CCM, vita mliyoianzisha ya kupambana na makanisa hamtoishinda

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,272
Baada ya CCM kufikiri wamemaliza nguvu za upinzani waliodhani ndio wakosoaji pekee, limeibuka wimbi la watumishi wa Mungu na viongozi wa dini na makanisa mbalimbali kumkosoa Rais waziwazi kwa utendaji wake.

Baada ya kuona hivyo, vijana wa CCM na serikali yake kwa kutumiwa au kujituma wenyewe wameanzisha vita na kanisa, wanawabeza na kuwajibu viongozi wa dini kama vile wanamjibu Mbowe, wanawaita viongozi wa dini ni vibaraka wa mafisadi, vibaraka wa wazungu, wezi wa mali ya umma n.k n.k.

CCM wameamua kupambana na kanisa kama vile wanapambana na CHADEMA au CUF. Niwaeleze CCM kuwa hii vita mliyoianzisha si lelemama ni kubwa kuliko wanavyodhania inaweza kukisambalatisha chama chenu na serikali yake, hebu chungulieni kwa majirani zetu Congo mpate kujifunza yanayotokea.

Kanisa ni tofauti na chama cha siasa, msitegemee Rais atakuja kupiga marufuku mikutano ya dini kama alivyopiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa hadi 2020. Msitegemee Rais atayafuta makanisa kama alivyosema atahakikisha kufikia 2020 hakutakuwa na chama cha upinzani. Anachoweza ni kuwasumbua baadhi ya viongozi wake lakini si kanisa.

Nguvu ya kanisa ni kubwa kuliko nguvu ya chama cha siasa kanisa lina nguvu kuliko hata serikali (anayebisha nitampa mifano). Kanisa lina waumini wa itikadi zote na wananchi wa vyama vyote wa ngazi zote na wa matabaka yote mijini na vijijini. Kanisa kama Roman Catholic na KKKT ni matawi tu yako duniani kote, kwahiyo kulia-attack kanisa la RC Tanzania ni ku attack makanisa yote ya Roman Catholics.

Nimalizie kwa kuwaonya vijana wa CCM na CCM yenyewe wasicheze na imani za watu, viongozi wa dini waheshimiwe na kanisa lazima liheshimiwe.
 
Watanzania wana akili za kutosha!

Kanisa lilijaribu kuwaburuza 2010 dhidi ya Jakaya lakin bila ya kujali dini zao walipuuza chuki pandikizwa!

Magu anatikiswa Na Kanisa arudishe ile Migao aliyoifyeka na akiwarudishia zile ruzuku watasahu yote waliyosema

Kanisa ndio Miaka yote lilikuwa linasisitiza tusichanganye Dini Na Siasa Kumbe Kwa kuwa walikuwa wanafaidika

Magenge yote ya Escrow yanapitia wakati mgumu
 
Watanzania wana akili za kutosha!

Kanisa lilijaribu kuwaburuza 2010 dhidi ya Jakaya lakin bila ya kujali dini zao walipuuza chuki pandikizwa!

Magu anatikiswa Na Kanisa arudishe ile Migao aliyoifyeka na akiwarudishia zile ruzuku watasahu yote waliyosema

Kanisa ndio Miaka yote lilikuwa linasisitiza tusichanganye Dini Na Siasa Kumbe Kwa kuwa walikuwa wanafaidika
Magufuli hatikiswi na kanisa anatikiswa na matendo yake, hakuna aliyeshindana na kanisa akabaki salama.
 
Quinine
Hujui nguvu ya kanisa iko wapi. Hayo siyo makanisa ni vijiwe vya wachumia Sadaka. Wanatafuta upepo wa kupita. Subiti Watapotea kama Ngwajima na Madude yake. Hawana jingine zaidi ya kutoa tamko ili wapate mvuto pasaka hii. Swali kwanini hawajasimama Pamoja kumpitisha lowasa awe raisi? Kwa nini walitudanganya wameonyeshwa Raisi ni lowasa?
 
Unafiki mbaya sana,Masheikh wakidhalilishwa hakuna anayeinyooshea kidole serikali lakini leo wameguswa kidogo tu Wachungaji na Maaskofu mnashindana kufungua threads za kulaumu serikali na CCM!
Mashehe huwa hawana unafiki kama wa Pengo
 
Hujui nguvu ya kanisa iko wapi. Hayo siyo makanisa ni vijiwe vya wachumia Sadaka. Wanatafuta upepo wa kupita. Subiti Watapotea kama Ngwajima na Madude yake. Hawana jingine zaidi ya kutoa tamko ili wapate mvuto pasaka hii. Swali kwanini hawajasimama Pamoja kumpitisha lowasa awe raisi? Kwa nini walitudanganya wameonyeshwa Raisi ni lowasa?
Unazungumzia kanisa gani, mimi nazungumzia makanisa yaliyotoa Waraka ya RC na KKKT.
 
Unafiki mbaya sana,Masheikh wakidhalilishwa hakuna anayeinyooshea kidole serikali lakini leo wameguswa kidogo tu Wachungaji na Maaskofu mnashindana kufungua threads za kulaumu serikali na CCM!
Hadi waislamu nao huwa hawainyoshei serkali kidole, pindi masheikh wanapodhalilishwa.??
Kwani wakristu wanawategemea waislamu kunyoosha kidole pindi watumishi wao wanapodhalilishwa..?
Kwani waislamu wanawategemea wakristu kunyoosha kidole pindi masheikh wao wanapodhalilishwa
 
Back
Top Bottom