya Kusini, Uingereza n.k.
Lengo ni kuzipa nguvu Mahakama hizo ili maamuzi yake yaweze kuheshimiwa na mahakama nyingine, kwa Mujibu wa mfumo mzima wa Kimahakama ulivyo.
Taasisi karibia zote za kiislamu zilitoa maoni hayo hayo pamoja na mengineyo. Tume ya warioba pia iliwaalika jumuia na taasisi hizo pale Karimjee hall, na taasisi hizo zikapeleka maoni yale yale kwa Maandishi na kwa mdomo.
Lakini kinacho onekana, Mheshimiwa Jaji warioba na kundi lake, walifanya kazi ya uwakala wa kanisa na bila woga, kutupililia mbali maoni hayo kabla ya hata kufikishwa bungueni kujadiliwa.
Sasa inashangaza sana kuyaita Maoni ya Tume ya Jaji warioba kua ni Maoni ya Watanzania.
Kwahiyo basi, walicho fanya CCM, nikuona kwamba huyu kama ameweza kuchakachua maoni ya wananchi na bado wana mshangilia, kwanini na sisi basi tushindwe.
Hivyo basi CCM chini ya MFUMO kristo amboa unaendelezwa kiujanja ujanja wanafanya hicho kinacho endelea sasa.
Tatizo ni uwelewa. Yaani hapa JF saa nyingine sijui tunajadiliana na watoto secondary hata sijui nini?. Ni shidaaa! Wapi tumewahi kusema kua tutawahukumu wakristo na wasiokua waislamu?.
Hilo likitokea ni kwa mapendekozo ya mtu binafsi au yeye na mwenza wake au familia yake. Hivyo ndivyo inavyotokea uingereaza kwa sasa. Wapo watu wasiokua waisalamu wanaopeleka mashitaka yao kwenye mahakama za kadhi kupewa hukumu na wanaridhika na kufurahishwa na hilo.
wanaotibiwa humo ni wakristo tupu?
try to think wise
Anzisheni chombo chenu cha kukusanya kodi sio TRA ambayo nayo inalipwa kwa kodi za watanzania wote.Mkishakianzisha na kutueleza kwamba mtaweza kuigharimia njooni tujadiliane jinsi ya kuweka mahakama za Kidini kwenye Katiba bila kuadhiri wapagani.Hatuwezi kuweka kwa kigezo kwamba Uganda ipo kwani mwingine atadai Tanzania nayo pawe na waasi wa Lord Resistance Army.Sio kila kitu kinaigwa.
Sasa hao watoto wako ni akina nani? Mbona wanakuuliza maswali yanakushinda?
Unaishiwa majibu unaita watu watoto, bora watoto weledi kuliko wakubwa wazembe wa kufikiri kama wewe Mzimu
Waislam msipende ubwete mahakama ya kidini kwa nchi isiyofuata dini nisawa na kumpeleka Mbwa msikitini, mnapesa za kuweza kuanzisha na kusimamia mahakama zenu.
Hivi kweli waislamu hamna uwezo wa kufanya mambo yenu wenyewe mpaka msaidiwe na wakristo,wabudha,wahindu na wapagani?Serikali iliwasaidia kuanzisha BAKWATA lakini kila siku mnaiponda kwamba ilianzishwa na Nyerere ili kuwadhulumu waislamu.Hata Mahakama ya Kadhi ikianzishwa na serikali mtalalamika imeanzishwa na mfumo kristo.Tafadhali jiaminini na ianzisheni wenyewe msisubiri kuwezeshwa kama wale wa jinsia ya pili.
Nakushukuru sana kinyungu. Kwakeli umenielewesha kwa weledi wa hali ya juu. Naomba nikiri kua hilo ilikua mimi silijui. Hili ni jibu la kwanza lililo nitosheleza kiu yangu tangu mjadala wa Katiba Mpya Uanze.
Kama hivyo ndio sahihi, that means, uhalali wa MAHAKAMA YA KADHI upo ndani ya serekali tatu. Napenda kukiri kama kuna ushahidi wowote wa nukuu ya Maneno yako, basi sina uhalali wa Moja kwa moja kuishutumu tume ya Jaji Warioba. Kwa Maana hiyo, jinamizi letu ni CCM, na nakuahidi, they will not live to be in power ever again, starting 2015.
Naomba niwekee wapi nitaiona hiyo nukuu, nianze kuomba radhi na kuelekeza mashambulizi yangu sehemu husika.
Nakukubalia respect wa boda. Ila mtego wa Utaifa kwa waislamu ndi Mtego uliwagharimu Waislamu katika nchi hii kwa kiwango kikubwa sana. Tafadhali fuatilia historia ya WATEMI Wailio pigania uhuru, Vita vya MAJI MAJI, TANU, EAMWS, BAKWATA na Julius Kambarage kuandikwa peke yake Katika historia rasmi ya nchi hiii.
Ah mkuu sasa ninyi hao wazee wote walikuwa wapi mpaka Nyerere akaandikwa peke yake kwenye historia rasmi ya nchi hii huoni kwamba madai yako yanawalakini au kutengeneza maswali mengi.?
Karibia mara zote, Waislamu wa nchi hii wamekua wakiweka Utaifa kwanza na Uislamu Baadae. Kinyume chake kimekuwa kwa Viongozi wakirsto na wakirsto waliopewa dhamana katika nchi hii. Mara zote wameweka Ukristo kwanza na Utaifa baadae.
Unaweza kutupa mfano moja wapo kwamba wakristu walitangiliza ukristu mbele na kuacha maslahi ya taifa nyuma?
Tumekuwa tukitoa maelezo mengi sana juu ya hali hiyo katika Munakasha mbalimbali ikiwemo hapa JF. Kwa bahati mbaya sana, kuna baadhi ya Waislamu bado hawajitambui. Wao wameweka Maslahi ya Matumbo yao Kwanza kuliko hata huo utaifa wenyewe. Hivyo Basi hua wanapopata fursa ya kuwekwa kwenye decisions boards, hua ni watu wakuburuzwa tu.
Sasa hapa kama hujitukani nadhani umeamua kuwadhalilisha watu bila kujijua Hapa unatitjibitishia kwamba wale waislam waliokuwa kwenye tume ya Warioba walitanguliza matumbo yao mbele na kusahau maslahi ya uislam bila shaka ndivyo unavyomaanisha.
Kwani katika hilo Bunge la CCM linaendelea ambalo limekosa uhalali wa kisiasa, waislamu hao bado wamo. Alhamdulahi, mwanasheria mkuu wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othaman kesha shtukia dili lao, kaamua kujitoa.
Sidhani kwamba ni sababu za kidini zilizosababisha mwanasheria wa Zanzibar akajitoa bali ni kuchakachuliwa kwa maoni ya wananchi naomba usichanganye vitu hivi.
Pamoja kua temesikia katika vyanzo vya siri kua Wabunge Waislamu wanajipanga kujitoa katika bunge linalo endelea kama Mahakama ya Kadhi haitatambuliwa, kama ambavyo waliamamua katika mikutano ya mabaraza ya kanisa kua kama mahakama ya kadhi ingepitishwa na kamati ya Mheshimiwa Brigedia Hassan Ngwilizi nao wangejitoa.
Mkuu wewe ni mtu mzima kwanini uongee vitu vya kufikirika lini haya madai yako yalitajwa ama kuwekwa wazi? mbona sisi wengine hatujawahi kusikia wewe ulisikiasikia wapi mkuu?
Mimi nadhani hili jambo lazima lijadiliwe kwa kina, faida na hasara zake kwa jamii ya watanzania kabla hali haijakua mbaya.
Mkuu kwanza nikutoe wasiwasi hali haiwezi kuwa mbaya kama unavyojaribu kutisha watu hapa. kama ilikuwa ikihitajika kufika huko (kwenye hali mbaya) tungeanza kwenye bunge la Katiba lakini tunashukuru mjadara wa watu makini uliwezesha kuvuka salama salimini huku hoja zikitawala na hatimae ufumbuzi kupatikana hivyo kujaribu kudai kwamba hali yaweza kuwa mbaya kwa jambi dogo kama mahakama ya Kadhi ni kujipa presha isiyokuwa na msingi wowote.
BACK TANGANYIKA
Baadaye mtadai mjengewe madrassa simply kwa kuwa mnalipa kodi!Hoja ya kodi ni hoja dhaifu sana kutolewa na mtu yoyote ambae ameenda shule na kuelewa masomo yake vyema. Kwani ni wakristo peke yao ndio wanaolipa kodi?. Basi sisi waislamu tunataka kodi zetu zigharamie Mahakama ya kadhi!. Sasa wewe shauri utaratibu gani utumike kuzitenganisha kodi hizo!.
Hoja ya kodi ni hoja dhaifu sana kutolewa na mtu yoyote ambae ameenda shule na kuelewa masomo yake vyema. Kwani ni wakristo peke yao ndio wanaolipa kodi?. Basi sisi waislamu tunataka kodi zetu zigharamie Mahakama ya kadhi!. Sasa wewe shauri utaratibu gani utumike kuzitenganisha kodi hizo!.
Baadaye mtadai mjengewe madrassa simply kwa kuwa mnalipa kodi!
Hoja ya kodi siyo dhaifu kama unavyotaka kujiaminisha! Dini zote zimejiwekea utaratibu wa kutatua migogoro ya waumini wao! Wakrito wana mabaraza ambayo hushughulikia maswala ya ndoa na haya hufanywa kwa kujitolea kwa wazee wa makanisa! Mambo ya mirathi huachwa kwa tamaduni za wahusika na dola!
Hivyo ni busara waislam watafute namna wanavyoweza kutatua migogoro ya ndoa na mirathi ya waumini wao!
Isitoshe kwa imani yenu waislam mnahubiri kutumia fedha halali na iliyopatikana kwa njia zinazokubalika na sharia, sasa iweje mnataka kutumia fedha zilizopatikana kwa njia ya riba, kodi za pombe nk.!
Kwani ndugu zetu waislam mnaona shida gani kuanzisha hiyo mahakama yenu wenyewe. Mnachoogopa ni nini, hamna uwezo!, hamuwezi kujiongoza! kwanini mnapenda miteremko. Hilo noi suala la imani yenu zaidi, jipangeni, fanyeni jitihada mijitegemee. Tusipotezeane muda hapa.
Hoja zenu za kitoto tulisha zijibu mara nyingi. Nyie vitoto vya Sunday school sijui uwezo wenu wa kufikiri umeharibiwa kiasi gani?. Hebu jaribuni kufikiria kwa akili zenu za kawaida bila communion juice. Sijui mnachanganyiwa na nini?
Hebu edit hiyo post yangu ulio inukuu, naona umenichanganyia pilau na mlenda. Umeniongezea maneno. Sivyo hivyo ilivyo!