Its Tesha
Senior Member
- Oct 6, 2025
- 168
- 606
Hapo awali, tulikuwa taifa la watu waliokuwa wanaenda makazini na kurudi majumbani bila ulinzi, tukiishi kwa amani tele. Hakuna aliyekuwa anamdhuru mwenzake; uungwana na utu vilikuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Leo hii mambo yamebadilika — watu wanalindwa baa, mitaani, na hata barabarani kana kwamba tuko vitani.
Hii siyo Tanzania tuliyoizoea. Watanzania si watu wa vurugu, si watu wa chuki; haya ni mambo mapya ambayo CCM wameyataka, na bado wanaendelea kuyataka.
Nchi ipo njia panda, hakuna kinachoendelea zaidi ya kukamatana, kuwindana, visasi na vilio. Ni hali ya huzuni na kuchanganyikiwa, hasa kwa wale waliokuwa na imani kwamba amani yetu ni ya kudumu.
Kwa sasa, ni wazi kabisa CCM wamechanganyikiwa, hawajui nini cha kufanya.
Hii siyo Tanzania tuliyoizoea. Watanzania si watu wa vurugu, si watu wa chuki; haya ni mambo mapya ambayo CCM wameyataka, na bado wanaendelea kuyataka.
Nchi ipo njia panda, hakuna kinachoendelea zaidi ya kukamatana, kuwindana, visasi na vilio. Ni hali ya huzuni na kuchanganyikiwa, hasa kwa wale waliokuwa na imani kwamba amani yetu ni ya kudumu.
Kwa sasa, ni wazi kabisa CCM wamechanganyikiwa, hawajui nini cha kufanya.