Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 1,110
- 4,997
Tulizani itachukua muda mrefu kuona mgawanyiko wa kisiasa ndani ya CCM ila sasa hali si shwari.
Wazee walipoambiwa wakae kimya wameamua kukaa kimya kuanzia juu hadi kwenye mikoa. Vijana walipoambiwa chama ni mali ya familia fulani flani nao wameelewa wameamua kuendelea na maisha mengine.
Tumeona kanda ya ziwa zimetumika mbinu zote kuwavuta watu imeshindikana, boda boda wamegoma, wafanyabishara wamegoma na wazee wa chama wamegoma kujitokeza barabarani. Imelazimu tufunge shule tupate japo wanafunzi.
Vyombo vya habari vimelipwa fedha si haba kuweka propaganda , waliotangulia hakukuwa na fedha za propaganda sasa zimepatikana. Hii yote itoshe kusema misingi ya chama chetu inazidi kutikiswa. Kama tunaweza kutegemea nguvu ya vyombo vya habari kufanya siasa wakati hao wapinzani wetu wao wanatumia nguvu ya umma hatuoni kama tumepotoka?
Mwisho, kuna dharau inaendelea na inafanywa na walioshiba dhidi ya wasioshiba. Kama viongozi wote watasubiri maelekezo ya mtu mmoja tunategemea jamii itafakari vipi? Kwamba mawaziri wameshindwa kufanya kazi hadi wakumbushwe ndipo wafanye?
Mwisho wananchi wanadanganywa, hakuna miradi ya maendeleo isiyo na bajeti. Tumeona tukiambiwa jenga stendi miezi minne, jenga barabara nne, sijui jenga nini lakini fedha za kufanya haya hakuna kwenye bajeti kuu ya nchi. Mawaziri wanaosema tutajenga fedha watatoa wapi?
Chama makini kinapaswa kufanya siasa za kimkakati siyo kinachoendelea hivi sasa. Ukimdhalilisha waziri kwamba miaka yote alikuwa amekaa bila kazi siyo jambo jema kisiasa.
Dunia imebadilika sasa, kubadili njia za usafiri kuvutia wananchi siyo jambo la kufanya karne hizi kwa sababu ukweli ni kwamba hakuna kiongozi anatumia pikipiki, bajaji, punda, ngamia ,lori nk. Viongozi wote maisha yao ni V8. Je, unatembelea bajaji au lori kuonyesha nini? Kwanza Lori siyo chombo cha usafiri.
Let us act smart tunaojua thinking capacity ya chama chetu tunaona kama tunadhalllilika kwa stori zinazoendelea mtaani. One man show siyo issue tena tufanye mambo kama wanavyofanya wenzetu kwenye majukwaa ya siasa badala ya kuandaa mazingira ya wizi wa kura kwa wrong doing za watu wachache wasiotaka kujifunza.
Wazee walipoambiwa wakae kimya wameamua kukaa kimya kuanzia juu hadi kwenye mikoa. Vijana walipoambiwa chama ni mali ya familia fulani flani nao wameelewa wameamua kuendelea na maisha mengine.
Tumeona kanda ya ziwa zimetumika mbinu zote kuwavuta watu imeshindikana, boda boda wamegoma, wafanyabishara wamegoma na wazee wa chama wamegoma kujitokeza barabarani. Imelazimu tufunge shule tupate japo wanafunzi.
Vyombo vya habari vimelipwa fedha si haba kuweka propaganda , waliotangulia hakukuwa na fedha za propaganda sasa zimepatikana. Hii yote itoshe kusema misingi ya chama chetu inazidi kutikiswa. Kama tunaweza kutegemea nguvu ya vyombo vya habari kufanya siasa wakati hao wapinzani wetu wao wanatumia nguvu ya umma hatuoni kama tumepotoka?
Mwisho, kuna dharau inaendelea na inafanywa na walioshiba dhidi ya wasioshiba. Kama viongozi wote watasubiri maelekezo ya mtu mmoja tunategemea jamii itafakari vipi? Kwamba mawaziri wameshindwa kufanya kazi hadi wakumbushwe ndipo wafanye?
Mwisho wananchi wanadanganywa, hakuna miradi ya maendeleo isiyo na bajeti. Tumeona tukiambiwa jenga stendi miezi minne, jenga barabara nne, sijui jenga nini lakini fedha za kufanya haya hakuna kwenye bajeti kuu ya nchi. Mawaziri wanaosema tutajenga fedha watatoa wapi?
Chama makini kinapaswa kufanya siasa za kimkakati siyo kinachoendelea hivi sasa. Ukimdhalilisha waziri kwamba miaka yote alikuwa amekaa bila kazi siyo jambo jema kisiasa.
Dunia imebadilika sasa, kubadili njia za usafiri kuvutia wananchi siyo jambo la kufanya karne hizi kwa sababu ukweli ni kwamba hakuna kiongozi anatumia pikipiki, bajaji, punda, ngamia ,lori nk. Viongozi wote maisha yao ni V8. Je, unatembelea bajaji au lori kuonyesha nini? Kwanza Lori siyo chombo cha usafiri.
Let us act smart tunaojua thinking capacity ya chama chetu tunaona kama tunadhalllilika kwa stori zinazoendelea mtaani. One man show siyo issue tena tufanye mambo kama wanavyofanya wenzetu kwenye majukwaa ya siasa badala ya kuandaa mazingira ya wizi wa kura kwa wrong doing za watu wachache wasiotaka kujifunza.