Ndugu wana JF,
Katika manispaa ya Moshi katika kata ya Kiborloni kutakuwa na uchaguzi mdogo baada ya Diwani wa kata hiyo ambaye pia alikuwa Naibu Meya wa Manispaa Bwana Vicent Rimoy kufariki.Uchaguzi huo utafanyika tarehe 9-2-2014.
Inavyoelekea mpaka sasa CCM wameelemewa kiasi cha kukosa kabisa wahudhuriaji kwenye mikutano yao ya hadhara.
Kama ilivy kawaida ya CCM wakaanza jitihada za kuhujumu uchaguzi ikiwa ni pamoja na kuwahadaa wapiga kura wauze shahada zao kwa sh 10,000 hadi 20.000 kutegemea na mwonekano wa mtu,jambo ambalo limelalamikiwa na Chama cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA).
Hata hivyo habari zimeenea tangu juzi kuwa kuna vijana wamechangamkia offer hiyo na ku -scan vitambulisho vya kupigia kura na kuwauzia CCM.
Kwa kuwa mazingira ya kuuziana ni kwenye giza na kazi hiyo inafanyika kati ya saa mbili hadi saa 4 usiku ,CCM wamejikuta wamenunua shahada zilizogushiwa na wauzaji watapiga kura kwa vitambulisho halali.
Mpango huu umeandaliwa kwa ustadi mkubwa na CHADEMA baada ya kugundua pasipo shaka kwamba CCM wananunua shahada za wapiga kura hasa nyakati za jioni na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa dhidi yao hata ukutoa taarifa TAKUKURU hata Polisi.
Mategemeo ya wengi uchaguzi huu utawaliza sana CCM kutokana na ujanja huu waliofanyiwa huku wakiamini shahada walizo nazo ni halali.
Katika manispaa ya Moshi katika kata ya Kiborloni kutakuwa na uchaguzi mdogo baada ya Diwani wa kata hiyo ambaye pia alikuwa Naibu Meya wa Manispaa Bwana Vicent Rimoy kufariki.Uchaguzi huo utafanyika tarehe 9-2-2014.
Inavyoelekea mpaka sasa CCM wameelemewa kiasi cha kukosa kabisa wahudhuriaji kwenye mikutano yao ya hadhara.
Kama ilivy kawaida ya CCM wakaanza jitihada za kuhujumu uchaguzi ikiwa ni pamoja na kuwahadaa wapiga kura wauze shahada zao kwa sh 10,000 hadi 20.000 kutegemea na mwonekano wa mtu,jambo ambalo limelalamikiwa na Chama cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA).
Hata hivyo habari zimeenea tangu juzi kuwa kuna vijana wamechangamkia offer hiyo na ku -scan vitambulisho vya kupigia kura na kuwauzia CCM.
Kwa kuwa mazingira ya kuuziana ni kwenye giza na kazi hiyo inafanyika kati ya saa mbili hadi saa 4 usiku ,CCM wamejikuta wamenunua shahada zilizogushiwa na wauzaji watapiga kura kwa vitambulisho halali.
Mpango huu umeandaliwa kwa ustadi mkubwa na CHADEMA baada ya kugundua pasipo shaka kwamba CCM wananunua shahada za wapiga kura hasa nyakati za jioni na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa dhidi yao hata ukutoa taarifa TAKUKURU hata Polisi.
Mategemeo ya wengi uchaguzi huu utawaliza sana CCM kutokana na ujanja huu waliofanyiwa huku wakiamini shahada walizo nazo ni halali.