CCM tumemshindwa Lowassa?

CCM tumemshindwa Lowassa?

Concrete

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2011
Posts
3,605
Reaction score
551
Ni jambo la wazi kabisa kwa sasa kuwa kwa vyovyote vile itakavyokuwa Edward Lowassa ana nafasi kubwa sana kuwa mgombea urais wa CCM 2015.

Lowassa ambaye huenda ndiye mtu anayejulikana na watanzania wengi zaidi kama ni mwanaCCM mchafu(Fisadi) zaidi lakini Lowassa ndiye mwanaCCM mwenye nguvu zaidi ndani na nje ya CCM kwa sasa.
Binafsi mpaka sasa sioni namna yoyote kwa chama changu cha mapinduzi kama kinaweza kuepusha Lowassa asiwe mgombea urais wa CCM 2015.

Mikakati mbali mbali ya makusudi ndani ya serikali na CCM imefanyika tena kwa juhudi kubwa ili kumdhibiti Lowassa kisiasa kuanzia kushinikiza kujiuzuru kwake uwaziri mkuu kwa kashfa ya Ufisadi mpaka mkakati wa kujivua gamba na kuteua mara mbili secretariety mpya ya CCM lakini bado havikusaidia kitu.

Karibu kila kada mwandamizi ndani ya CCM imeshachoka kumdhibiti Lowassa na wapambe wake kisiasa na kwa sasa karibu kila kada wa CCM ambaye hampendi Lowassa ameanza kumwogopa sana au kujipendekeza. Mfano rahisi kabisa ni Nape Nnauye ambaye anaogopa kabisa kutaja hata neno Lowassa au Fisadi hadharani kwa sasa na Mwigulu Nchemba ambaye tayari 'ametangaza' kuwa yuko pamoja na Lowassa bega kwa bega katika mbio za urais.

Wakati Lowassa akizidi kuchanja mbuga katika mbio zake za urais kisiasa kupitia makundi mbalimbali ya kijamii na kidini, kambi zingine hasimu za urais ndani ya CCM zimechoka sana na wamebaki kulalamika, kunung'ung'unika na kuhangaika tu.
Kuanzia kambi ya Samweli Sitta, Benard Membe, Fredrick Sumaye nk. kwa sasa wanasubiri miujiza ya kisiasa pekee ndani ya CCM ili waweze kumshinda Lowassa.

Swali, CCM tumeshindwa kumdhibiti Lowassa?
 
Wajumbe wa vikao husika ndio waamuzi wa mwisho. Nyingine zote porojo tu...
 
Wajumbe wa vikao husika ndio waamuzi wa mwisho. Nyingine zote porojo tu...
Ndio hao hao ninaowazungumzia hapa. Wajumbe ni wawakilishi wa watu wengine. Kama ukitafiti kidogo tu utagundua wajumbe wengi sana wa vikao vya maamuzi vya CCM ni wapambe wa Lowassa.
 
ni jambo la wazi kabisa kwa sasa kuwa kwa vyovyote vile itakavyokuwa edward lowassa ana nafasi kubwa sana kuwa mgombea urais wa ccm 2015.

Lowassa ambaye huenda ndiye mtu anayejulikana na watanzania wengi zaidi kama ni mwanaccm mchafu(fisadi) zaidi lakini lowassa ndiye mwanaccm mwenye nguvu zaidi ndani na nje ya ccm kwa sasa.
Binafsi mpaka sasa sioni namna yoyote kwa chma changu cha mapinduzi kama kinaweza kuepusha lowassa asiwe mgombea urais wa ccm 2015.

Mikakati mbali mbali ya makusudi ndani ya serikali na ccm imefanyika tena kwa juhudi kubwa ili kumdhibiti lowassa kisiasa kuanzia kushinikiza kujiuzuru kwake uwaziri mkuu kwa kashfa ya ufisadi mpaka mkakati wa kujivua gamba na kuteua mara mbili secretariety mpya ya ccm lakini bado havikusaidia kitu.

Karibu kila kada mwandamizi ndani ya ccm imeshachoka kumdhibiti lowassa na wapambe wake kisiasa na kwa sasa karibu kila kada wa ccm ambaye hampendi lowassa ameanza kumwogopa sana au kujipendekeza. Mfano rahisi kabisa ni nape nnauye ambaye anaogopa kabisa kutaja hata neno lowassa au fisadi hadharani kwa sasa na mwigulu nchemba ambaye tayari 'ametangaza' kuwa yuko pamoja na lowassa bega kwa bega katika mbio za urais.

Wakati lowassa akizidi kuchanja mbuga katika mbio zake za urais kisiasa kupitia makundi mbalimbali ya kijamii na kidini, kambi zingine hasimu za urais ndani ya ccm zimechoka sana na wamebaki kulalamika, kunung'ung'unika na kuhangaika tu.
Kuanzia kambi ya samweli sitta, benard membe, fredrick sumaye nk. Kwa sasa wanasubiri miujiza ya kisiasa pekee ndani ya ccm ili waweze kumshinda lowassa.

Swali, ccm tumeshindwa kumdhibiti lowassa?

lowassa ndani ya ccm ni dume la mbegu!!!!wamuulize sophia simba na beatrice shellukindo!!!
 
kwa hiyo unataka kusema 2015, Nappe anahama nchi.?
 
CCM wameshaozea kukata majina sasa nangojea siku watakapokata jina la Jamaa njisi zahma itakavyokuwa -- so far wapo wana CCM 4 wanaoonyesha nia ya urais kwa tiket ya CCM
Nimewapanga kutokana na nguvu zao nje na ndani ya chama
1. Edward Lowassa
2. Samweli Sitta
3. Benald Membe
4. Lazaro Nyarandu

Wengine watakuwa wanatimiza idadi tu (making up the numbers)
 
lowassa ndani ya ccm ni dume la mbegu!!!!wamuulize sophia simba na beatrice shellukindo!!!
Hata Mary Naggu, Hawa Ghasia, Anna Makinda, Pindi Chana, Zakia Meghji na Asharose Migiro wanakiri hivyo.
Huyu Lowassa kwa akina mama wa CCM kawashika pabaya sana. Hakuna mwanamama mwandamizi wa CCM anayeweza kufurukuta mbele ya Lowassa kisiasa. Hata Anna Kilango Mallecela ni suala la muda tu, soon atanyosha mikono.
 
Mi nataka lowassa ashinde urais,halafu cabinet yake ichnganywe na upinzqni ndio hii nchi itatengemaa,hii nchi inahitaji mtu mbabe na sio mropokaji ovyo na muuza meno.
 
CCM wameshaozea kukata majina sasa nangoea siku watakapokata jina la Jamaa njisi zahma itakavyokuwa -- so far wapo wana CCM 4 wanaoonyesha nia ya urais kwa tiket ya CCM
Nimewapanga kutokana na nguvu zao nje na ndani ya chama
1. Edward Lowassa
2. Samweli Sitta
3. Benald Membe
4. Lazaro Nyarandu

Wengine watakuwa wanatimiza idadi tu (making up the numbers)
Mkuu kwenye hiyo list hauko sawa sawa, huyo Lazaro Nyarandu hayuko kabisa(Anazuga tu na wala hana nguvu yoyote), kifupi yuko Kambi moja na Samwel Sitta ambayo pia yuko Mwakyembe.

List ni ndefu ila wenye nguvu ni watu wanne tu, na mpangilio uko kama ifuatavyo.
1/Edward Lowassa.
2/Benard Membe.
3/Samwel Sitta.
4/Mizengo Pinda.

Zipo kambi zingine ambazo ni hafifu sana kama ya Fredrick Sumaye, Abdallah Kigoda, John Magufuli(Inasemekana yupo kambi moja na Lowassa), Steven Wassira(Pia yuko kambi moja na Lowassa), Emanuel Nchimbi(Yupo kambi moja na Lowassa)
 
CCM wameshaozea kukata majina sasa nangoea siku watakapokata jina la Jamaa njisi zahma itakavyokuwa -- so far wapo wana CCM 4 wanaoonyesha nia ya urais kwa tiket ya CCM
Nimewapanga kutokana na nguvu zao nje na ndani ya chama
1. Edward Lowassa
2. Samweli Sitta
3. Benald Membe
4. Lazaro Nyarandu

Wengine watakuwa wanatimiza idadi tu (making up the numbers)
Mkuu kwenye hiyo list hauko sawa sawa, huyo Lazaro Nyarandu hayuko kabisa(Anazuga tu na wala hana nguvu yoyote), kifupi yuko Kambi moja na Samwel Sitta ambayo pia yuko Mwakyembe.

List ni ndefu ila wenye nguvu ni watu wanne tu, na mpangilio uko kama ifuatavyo.
1/Edward Lowassa.
2/Benard Membe.
3/Samwel Sitta.
4/Mizengo Pinda.

Zipo kambi zingine ambazo ni hafifu sana kama ya Fredrick Sumaye, Abdallah Kigoda, John Magufuli(Inasemekana yupo kambi moja na Lowassa), Steven Wassira(Pia yuko kambi moja na Lowassa), Emanuel Nchimbi(Yupo kambi moja na Lowassa)
 
Ni jambo la wazi kabisa kwa sasa kuwa kwa vyovyote vile itakavyokuwa Edward Lowassa ana nafasi kubwa sana kuwa mgombea urais wa CCM 2015.

Lowassa ambaye huenda ndiye mtu anayejulikana na watanzania wengi zaidi kama ni mwanaCCM mchafu(Fisadi) zaidi lakini Lowassa ndiye mwanaCCM mwenye nguvu zaidi ndani na nje ya CCM kwa sasa.
Binafsi mpaka sasa sioni namna yoyote kwa chama changu cha mapinduzi kama kinaweza kuepusha Lowassa asiwe mgombea urais wa CCM 2015.

Mikakati mbali mbali ya makusudi ndani ya serikali na CCM imefanyika tena kwa juhudi kubwa ili kumdhibiti Lowassa kisiasa kuanzia kushinikiza kujiuzuru kwake uwaziri mkuu kwa kashfa ya Ufisadi mpaka mkakati wa kujivua gamba na kuteua mara mbili secretariety mpya ya CCM lakini bado havikusaidia kitu.

Karibu kila kada mwandamizi ndani ya CCM imeshachoka kumdhibiti Lowassa na wapambe wake kisiasa na kwa sasa karibu kila kada wa CCM ambaye hampendi Lowassa ameanza kumwogopa sana au kujipendekeza. Mfano rahisi kabisa ni Nape Nnauye ambaye anaogopa kabisa kutaja hata neno Lowassa au Fisadi hadharani kwa sasa na Mwigulu Nchemba ambaye tayari 'ametangaza' kuwa yuko pamoja na Lowassa bega kwa bega katika mbio za urais.

Wakati Lowassa akizidi kuchanja mbuga katika mbio zake za urais kisiasa kupitia makundi mbalimbali ya kijamii na kidini, kambi zingine hasimu za urais ndani ya CCM zimechoka sana na wamebaki kulalamika, kunung'ung'unika na kuhangaika tu.
Kuanzia kambi ya Samweli Sitta, Benard Membe, Fredrick Sumaye nk. kwa sasa wanasubiri miujiza ya kisiasa pekee ndani ya CCM ili waweze kumshinda Lowassa.

Swali, CCM tumeshindwa kumdhibiti Lowassa?
Kwani wewe siku hizi umeacha kuwa mpiga debe wa heche pale bavicha umehamia ccm we si kundi moja na akina molemo,ben,vut- nkuvute sasa ya ccm umeyajuaje au yanakuhusu nini kama siyo umbea mtupu utasutwa.
 
Hata Mary Naggu, Hawa Ghasia, Anna Makinda, Pindi Chana, Zakia Meghji na Asharose Migiro wanakiri hivyo.
Huyu Lowassa kwa akina mama wa CCM kawashika pabaya sana. Hakuna mwanamama mwandamizi wa CCM anayeweza kufurukuta mbele ya Lowassa kisiasa. Hata Anna Kilango Mallecela ni suala la muda tu, soon atanyosha mikono.

Mkuu,Anne akiliango anyooshe mikono mara ngapi!!?
Kwisha habari yake
 
Mkuu kwenye hiyo list hauko sawa sawa, huyo Lazaro Nyarandu hayuko kabisa(Anazuga tu na wala hana nguvu yoyote), kifupi yuko Kambi moja na Samwel Sitta ambayo pia yuko Mwakyembe.

List ni ndefu ila wenye nguvu ni watu wanne tu, na mpangilio uko kama ifuatavyo.
1/Edward Lowassa.
2/Benard Membe.
3/Samwel Sitta.
4/Mizengo Pinda.

Zipo kambi zingine ambazo ni hafifu sana kama ya Fredrick Sumaye, Abdallah Kigoda, John Magufuli(Inasemekana yupo kambi moja na Lowassa), Steven Wassira(Pia yuko kambi moja na Lowassa), Emanuel Nchimbi(Yupo kambi moja na Lowassa)
mkuu niliambiwa na kigogo mmoja wa ccm kwamba sifa aliyonayo tyson (wassira) ni kutokuwa na makundi ndani ya chama na ndiyo maana wakampa kura nyingi sana kwenye mkutano wao na kumkabidhi kazi ya kuimaliza CDM ambayo juzi katangaza kwamba ni ngumu na imemshinda.

Sasa mbona wewe umemuweka kwenye makambi? una uhakika?
 
Mkuu kwenye hiyo list hauko sawa sawa, huyo Lazaro Nyarandu hayuko kabisa(Anazuga tu na wala hana nguvu yoyote), kifupi yuko Kambi moja na Samwel Sitta ambayo pia yuko Mwakyembe.

List ni ndefu ila wenye nguvu ni watu wanne tu, na mpangilio uko kama ifuatavyo.
1/Edward Lowassa.
2/Benard Membe.
3/Samwel Sitta.
4/Mizengo Pinda.

Zipo kambi zingine ambazo ni hafifu sana kama ya Fredrick Sumaye, Abdallah Kigoda, John Magufuli(Inasemekana yupo kambi moja na Lowassa), Steven Wassira(Pia yuko kambi moja na Lowassa), Emanuel Nchimbi(Yupo kambi moja na Lowassa)
Mbona hujamuongeza zito kabwe na tundu lisu fyatu naye yupo kambi hiyo.
 
Kwani wewe siku hizi umeacha kuwa mpiga debe wa heche pale bavicha umehamia ccm we si kundi moja na akina molemo,ben,vut- nkuvute sasa ya ccm umeyajuaje au yanakuhusu nini kama siyo umbea mtupu utasutwa.

Uncle Deo nahisi unachukia sana kuona mwanaCCM anakuja mtandaoni kuikosoa CCM na kuishauri pia.

Ila kukujibu tu, Mimi ni 'mwanaCCM' tena mwenye itikati za TANU ila silidhishwi kabisa na namna chama changu cha CCM kinavyoendeshwa na pia kinavyofanya siasa zake kwa sasa.

Turudi kwenye topic yetu, Swali, CCM tumemshindwa Lowassa?
 
Last edited by a moderator:
Mimi sioni malaika CCM.Binafsi napenda upinzani wachukue dola 2015.Ila iwapo kutakuwa na mizengwe yeyote ile basi Lowassa apewe na aunde serikali ya kitaifa wapinzani wawemo na mahasimu wa kisiasa watakaoridhia kama wapo.Visasi na urafiki havikubaliki..Katiba mpya hopefully itakuwepo hivyo yeyote awaye ajali maendeleo kwa kutumia vyema raslimali ns awe na uthubutu wa kukemea na kuchukua hatua stahiki.Chonde chonde hatutaki machafuko tujali chaguo la wananchi.Ila huko CCM patatoka kivumbi kwenye kinyanganyiro
 
[QUOTE=ZeMarcopolo;6939626
GENGE LA WAHUNI NA WAFADHIRI WA WAUZA UNGA CCM HUWA WANA VIKAO SAHIHI?
 
Back
Top Bottom