CCM wasusia mapokezi ya Mwenge Tanga

Dec 11, 2010
3,321
6,328
KATIKA hali isiyo ya
kawaida, Chama cha
Mapinduzi (CCM) mkoani
hapa kimesusa kushiriki
katika mapokezi ya mbio za Mwenge ulioanza
kukimbizwa mkoani
Tanga juzi.

Mwenge huo uliopokewa
Wilaya ya Pangani
ukitokea Mkoa wa Pwani,
viongozi wa CCM, ngazi ya
mkoa na wilaya
hawakuonekana katika shughuli hizo jambo lililozusha maswali mengi
kwa wananchi.

CCM kabla na hata baada ya kuingia kwa mfumo wa
vyama vingi vya siasa,
imekuwa mstari wa mbele katika shughuli zote za mbio za Mwenge wa
Uhuru, ikizitumia jumuiya
zake na hasa ile ya Umoja
wa Vijana kushiriki
kikamilifu tangu mwanzo
hadi mwisho wa mbio hizo.

Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Tanga, Mussa Shekimweri, alipoulizwa
juu ya hatua hiyo, alikataa kuzungumza akidai kuwa
Katibu wake, Gustav Muba, ndiye atakayetoa taarifa
hizo.
Hata hivyo, Muba
alipoulizwa na kuambiwa kuwa mwenyekiti wake
ndiye aliyemtaka atoe
kauli, alisema kuwa chama hakina maelezo, badala
yake akadai kuwa
msemaji wa jambo hilo ni Mkuu wa Mkoa, Chiku Gallawa.

Chanzo: Tanzaniadaima
 
"Kuwasha mwenge,
Kuwasha mwenge,
Na kuuweka Kilimanjaro.
Umulike hata nje ya mipaka yetu,
Ulete tumaini.
Pale ambapo hapana matumain.
Upendo mahali ambapo panachuki,
Na heshima ambapo pamejaa dharau!"

Kama tunauwasha mwenge na kuukimbiza kwa malengo yatu ya awali, nadhani tutakuwa tunatenda haki na tutaheshimiwa na vizazi vijavyo. Lakini, kwakuwa tumeyaacha na kuyasahau malengo ya kuwasha mwenge, nadhani ni wakati muafaka wa kuuweka jumba la makumbusho ili utumike kuwafundisha watoto wetu mambo mema tuliyowahi kuyafanya kwa nchi yetu na si kujitafutia kudharaulika kunakofanywa sasa.
Hongereni ccm Tanga kama mmesusa kwa sababu hizi.
 
Tanga kwa siitofautishi na Arusha au Tunduma uatakumbuka kwenye sherehe za May mosi Mh Rais alipokelewa na wanachama wa CUF badala ya CCM kama tulivyo zoea pia
 
yaani hadi CCM Tanga wamesusa. Pole baba MwanaAsha maana kama joto ya jiwe unaipata
 
Mi nadhani Mwenge kwa sasa hauna tena tija, bora uwekwe makumbusho Filipo ibaki historia yake tuu. Mwenge ni kiini macho kwa sasa.
 
Last edited by a moderator:
Sasa kama hawajapewa posho, waje huko kufanya nini? Posho kwanza, mengine baadaye kudadadeki.
Au nakosea Mh. Lusinde?
 
MWENGE? HEBU NIM-QUOTE MH. GODBLESS LEMA AKIWA PALE UBUNGO-MWISHO KIBO, JUZI
"...Huu mnaosema Mwenge..mwenge..mwenge ni moto tu huu unakimbizwa kwa gharama ya Sh Million 200..
ili kwenda kufungua choo cha shule cha kilichojengwa kwa Sh Laki 2, zahanati ya sh laki Sita..
Ni uchawi wa chama chao ni mazindiko tu yao kuwahadaa wananchi.. ni Moto tu huo unakimbizwa kwa Mabilioni
ya pesa za walipa kodi'
 
MWENGE? HEBU NIM-QUOTE MH. GODBLESS LEMA AKIWA PALE UBUNGO-MWISHO KIBO, JUZI
"...Huu mnaosema Mwenge..mwenge..mwenge ni moto tu huu unakimbizwa kwa gharama ya Sh Million 200..
ili kwenda kufungua choo cha shule cha kilichojengwa kwa Sh Laki 2, zahanati ya sh laki Sita..
Ni uchawi wa chama chao ni mazindiko tu yao kuwahadaa wananchi.. ni Moto tu huo unakimbizwa kwa Mabilioni
ya pesa za walipa kodi'

Mkuu umeshaniharibia siku aisee, nammiss sana huyu kamanda mpiganaji!
 
"Kuwasha mwenge,
Kuwasha mwenge,
Na kuuweka Kilimanjaro.
Umulike hata nje ya mipaka yetu,
Ulete tumaini.
Pale ambapo hapana matumain.
Upendo mahali ambapo panachuki,
Na heshima ambapo pamejaa dharau!"

Kama tunauwasha mwenge na kuukimbiza kwa malengo yatu ya awali, nadhani tutakuwa tunatenda haki na tutaheshimiwa na vizazi vijavyo. Lakini, kwakuwa tumeyaacha na kuyasahau malengo ya kuwasha mwenge, nadhani ni wakati muafaka wa kuuweka jumba la makumbusho ili utumike kuwafundisha watoto wetu mambo mema tuliyowahi kuyafanya kwa nchi yetu na si kujitafutia kudharaulika kunakofanywa sasa.
Hongereni ccm Tanga kama mmesusa kwa sababu hizi.

Umenena kweli mkuu maana sasa hivi hakuna matumaini tena !
 
KATIKA hali isiyo ya
kawaida, Chama cha
Mapinduzi (CCM) mkoani
hapa kimesusa kushiriki
katika mapokezi ya mbio za Mwenge ulioanza
kukimbizwa mkoani
Tanga juzi.

Mwenge huo uliopokewa
Wilaya ya Pangani
ukitokea Mkoa wa Pwani,
viongozi wa CCM, ngazi ya
mkoa na wilaya
hawakuonekana katika shughuli hizo jambo lililozusha maswali mengi
kwa wananchi.

CCM kabla na hata baada ya kuingia kwa mfumo wa
vyama vingi vya siasa,
imekuwa mstari wa mbele katika shughuli zote za mbio za Mwenge wa
Uhuru, ikizitumia jumuiya
zake na hasa ile ya Umoja
wa Vijana kushiriki
kikamilifu tangu mwanzo
hadi mwisho wa mbio hizo.

Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Tanga, Mussa Shekimweri, alipoulizwa
juu ya hatua hiyo, alikataa kuzungumza akidai kuwa
Katibu wake, Gustav Muba, ndiye atakayetoa taarifa
hizo.
Hata hivyo, Muba
alipoulizwa na kuambiwa kuwa mwenyekiti wake
ndiye aliyemtaka atoe
kauli, alisema kuwa chama hakina maelezo, badala
yake akadai kuwa
msemaji wa jambo hilo ni Mkuu wa Mkoa, Chiku Gallawa.

Chanzo: Tanzaniadaima

Mwenge wa Laana!
 
Back
Top Bottom