CCM siipendi Lowassa simwamini

bizplan

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2013
Posts
592
Reaction score
574
Wadau nipo nina waza na kuwazua. Kura yangu nampa nani. Najua ni siri yangu ila mpaka sasa sijajua kura yangu ya uraisi inaenda wapi.

Ubunge na Udiwani sina shida ila hiyoo ya urais. Sababu kuu ni kwamba CCM siipendi lakini Lowassa mgombea UKAWA simwamini.

Wanaoweza kunishawishi karibuni maana nina watu ninaweza washawishi nikishawishika.
 

Ushindwe kushawishiwa na wanasiasa huko majukwaani uje ushawishie hapa? Anyway kuna vyama vingine vingi tu UDP, ACT Wazalendo, TLP, n.k.
 
Km mie ila kubwa mama tz hivyo ukombozi kwanza ss mengine yatafuata ccm siitaki kabisa na Lowasa simpendi ila pombe anaingia hatiani kwa ajili hiyo tu
 

NItakupa hii kama wabunge 99% wameingia kwa rushwa kwenye kura ya maoni kupitia chama cha Magufuli,na tunaamini kati yao wabunge 66 watachaguliwa kuwa mawaziri/naibu mawaziri je VITA dhidi ya RUSHWA itapigwa kweli????
 
Uraisi ni taasisi na sio mtu. Taasisi ya kuaminika ni chadema
 

Yaan mawazo yako sawa na yangu 100% sema umeniwahi tu kulisema hili....
Na mameno uliyoyatumia ni yale yale.... mimi naongezea... ''namkubali magufuli lakin ccm yake siipendi na ni muumini/napenda mabadiliko"
 
NItakupa hii kama wabunge 99% wameingia kwa rushwa kwenye kura ya maoni kupitia chama cha Magufuli,na tunaamini kati yao wabunge 66 watachaguliwa kuwa mawaziri/naibu mawaziri je VITA dhidi ya RUSHWA itapigwa kweli????
Kama ni rushwa kwenye chaguzi za ndani hakuna wa kumcheka mwenzie kati ya ccm na Chadema.

Kwa huku niliko vilihitajika vikao vya ndani kumaliza migogoro na mizengwe kwenye chaguzi tena Hadi udiwani watu wamehonga sana kupitia Chadema.
 
Chagua Magufuli, binafsi nina imani anaenda fumua mfumo wa sisiemu wa sasa kwa sababu ya fundisho walilolipata sasa kuwa watu wanataka mabadiliko. Magufuli kama Magufuli ni mtu wa kumwamini, nikimuangalia machoni ni mtu anayemaanisha kitu anachokisema. Lowasa ameshaonesha kuwa hana msimamo.
CHAGUA JPM kwa ajili ya Tanzania mpya, Mwalimu JK alisema watanzania wasipopata mabadiliko ndani ya sisiemu basi watayatafuta hayo mabadiliko nje ya sisiemu, Maana yake uwezekano wa kupata hayo mabadiliko ndani ya sisiemu inawezekana, na ktk wagombea wote wa sisiemu waliopita, Mkapa alipigiwa debe na Nyerere, Kikwete alikuwa na nyota ya 'usupa star yaani kama rock star', watu walitokea tu kumpenda na pia slogan yake ya maisha bora kwa kila mtanzania iliamsha watu, ila kiukweli Kikwete alibebwa na 'usupa star', ILA HALI NI TOFAUTI KWA MAGUFULI, KAJIBEBA MWENYEWE NA HAMNA ALIYEMBEBA ASILIMIA KUBWA, WAKUBWA WENGI KAMA WARIOBA WANAOTUSHAWISHI TUMCHAGUE MAGUFULI NI KWA SABABU AMEONA NA TUMEONA UADILIFU WAKE NA UCHAPA KAZI WAKE, HII HAINA UBISHI PIA NI MCHA MUNGU, ANAMUOGOPA MUNGU HIVYO ASEMACHO ANAMAANISHA HATA KTK BODY LANGUAGE YAKE,
Ndugu yangu fanya maamuzi sahihi, chagua Magufuli.
 
Kanuni ya mafanikio maishani ni kujaribu kitu tofauti, na sasa tunapaswa kuchagua ukawa /Lowasa kwa vile ccm tumeshaogozwa nayo kwa miaka mingi tayari. Baada ya miaka tuseme kumi hivi tutawaondoa ukawa/cdm. Cha msingi kusiwe na chama kudumu madarakani
 
Nawashauri mchague lowasa ,ni heri umchague usiemwamini kuliko unaemchukia,na uzuri ushasema unataka mabadiliko na yapo chadema c ccm Mkuu ,kumbuka ni rahisi kufanya kazi na mtu usie mwamini kuliko usie mpenda!!
 

kweli magufuri body language imenishawishi sana kula Yangu atachukua ila huku chini wajipange!!!
 
Chagua Magufuli ndg. Usipoteze muda wako na wachaga hao.
 
Uraisi ni taasisi na sio mtu. Taasisi ya kuaminika ni chadema

CHADEMA haiaminiki tena, Lowassa alisema hatohama sisiemu kamwe baada ya kukatwa kahama, Sumaye alisema endapo sisiemu wangemsimamisha Lowassa kuwa mgombea urais, angeng'atuka kama mwanachama wa sisiemu, leo yule fisadi aliyesema yuko nae chama kimoja, na CHADEMA AMBAO WAMETUMIA ZAIDI YA MIAKA KUMI KUSEMA KUWA LOWASA NI FISADI, LEO WANASEMA SIO FISADI, hivyo CHADEMA ni taasisi ambayo inaweza ikatupa ahadi za kwenda kufanya jambo fulani ila watakapoingia ikulu wakafanya kinyume maana wameonesha kuwa hawana msimamo wote kuanzia Lowassa, sumaye, mbowe, Tundu lissu na chadema kwa ujumla, hawa sio wa kupewa nchi maana hawamaanishi wakisemacho, watauza nchi!
 
Nyerere alipoomba uhuru kwa waingereza aliwaambia watanganyika kua tunaomba uhuru kwa waingereza wasipo tupatia,tutamwomba mungu atusadie ,na tusipo pata tutamwomba hata shetani atusaidie mana shida yetu ni uhuru wa tanganyikaaa
 
endelea kutafakari... hivi ukiwa kwenye gari bovu likakwama utalisukuma ukiwa ndani yake au itabidi ushuke utafute lingine au fundi mpya akuasaidie.? unaonaje? umewahi kujiuliza kila baada ya miaka mitano unalipatia service, unapaka rangi , na mengine mengine, ukitegemea litafanya kazi yako vizuri afu ghafla limezimika na ndio safari imeanza utafanyaje? fungukeni . nunua gari jipya, hata kama ni used japan litakusukuma kuliko la muhindi kkooo.
 
Nyerere alipoomba uhuru kwa waingereza aliwaambia watanganyika kua tunaomba uhuru kwa waingereza wasipo tupatia,tutamwomba mungu atusadie ,na tusipo pata tutamwomba hata shetani atusaidie mana shida yetu ni uhuru wa tanganyikaaa

Nyerere alisimamia kauli zake na kuwaaminisha wa Tanzania kwa vitendo.
Sio hawa wapiga dili.
 

Nimekuelewa mkuu namii naamini katika hilo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…