CCM wanajua wanachokifanya,

CCM wanajua wanachokifanya,

Mapambano Yetu

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2012
Posts
1,133
Reaction score
2,128
Ukitafakari mazingira yanayoandaliwa na ccm dhidi ya kura ya maoni na maandalizi ya uchaguzi mkuu mwakani utakubaliana na Mimi Kuwa wanajua nini wanafanya na ni kwa jinsi gani watafanikiwa.

Huku mtaani kwetu Mabalozi wa nyumba kumi kumi wanakusanya vitambulisho vya kupigia kura, lengo liko kwenye mabano.

Baadhi ya maeneo ccm wanachangisha michango ya Siri kutoka kwa wafanya biashara na taasisi. Michango hiyo ni Kuanzia laki moja na kuendelea, lengo pia liko kwenye mabano.

Tumekwisha they know what they are doing.
 
Kama jambo hili linaukweli basi wananchi wa nchi hii ndo tatizo utakubali vipi kupokea amri /maagizo kutoka kwa balozi mtu ambaye kikatiba hatambuliki? Mambo ya mjumbe wa nyumba kumi ni ya ccm akikufata mtu kama huyo akakuomba kitambulisho na kukutoza michango muulize mamlaka hayo kayapata wapi.
 
Mimi ni mwanahesabu,,iko hivi
A.Wanachama na wapenzi/wafurukutwa wa chama tawala wa kawaida na wafanya biashara wenye nia njema na chama kuendelea kushika dola wanaaswa kukichangia chama kiasi chochote kukamilisha ajenda ya Kura ya maoni,uchaguzi wa serekali za mitaa na uchaguzi mkuu 2015
B.Fedha zotakazokusanywa zitatolewa kwa wale watukutu na wasio na msimamo wa uhakika na mapenzi mema ya chama ndio hupewa fungu kwa ajili ya kuwashawishi kubaki njia kuu na pia kuwabadili mtizamo wale wote wenye tamaa ya rupia kujiunga na chama kikuu.
Huu ni mtazamo wangu na hauhusiani na mipango yoyote ya chama kikuu.
 
Back
Top Bottom