CCM tupo katika mwanguko mkubwa

Mkuu unaposema wabunge wa CCM wanayaacha ya kutetea wananchi, kuisimamia serikali na kujadili bajeti sikuelewi hata kidogo!

Wote hapa tuoangalia bunge tumeshuhudia jinsi wabunge wengi wa CCM wanavyojadili kwa ufanisi na ustaarabu mkubwa wanapotoa michango yao.

Unapoona yanatokea tofauti na nilivyoandika kwenye aya yangu ya pili, basi ujue kuna utovu wa nidhamu uliosababishwa na kambi ya upinzani.
 
Absalom kibanda alisema sekretariat mpya ya ccm chini ya comred kinana si ya kupuuzwa, unaona sasa mmeanza kuweweseka..na bado
 
hiyo inaitwa kupaa kwa ccm na anguko la ccm .
futilia ziara ya nape utamwonea huruma!
 
Ni ajabu sana miaka 52 ya uhuru na ukubwa wa serikali yote lakini wameshindwa kutatua tatizo la wanafunzi kukalia mawe.
 
Chadomo wanahangaika mara wajifanye CCM yaani ni kuhangaika kama kuku anaetaka kutaga.Nenda Babu akakupe kifuta jasho chako.
 

mkuu hawa watu wamekabwa koo, wameanza kutapatapa..mwanachama wa ccm hawezi kuleta huu ujinga hapa jukwaani
 
ccm ina wabunge wanne tu wanaotoa michango ya maana bungeni,hao wengine ni waimba taarabu na mipasho.
1.DEO
2.ESTER BULAYA
3.KANGILUGOLA
4.na mbunge wa kisesa,MH MPINA
 
Hii ni sawa na Chama kinachopokea mamilioni kwa mwezi kushindwa kujenga ofisi zake.Siku kikipewa madaraka si ndio kitafilisi nchi
Ni ajabu sana miaka 52 ya uhuru na ukubwa wa serikali yote lakini wameshindwa kutatua tatizo la wanafunzi kukalia mawe.
 
Mfe na muishie Jehanamu ya moto wa milele.
 
Ccm kwa sasa ndio ipo imara kuliko wakati mwingine wowote ule..mtahangaika sana

unajifariji tu kak ila ukweli utabakia palepale. yafaa mtu mzima ukawa mchambuzi na mwenye maono zaidi kuliko kukataa ukweli. Baadhi ya vilaza wa ccm ndo upo wewe kwa kua ni kipofu na usiye na maono ya kukisaidia chama chako. bisha kitu ambacho ni cha kweli na ndo utakuwa na confidence ya kutetea jambo. kwa hali ilivyo watanzania wanaelewa sana jisi mnavyohangaika kila kona na kutumia fedha nyingi, mamliki, polisi usalama wa taifa, waandishi, wakuu wa wilaya na mikoa, watanzazaji na vyombo vingined kutaka kuzima democrasia inayochochewa na wananchi kupewa taarifa ya hali halisi. wewe unajifariji tu hujui uchungo uliopo kwenye mioyo ya watanzania wengi kuanzia Mtwara mpaka kagera. Wamejeruhiwa na ufisadi, poraji, wizi unaofanywa na wawekezaji kwa mgongo wa ccm, maisha yamekuwa magumu kila siku wananchi wanataabika ninyi mnaleta kina nape kuja kuongopea ili hali uhalisia unajulikana. ni vyema mketumia muda wenu mkajitakasa kwa kuchapa kazi na sio kila kukicha kuanzia bungeni kila anayesimama anasema chadema, kwa mikutano chadema yaani mnakera sana. Nape alivyo kilaza morogoro anawahadaa wananchi kuwa chadema ndio wametukana bngeni angali waliotoa matusi wote ni ccm. ANAONGEA KWA FUJO KAMA ANARAP VILE ILI KUONESHA HASIRA KUMBE ANABAKI AKIDHASRAULIKA. HAMNA JAMBO BAYA KAMA UONGO NA HADAA. sasa trustya mwananchi itatoka wapi? Tunamuona serukama, nkamia, lusinde live ndo walitoa LUIGHA CHAFU NA MAMA ABDALLAH AKAKEMEA, SASA YEYE ANASEMA NI CHADEMA!IS IT SENSIBLE?NO!TUMEWAJUA KUWA NI NINYI NI WATAALAMU WA UONGO NA HADAA. UKWELI KWENU NI MWIKO UONGO DAIMA NDIO MSINGI WENU WA USHINDI.HAMTAFIKA MBALI.
 
alikuja dr malaria sugu akaondoka. Akaja kupeng'e akaondoka. Faiza foxy nae akatoweka. Akaja rejao akatoweka. Akaja chama akatoweka. Akaja majebere akapotea. Sasa bungeni. Kipindi chote hiki ritz yupo tu! Jiteteeni sasa
 
ccm ina wabunge wanne tu wanaotoa michango ya maana bungeni,hao wengine ni waimba taarabu na mipasho.
1.DEO
2.ESTER BULAYA
3.KANGILUGOLA
4.na mbunge wa kisesa,MH MPINA

wabunge wa ccm wapo organised, hawalipuki ovyo na wala hawana muda wa kuchezea kwa hiyo hao wachache uliowaona ni wawakilishi wa wengi...lekule laizer anakusalimia sana.mwigulu na jafo
 
Kwa kweli umenena bila kumumunya maneno. Kazi kwetu sisi kama vijana kuikomboa nchi yetu 2015 kupitia CHADEMA chini ya Rais wetu Dr Slaa.
 
........''Mkuu mbona hata mwenyekiti wetu siku si nyingi zilizopita alituambia tusitegemee polisi,tuwajibu wapinzani,ndio tunavyofanya.Hii sio kazi ya PR machines pale Lumumba pekee yake,hata spika na naibu wake, hata wabunge,hata sisi humu JF,mwenzetu Pasco,Lukosi,Bungeni,Ritz na wengineo.We huoni kwenye deni la taifa,billion 600 hazina maelezo sasa wapinzani wakichukua nchi huyu mtalii wetu itabidi ajibu zilienda wapi.Hawa Wadanganyika inabidi tuwatawale milele,tutengeneze Katiba ya hovyo itayo kidhi matakwa yetu,tukijengee chama uwezo wa kifedha kwa kufanya biashara ya gesi kule Mtwara kama middleman,tutumie TISS kama chombo cha kuogofya wapizani na tuwe na nguvu kazi ya kutosha kuhubiri mambo yetu kila mkoa na wilaya yaani DCs na RCs.Kwa mikakati hii tutatawala mpaka basi au mpaka pale tutakapomaliza hizi rasimali zao ndio tuwaachie wapizani..........''

Haya ndio mawazo ya wenzetu walioshika dola.Ila mapambano yanaendelea na haki siku zote lazima itafutwe iwe kwa hiari au kwa kusuruba.
 
Mimi pia naona anguko hilo na hakika CCM sichama chakufa chenyewe ila kitakufa kwa kuuwawa na tuliowapa uongozi wa chama chetu. Mimi nasikitika kuwa BUNGE limegeuka la watawala na watawaliwa. Watawala ni wabunge na mawaziri wa CCM watawaliwa ni Wabunge wachache sana wa upinzani. Je wabunge wa CCM wasipowatetea wananchi na badala yake wakawa wanatetea serikali basi sisi wananchi hatuna lakufanya tusubiri hadi 2015 tubadili serikali huu ndio utakuwa ukombozi wetu wananchi
 

acheni ku lwakatare watu..
 
Kamuulize mwigulu nchemba madelu ndio atakwambia umakini wa ccm sio ukurupuke na njaa zako za kulipwa kwa thred na post uje uwahadae watu humu.mleta mada shame on you!
Mkuu unakera sana hapa jamvini jifunze jinsi ya kupangilia comment zako badala ya kujaza ukurasa mzima kwa vicoment vifupi vifupi vya kijinga
 
[JFMP3]WANA CCM WENZAKO....!
:lalala: [/JFMP3]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…