CCM wapo njiapanda bunge la katiba

CCM wapo njiapanda bunge la katiba

mcfm40

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2010
Posts
4,452
Reaction score
3,152
Wamejiweka kwenye dillemma mbaya kabisa. Kila upande wanaogusa hauna nafuu. Wanatamani kuahirisha bunge la katiba wanaona aibu wakiwa na wasiwasi pia na impact yake kwao kisiasa. kwamba ukawa wataonekan wameshinda.

Kuendelea na bunge nako kuna adhari mbaya pia. hawatakuwa na theluthi mbili wakati wa kufanya maamuzi na hivyo katiba kukwama. hivyo lawama watabeba wao.

Pia mambo yote wanayofanya mle hasa kuondoa maoni ya wananchi na kujipendelea wao yatafanya mchakato uonekane haukuwa na maana. Hivyo watalaumiwa wao moja kwa moja.na pia ni kujitia kitanzi maana inawaonesha rangi zao hasa.

Inaonekana kwamba wameamua kuchagua the lesser evil ambalo ni kuendelea na BMK potelea mbali. Lakini mimi naona wamechagua vibaya hili lesser evil.

Hili lina adhari mbaya zaidi kwao kuliko wangeamua kusimamisha mchakato na kuweka mambo sawa kwanza. Pampoja na kwamba wangejisikia kam wamezidiwa na ukawa lakini wangeonekana wamekuwa na busara zaidi. na wangejiepusha na aibu kubwa zaidi mbele ya safari hasa hii ya kula posho na raismu kwenda kukataliwa na wananchi.

Ila kwa vyovyote vile CCM watakavyofanya ukawa watakuwa na ushindi km wataendelea kushiklia msimamo wa kutorudi bungeni. hasa hili la kukubali kupoteza maposho yote hayo kwa ajili ya kutetea maoni ya wananchi yaliyomo kwenye katiba.

Na sasa ukawa wanazidi kupata nguvu kutokana na CCM kuanza kuondoa waziwazi yale maoni mazuri ambao watu waliyashabikia sana km kuwadhibiti wabunge, mawaziri kutokuwa wabunge, kupunguza mamlaka ya rais.

Hili linaonesha kinagubaga kwamba kweli CCM hawana nia njema na hili swala la katiba.

Ukawa shikilieni hapohapo matapoteza maposho manono lakini matagain sana kisiasa! Mwisho wa siku madudu ya CCM yataonekana.
 
Kuna picha moja ina mtu kapaka rangi hadi kajikuta kwenye kona hajui amalizieje...
When you start something first think how to finish it
 
Kaa jingine la moto... halitemeki wala hakimezeki...

Kama Lowassa
 
BMK hawana cha maana wanachofanya DDM kama walianza na zile sura(MUUNGANO) wakashindwa kuelewana iweje waendelee na sura zingne? naamini sura zingine zimebase kwenye muungano ndo maana waliamua waanze na muundo wa muungano cha ajabu wameshindwa kuamua ni aaina gani ya muungano inatufaa afu wanaendelea na sura zingine.Je wakiendelea kujadili mambo ambayo hayapo kwenye rasimu ya pili ya katiba then hiyo katiba ije ikataliwe na wananchi MTARUDISHA HIZO KODI ZETU MNAZOKULA? me CCM wananishangaza sana kweli hamwoni athari gani tutapata baadae au bora liende sometimes kubaliN kukosolewa we are all building the same country kumbukeni waliotoa maoni ni WATANZANIA SIO WANACCM,CDM CUF OR NCCR-MAGEUZI
 
Wengine wameanza kujiunga na Ukawa. Wengi watafuata
JK huna think Tanks. Bora utumie JF kuna vichwa vya ukweli.
 
CCM wameamua potelea mbali lolote litakalokuwa wao awajali ilimradi wamepata fedha.na wanasema wazi kwamba,wanao uwezo wa kubadilisha maoni yoyote yaliyotolewa na wananchi
 
Hawa nisawa nagari iliyopoteza muelekeo,wamekosa hata mtu wakuweka kigogo ,hivyo basi tuwaache waporomokee shimoni sie tukaokote mizoga nakwenda kuizika hii itakuwa salama kwetu maana tukiendelea kuiacha itatukwaza kwa kutunukia uozo.
 
Hawa nisawa nagari iliyopoteza muelekeo,wamekosa hata mtu wakuweka kigogo ,hivyo basi tuwaache waporomokee shimoni sie tukaokote mizoga nakwenda kuizika hii itakuwa salama kwetu maana tukiendelea kuiacha itatukwaza kwa kutunukia uozo.

Hivi hawa jamaa wanakosa kabsa wazee wa busara kuwaonesha huku tuendako siko? Maslahi ya muda mfupi haya yataipeleka nchi pabaya. Halafu nasikia prof. Shivji ameitwa kuwashauri muundo wa muungano. lakini ni Prof. huyu huyu aliyeliponda sana mchakato wa kuapata hii katiba has muundowa BMK kwamba lilipaswa liwe la kuchaguliwa moja kwa moja na wananchi. Kwa muda mrefu wa maisha yake amekuwa mtetezi wa wanyonge. Nachojiuliza ni je Shivji haoni jinsi maoni ya wanyonge yanavyonyongwa na BMK? Je anabariki na kwenda kushirikiana nao kuzidi kuwakandamiza maoni ya watanzania kwa kushirikiana na watawala? Shivji yupo tayari kwa athari zitakazompata hasa kupoteza hadhi yake kam msomi aliyeaminika kwa kusaidia kuvuruga mchakato wa katiba?

Anataka kuishi katika hii nchi kama mwizi? Km hataki basi awaambie CCM ukweli kwamba wananchofanya sio! Asimamie usomi wake. Ukuu wa maoni ya wananchi katika katiba ambao shivji amekuwa akiupigia kelele uko wapi? Katiba kama muafaka wa kitaifa ambao ndio umekuwa wimbo wake ndicho kinachofanyika dodoma?
 
CCM wameamua kujitoa ufahamu kwa makusudi. Sasa wanaanza sinema ya kuja mbele ya waandishi wa habari wakijifanya eti kukanushana huku ikiwa ni gia ya kuvunja bunge la katiba kwa maana ya eti wengi wao wameona ni busara kuungana na ukawa!!
 
Nasema hivi... katiba itakayopitishwa na BMK lazima ipite kwani waliobungeni ni wawakilishi halali wa wananchi na kura itasimamiwa kuhakikisha hiyo katiba inapita tu. Tunashukur kuwa Zenji kuliko na tatizo sasa 2/3 itapatikana bila shida yoyote.UKAWA shauri yenu...!!!?
 
Back
Top Bottom