Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,883
- 6,402
Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi ya CCM na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Rajabu Maganya, amesema mchakato wa Katiba Mpya ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2030.
Maganya amesema mchakato huo hauwezi kukamilika ndani ya mwaka mmoja, lakini ameeleza kushangazwa na baadhi ya vyama vya siasa na watu wanaohamasisha wananchi kupigania Katiba Mpya kana kwamba imezuiwa.
"Ni nani aliyezuia Katiba Mpya? Ni nani amesema hakutakuwa na Katiba Mpya?" amehoji Maganya, akisisitiza kuwa Serikali na CCM hazijawahi kutangaza kuwa mchakato huo hautafanyika.
Maganya ametoa kauli hiyo leo, Julai 24, 2026, jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika eneo la Sinza, Wilaya ya Ubungo.
Soma Pia: Dkt. Nchimbi: Hakuna sheria inayotengua Katiba. Watanzania pambaneni kupata Katiba mpya
Kauli yake imeibua mjadala miongoni mwa Watanzania, ikitolewa siku ambayo Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Dkt. Emmanuel Nchimbi, pia alizungumzia suala la Katiba Mpya wakati wa Mkutano Mkuu wa 15 wa wanachama wa watetezi wa haki za binadamu uliofanyika leo, Julai 24, 2026.
Maganya amesema mchakato huo hauwezi kukamilika ndani ya mwaka mmoja, lakini ameeleza kushangazwa na baadhi ya vyama vya siasa na watu wanaohamasisha wananchi kupigania Katiba Mpya kana kwamba imezuiwa.
"Ni nani aliyezuia Katiba Mpya? Ni nani amesema hakutakuwa na Katiba Mpya?" amehoji Maganya, akisisitiza kuwa Serikali na CCM hazijawahi kutangaza kuwa mchakato huo hautafanyika.
Maganya ametoa kauli hiyo leo, Julai 24, 2026, jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika eneo la Sinza, Wilaya ya Ubungo.
Soma Pia: Dkt. Nchimbi: Hakuna sheria inayotengua Katiba. Watanzania pambaneni kupata Katiba mpya
Kauli yake imeibua mjadala miongoni mwa Watanzania, ikitolewa siku ambayo Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Dkt. Emmanuel Nchimbi, pia alizungumzia suala la Katiba Mpya wakati wa Mkutano Mkuu wa 15 wa wanachama wa watetezi wa haki za binadamu uliofanyika leo, Julai 24, 2026.