Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,557
- 41,067
Putin, majeshi yake yalipoanza kuelemewa kutokana na mashambulio ya Ukraine kwa msaada wa sialaha za mataifa ya Magharibi, huku maeneo ambayo aliyokuwa ameyateka awali, yakirudi kwenye himaya ya Ukraine, aliamua kufanya maamuzi magumu na ya aibu lakini ya kuokoa jahazi.
Putin aliamua kuwatumia waovu (wafungwa) kumkwamua. Akaamuru wafungwa wote ambao watakuwa tayari kwenda mstari wa mbele kwenye vita dhidi ya Ukraine na kupigana upande wa Russia, kwanza wangepata msamaha wa vifungo walivyokuwa wakitumikia, na pia wangelipwa pesa iliyo sawa na dola 5,000 kwa mwezi. Wengi walichangamkia hiyo offer, japo kwa wengi, vifungo vyao vikabadilika kuwa adhabu ya kifo, kwa sababu walipopelekwa mstari wa mbele ilikuwa ndiyo mwisho wa maisha, na malipo ya dola 5,000 kwa mwezi yakageuka kuwa malipo hewa.
Kwa hali inavyoenda, inaonekana CCM imeamua kuiga mbinu ya Putin. Wale ambao, bila mashaka yoyote, ni watu waovu kwa kipimo cha aina yoyote, tena uovu mkubwa, kama kushiriki na kusimamia mauaji, utekaji wa watu, uporaji wa mali za watu kwa kutumia nafasi walizokuwa nao, ambao kuna wakati ili kujitakasa, CCM iliamua kuwaweka kando, sasa imeamua kuwarudisha na kuwapeleka mstari wa mbele. Je, watafia mstari wa mbele, lakini wataiokoa CCM AU watafia mstari wa mbele na kuimalizia CCM, tujipe muda.
Lakini historia inatueleza ni vigumu sana kuupata ushindi mwema kwa kutumia waovu, japo kuna nafasi ya kuupata ushindi katika uovu kwa kuwatumia waovu.
Putin aliamua kuwatumia waovu (wafungwa) kumkwamua. Akaamuru wafungwa wote ambao watakuwa tayari kwenda mstari wa mbele kwenye vita dhidi ya Ukraine na kupigana upande wa Russia, kwanza wangepata msamaha wa vifungo walivyokuwa wakitumikia, na pia wangelipwa pesa iliyo sawa na dola 5,000 kwa mwezi. Wengi walichangamkia hiyo offer, japo kwa wengi, vifungo vyao vikabadilika kuwa adhabu ya kifo, kwa sababu walipopelekwa mstari wa mbele ilikuwa ndiyo mwisho wa maisha, na malipo ya dola 5,000 kwa mwezi yakageuka kuwa malipo hewa.
Kwa hali inavyoenda, inaonekana CCM imeamua kuiga mbinu ya Putin. Wale ambao, bila mashaka yoyote, ni watu waovu kwa kipimo cha aina yoyote, tena uovu mkubwa, kama kushiriki na kusimamia mauaji, utekaji wa watu, uporaji wa mali za watu kwa kutumia nafasi walizokuwa nao, ambao kuna wakati ili kujitakasa, CCM iliamua kuwaweka kando, sasa imeamua kuwarudisha na kuwapeleka mstari wa mbele. Je, watafia mstari wa mbele, lakini wataiokoa CCM AU watafia mstari wa mbele na kuimalizia CCM, tujipe muda.
Lakini historia inatueleza ni vigumu sana kuupata ushindi mwema kwa kutumia waovu, japo kuna nafasi ya kuupata ushindi katika uovu kwa kuwatumia waovu.