Halmashauri Kuu ya
CCM (NEC) iliyokutana leo imeadhimia
kupunguza wajumbe wa kamati hiyo
kutoka 34 hadi 24 pia wajumbe wa
Halmshauri Kuu kutoka 388 hadi 158.
Akizungumza mara baada ya kikao
hicho, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa
CCM, Nape Nnauye amewaambia
wanahabari leo mbali na hao pia
kamati kuu imeadhimia kupunguza
wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa
na wilaya sanjari na idadi ya vikao.
“Kamati Kuu imeazimia kufanya
uhakiki wa wanachama wake, tumeona
ipo haja ya kufanya uhakiki wa
wanachama wetu na jumuiya zake ili
kujua idadi sahihi ya wanachama wetu
kwa wakati huu kwa sababu kila
kukicha wanachama wanaongezeka na
kuna hisia wapo wengine ni hewa,”
alisema Nape
Aliongeza kuwa uhakiki huo utafanyika
kwa kutumia kadi kieletroniki na
kuachana na kadi za kawaida na
mchakato huo utakwenda sambamba
na kufuta kadi za cha jumuiya za
chama.
Mbali na Nape ambaye ni Waziri wa
Habari, Sanaa ,Utamuduni na Michezo,
amesema Mwenyekiti wa CCM Dk John
Magufuli amemteua Rodrick Mpogolo
kushika nafasi ya Naibu Katibu Mkuu
Bara, awali ilikuwa ikishirikiriwa na
Rajabu Luhavi aliyeteuliwa kuwa
balozi.
Kamati hiyo imemteua Kanali Lubinga
Ngemela kuwa Katibu wa Halmshauri
Kuu ya Taifa ya Siasa na Uhusiano wa
Kimataifa awali nafasi hiyo ilikuwa
ikishikiliwa na Dk Asha Rose Migiro
aliyeteuliwa kuwa Balozi wa Uingereza.
Hongera sana CCM well done.