Imebainika kuwa chama cha Mapinduzi mkoa wa Arusha kinatumia fedha nyingi ili kuwakodisha mabaunsa 7 kutoka klabu mbali mbali za usiku jijini Arusha kwa lengo la kuwafanyia Fujo wanachama wa chadema mkoani Humo.
Mabaunsa hao ambao kwa mara ya kwanza walionekana katika mahakama Kuu ya Arusha wakiwa wamevaa miwani meusi wakati wa kesi ya Nape Nnauye ambapo hata Hivyo hakufika mahakamani hapo kutokana na kuumwa.
Mwandiahi wa habari hizi aliwashuhudia tena mabaunsa hao muda Mfupi baada ya kesi ya viongozi waandamaizi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo chadema wakiwa katika viwanja vya mahakama Hiyo.
Waliingia kwa makundi ambapo kundi la kwanza liliingia na watu watatu na kwenda kukaa nyuma ya gari la katibu mkuu wa chadema Dk Wilbroad Slaa.
Hata Hivyo baadhi ya watu waliokuwepo mahakamani hapo wamedai kuwa mara Nyingi mabaunsa hao wamekuwa wakionekana katika ofisi za ccm mkoani hapo na kwamba tayari taarifa zinadai kuwa wanalipwa pesa Ndefu kwa ajili ya kushinikiza Fujo za Arusha ili baadae ionekane kuwa zimefanywa na wafuasi wa chadema.
Hat Hivyo muda mfupi baada ya Dk Slaa na viongozi wengine wa chama kuondoka mahakamani hapo mabaunsa hao nao waliondoka na kuelekea Ofisi za CCM Mkoa.
Hata Hivyo kijana mmoja ambaye ni mwanachama wa chadema alidai kuwa mmoja wa mabaunsa hao siku tatu zilizopita alifika katika eneo lake la kazi maeneo ya Unga Limited akiwa na panga na kumtishia maisha.
Taarifa zinadai kuwa mabaunsa hao wameamua kuzisahau kazi zao na kufanya kazi na ccm kwa malipo mazuri ili kuhakikisha kuwa wanachafua na kuvuruga kabisa nguvu ya upinzani Jijini Humo.
Taarifa Hizo zinaendelea kudai kuwa awali watu hao walikuwa walinzi wanaokodiwa na chadema na kwamba wameamua kugeuka baada ya kuahidiwa donge nono la shilingi laki moja kwa siku.
Source:bofya hapa:CCM YADAIWA KUKIHUJUA CHADEMA
Mabaunsa hao ambao kwa mara ya kwanza walionekana katika mahakama Kuu ya Arusha wakiwa wamevaa miwani meusi wakati wa kesi ya Nape Nnauye ambapo hata Hivyo hakufika mahakamani hapo kutokana na kuumwa.
Mwandiahi wa habari hizi aliwashuhudia tena mabaunsa hao muda Mfupi baada ya kesi ya viongozi waandamaizi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo chadema wakiwa katika viwanja vya mahakama Hiyo.
Waliingia kwa makundi ambapo kundi la kwanza liliingia na watu watatu na kwenda kukaa nyuma ya gari la katibu mkuu wa chadema Dk Wilbroad Slaa.
Hata Hivyo baadhi ya watu waliokuwepo mahakamani hapo wamedai kuwa mara Nyingi mabaunsa hao wamekuwa wakionekana katika ofisi za ccm mkoani hapo na kwamba tayari taarifa zinadai kuwa wanalipwa pesa Ndefu kwa ajili ya kushinikiza Fujo za Arusha ili baadae ionekane kuwa zimefanywa na wafuasi wa chadema.
Hat Hivyo muda mfupi baada ya Dk Slaa na viongozi wengine wa chama kuondoka mahakamani hapo mabaunsa hao nao waliondoka na kuelekea Ofisi za CCM Mkoa.
Hata Hivyo kijana mmoja ambaye ni mwanachama wa chadema alidai kuwa mmoja wa mabaunsa hao siku tatu zilizopita alifika katika eneo lake la kazi maeneo ya Unga Limited akiwa na panga na kumtishia maisha.
Taarifa zinadai kuwa mabaunsa hao wameamua kuzisahau kazi zao na kufanya kazi na ccm kwa malipo mazuri ili kuhakikisha kuwa wanachafua na kuvuruga kabisa nguvu ya upinzani Jijini Humo.
Taarifa Hizo zinaendelea kudai kuwa awali watu hao walikuwa walinzi wanaokodiwa na chadema na kwamba wameamua kugeuka baada ya kuahidiwa donge nono la shilingi laki moja kwa siku.
Source:bofya hapa:CCM YADAIWA KUKIHUJUA CHADEMA