CCM yakanusha tuhuma za CHADEMA

CCM yakanusha tuhuma za CHADEMA

babalao 2

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
5,425
Reaction score
3,300
attachment.php


SIKU moja baada ya Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), kudai CCM inashirikiana na baadhi ya viongozi wake kukisaliti chama hicho, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amekanusha tuhuma hizo.

Nape alisema CCM haihusiki na mgogoro wowote ndani ya chama hicho, hivyo wanapaswa kumtafuta mchawi wao siyo kukilaumu chama chake. "Mchawi wanaye wenyewe ndani ya chama chao,hatuhusiki na lolote hivyo wanapaswa kujipanga na kuulizana kubaini tatizo linalowasumbua," alisema.

Aliongeza kuwa CCM haina muda wa kuhujumu chama hicho, ila wana muda wa kutekeleza ilani za chama maeneo mbalimbali nchini.
Nape alisema kutokana na hali hiyo, CCM imejipanga kuhakikisha ahadi zinatekelezwa kwa vitendo, ikiwamo maazimio yaliyotolewa kwenye mkutano mkuu wa chama hicho.Baadhi ya viongozi wa BAVICHA wanaodaiwa kushirikiana na CCM kudhooficha CHADEMA na
wengine walifukuzwa uanachama.

Miongoni mwa viongozi hao ni aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Bavicha, Juliana Shonza,Habib Mchange, Mtera Mwampamba, Gwakisa Burton na Joseph Kasambala.
 

Attachments

  • uploadfromtaptalk1357707148177.jpg
    uploadfromtaptalk1357707148177.jpg
    30.3 KB · Views: 1,648
Shibe ya Nape bana, just breaking the wind
Ccm haijui siasa na sasa wameshikwa pabaya kila wazimu wanaoujaribu kuvuruga Chadema jamaa wanawaumbua kwa kuzimilia mbali njama zao!!Tangu lini CCM ikafanya siasa bila kutisha kuhujumu upinzani kutisha watu kudharau raia wa Tz kudhalilisha watumishi wa Umma na ujinga mwingine mwingi tu?Siku za Ccm zimeisha na wananchi wanaanzisha ukombozi kupitia Chadema na Mungu wa haki aibariki chadema na kuilaani Ccm iendelee kuchakaa kila kuchao
 
Na Tyson kwenye kampeni ya NEC alisema yeye ni kiboko ya CDM, unafikiri alimaanisha nini? ndiyo hayo yanayotokea, lakini hilo lisiwatishe CDM ili mradi limegundulika mapema ni kuchukua tahadhari mapema, siasa ni mchezo mchafu na lazima ukubaliane nao hakuna urahisi kutaka kusonga mbele lazima upambane, CDM pambaneni hadi kieleweke, maana kesho wataaza na mbinu nyingie, ukumbuke hata na kashfa za Dr. Silaha na mchumba wake zilivyoendeshwa.
 
Du nilimwona huyu jamaa kwenye mkasi ndio nikaamini CCM kumejaa vilaza, wapenda sifa na wanaojali matumbo yao kwanza.
 
Ngoma ikivuma,ikavuma,ikavuma tena,vuvuu,vuvuu mwisho upasuka R.I.P CDM

Toka Burton sat shop.
 
Nape mchumia tumbo ataongea nini!

Mipango yake imeshindwa
 
bora angekaa kimya
Nape anadhani watanzania ni wajinga hawaoni yanayoendelea?
hao hao waliowatuma kuhujumu pamoja na shahidi zilizopo zitawaumbua zaidi
Heche shuka data baba waaibishe waaibike zaidi.mwaka huu wataumbuka zaidi
chama chetu mnajiabisha acheni kutaja chadema kila kukicha tekelezeni ilani zenu
walau mpate wabunge 20 mwaka 2015
 
Ulitegemea wakubali?hata ya Mwembeyanga walikanusha
 
Kwa mtu ambae ana akili timamu kuishangilia ccm ni sawa na kufuraia kupata ngoma.we beza cdm moto wake utauona tu..fichadi we
 
bora angekaa kimya
Nape anadhani watanzania ni wajinga hawaoni yanayoendelea?
hao hao waliowatuma kuhujumu pamoja na shahidi zilizopo zitawaumbua zaidi
Heche shuka data baba waaibishe waaibike zaidi.mwaka huu wataumbuka zaidi
chama chetu mnajiabisha acheni kutaja chadema kila kukicha tekelezeni ilani zenu
walau mpate wabunge 20 mwaka 2015

Nilisha sema huko nyuma kwamba ccm hasa sekretarieti ni wepesi muno kwa kwa sababu ya kukosa viongozi wachambuzi wa hoja na matatizo yanayolikabili taifa badala yake umma wa watz umeshuhudia viongozi wakubwa hasa naibu katibu mkuu, mhe. Nchemba wakipiga propaganda na siasa za uzushi dhidi ya vyama vya upinzani. Nilishangaa siku moja kwenye Startv Nchemba akilidanganya taifa kwamba vyama vya upinzani ktk nchi jirani vilivyobahatika kushinda uchaguzi na kuunda serikali eti vilifanya hivyo mara moja na vyama vya zamani kuendelea kutawala. Huyu ni kiongozi mkuu lkn hana kumbukumbu kuwa alichokiongoza kenyatta kupata uhuru kenya ni historia, chama alichokiongoza kaunda kupata uhuru zambia ni historia, uganda, malawi, rwanda, drc congo nk nk. Ccm baada ya kuona kimekosa mvuto kwa raia ss kinakimbilia kununua wanachama wa vyama vya upinzani ili kuleta mgawanyiko, vyombo vya habari ss vinaimba kila siku utekelezaji wa ilani! Yote hii ni kutapatapa kwa ili kiungwe mkono na raia lkn it is too late to catch a moving train! Chama kilichoongoza nchi zaidi ya miaka 50 kinaangaika kujitangaza kila siku kuonesha nini kimefanya! Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza. Watz wa sasa wanaona wenyewe, serikali haina sababu ya kutumia pesa za walipa kodi kwa kulipia matangazo kwenye vyombo vya habari kutafuta umaarufu uliopotea. Hii ni tz wenye vijana wa.com wasiosubili serikali iwambie imefanya nini! Wanajua wenyewe kama imefanya na kwa ubora upi! Purukushani zote zinaonesha ccm sasa inatapatapa na kweli haiponi kwa mipango hii.
 
Bila kujua ndio wanazidi kukiimarisha na kukijenga chama cha demokrasia na maendeleo na wao wakiendelea kuchochea hasira na chuki za wananchi dhidi yao kwa kushindwa kuwatatulia matatizo lukuki waliyoyaleta na kuwasababishia wananchi hawa kwa takribani miaka 51 iliyopita. kama wana muda wa kufanya uchafu katika vyama vingine wakakosa muda wakukinusuru chama chao na kuondoa matatizo waliyonayo watanzania basi watakuwa na shahada ya utaahira.
 
attachment.php

SIKU moja baada ya Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), kudai CCM inashirikiana na baadhi ya viongozi wake kukisaliti chama hicho, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amekanusha tuhuma hizo.

Nape alisema CCM haihusiki na mgogoro wowote ndani ya chama hicho, hivyo wanapaswa kumtafuta mchawi wao siyo kukilaumu chama chake. “Mchawi wanaye wenyewe ndani ya chama chao,hatuhusiki na lolote hivyo wanapaswa kujipanga na kuulizana kubaini tatizo linalowasumbua,” alisema.

Aliongeza kuwa CCM haina muda wa kuhujumu chama hicho, ila wana muda wa kutekeleza ilani za chama maeneo mbalimbali nchini.
Nape alisema kutokana na hali hiyo, CCM imejipanga kuhakikisha ahadi zinatekelezwa kwa vitendo, ikiwamo maazimio yaliyotolewa kwenye mkutano mkuu wa chama hicho.Baadhi ya viongozi wa BAVICHA wanaodaiwa kushirikiana na CCM kudhooficha CHADEMA na
wengine walifukuzwa uanachama.

Miongoni mwa viongozi hao ni aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Bavicha, Juliana Shonza,Habib Mchange, Mtera Mwampamba, Gwakisa Burton na Joseph Kasambala.
by Yericko Nyerere.
Taarifa za kuaminika toka ndani ya ccm zinasema kuwa kumeibuka sekeseke la aina yake juu ya hatima ya masalia waliofukuzwa chadema,

Hasira za wanaccm zimeibuka baada ya siri kuvuja kuwa katibu mwenezi wa ccm ndugu NAPE NNAUYE aliwaahidi masalia wa chadema kuwa ikiwa watafukuzwa hasa (Juliana Shonza), ccm itawapokea kwa sherehe kubwa na kulikuwa na makubaliano zaidi kuwa aliyekuwa Makamu mwenyekiti wa BAVICHA ndugu Juliana Shonza atapatiwa nafasi ya UONGOZI ccm!

Taarifa hii imewachefua wanaccm wengi hasa vijana, huku wakisema wao wamejipanga mstari tangu 2010 kusubiri nafasi za ungozi, hivyo hawezi kutokea mtu tu tena asiyeijua ccm akajichomeka mbele ya mstari nakupata uongozi wa chama ghafla tu,
Wameapa kuwa hilo hawakubali kuliona likitendeka, heri chama kife kuliko kudhalauliana tu!

Katika kuthibitisha kuwa upepo ndani ya ccm ni mbaya, tangu juzi tarehe 07/01/2013 mawasiliano ya Shonza na Nape yamekuwa makubwa lakini kipengele cha kupewa uongozi ndani ya ccm pindi akijiunga tu ndicho kinakuwa kizito kwa Nape kumthibitishia Shonza!

Mfano: ujume ulionaswa wa Nape kwenda kwa Shonza unasema, "Juliana tunaandaa mapokezi mazito na tutazunguka na wewe nchi nzima"

Lakini kuthibitisha kuwa Shonza aliupata ujumbe huo anajibu,

"Mkuu nipo tayari, vp lakini nafasi ya uongozi? Fanya kama tulivyokubalia nafasi yoyote ambayo itaendelea kuniweka mbele ya jamii, mimi ni mwanasiasa bwana"


Muono wangu:

Kazi iliyofanywa na Chadema ni adhimu na murua, hakuna chama cha upinzani barani afrika kilichoweza kuchukua maamuzi magumu kama haya tena katika kipindi cha hatari kama hiki cha mwaka mmoja tu kabla ya uchaguzi,

Matokeo ya maamuzi haya yameisambaratisha ccm na sasa wanaweweseka tu kutafuta mbinu mbadala za kudhoofisha upinzani!i

Mimi kama mwanachadema ninaamini waliofukuzwa ni vidagaa tu, lakini mapapa wa uasi wapo ndani ya kamati kuu ya Chadema,

Naiomba ifanye maamuzi magumu zaidi ili kuizika kabisa ccm na vibaraka wao waliokuwa ndani ya Chadema!

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Chadema na wanyoofu wake!

Reply Report Post
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom